< Psalmi 91 >

1 Ti što prebivaš pod zaštitom Višnjega, što počivaš u sjeni Svemogućega,
Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
2 reci Jahvi: “Zaklone moj! Utvrdo moja! Bože moj u koga se uzdam!”
Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
3 Jer on će te osloboditi od zamke ptičarske, od kuge pogubne.
Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
4 Svojim će te krilima zaštititi i pod njegova ćeš se krila skloniti: Vjernost je njegova štit i obrana!
Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
5 Nećeš se bojati strašila noćnoga ni strelice što leti danju,
Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
6 ni kuge što se šulja kroz tmine, ni pošasti što hara o podne.
wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
7 Pa nek' padaju tisuće kraj tebe, deseci tisuća s desne tvoje, tebi se neće primaći!
Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
8 Tek što okom pogledaš, već ćeš vidjeti plaću grešnika.
Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
9 Jer Jahve je zaklon tvoj, Višnjega odabra sebi za okrilje.
Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
10 Neće te snaći nesreća, nevolja se neće prikučiti šatoru tvojemu.
basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
11 Jer anđelima svojim zapovjedi da te čuvaju na svim putima tvojim.
Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
12 Na rukama će te nositi da se ne spotakneš o kamen.
Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
13 Nogom ćeš gaziti lava i ljuticu, zgazit ćeš lavića i zmiju.
Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
14 Izbavit ću ga jer me ljubi, zakrilit ga jer poznaje ime moje.
Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
15 Zazvat će me, a ja ću ga uslišiti, s njim ću biti u nevolji, spasit ću ga i proslaviti.
Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
16 Nasitit ću ga danima mnogim, pokazat' mu spasenje svoje.”
Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”

< Psalmi 91 >