< Psalmi 88 >

1 Pjesma. Psalam. Sinova Korahovih. Zborovođi. Po napjevu “Bolest”. Za pjevanje. Poučna pjesma. Ezrahijca Hemana. Jahve, Bože moj, vapijem danju, a noću naričem pred tobom.
Yahwe, Mungu wa wokovu wangu, ninalia mchana na usiku mbele zako.
2 Neka dopre do tebe molitva moja, prigni uho k vapaju mome.
Sikiliza maombi yangu; utazame kulia kwangu.
3 Jer mi je duša zasićena patnjama, moj se život bliži Podzemlju. (Sheol h7585)
Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni. (Sheol h7585)
4 Broje me k onima što u grob silaze, postadoh sličan nemoćniku.
Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
5 Među mrtvima moj je ležaj, poput ubijenih što leže u grobu kojih se više ne spominješ, od kojih si ustegao ruku.
Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
6 Smjestio si me u jamu duboku, u tmine, u bezdan.
Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.
7 Teško me pritišće ljutnja tvoja i svim me valima svojim prekrivaš.
Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. (Selah)
8 Udaljio si od mene znance moje, Óučini da im gnusan budem: zatvoren sam, ne mogu izaći.
Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
9 Od nevolje oči mi gasnu: vapijem tebi, Jahve, iz dana u dan, za tobom ruke pružam.
Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.
10 Zar na mrtvima činiš čudesa? Zar će sjene ustati i hvaliti tebe?
Je! utafanya miujiza kwa ajili ya wafu? Wale waliokufa watafufuka na kukusifu wewe? (Selah)
11 Zar se u grobu pripovijeda o tvojoj dobroti? O vjernosti tvojoj u Propasti?
Uaminifu wa agano lako utatangazwa kaburini? au uaminifu wako mahali pa wafu?
12 Zar se u tmini objavljuju čudesa tvoja i tvoja pravda u Zaboravu?
Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani? au haki yako katika mahali pa usahaulifu?
13 Ipak ja vapijem tebi, Jahve, prije jutra molitvom te pretječem.
Lakini ninakulilia wewe, Yahwe; wakati wa asubuhi maombi yangu huja kwako.
14 Zašto, Jahve, odbacuješ dušu moju? Zašto sakrivaš lice od mene?
Yahwe, kwa nini unanikataa? Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?
15 Bijedan sam i umirem već od dječaštva, klonuh noseći tvoje strahote.
Nimekuwa nikiteswa kila siku na hatihati ya kifo tangu ujana wangu. Nimeteseka dhidi ya hofu yako kuu; ninakata tamaa.
16 Preko mene prijeđoše vihori tvojega gnjeva, strahote me tvoje shrvaše,
Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu, na matendo yako ya kutisha yameniangamiza.
17 okružuju me kao voda sveudilj, optječu me svi zajedno.
Siku zote yananizingira mimi kama maji; yote yamenizunguka mimi.
18 Udaljio si od mene prijatelja i druga: mrak mi je znanac jedini.
Wewe umemuondoa kwangu kila rafiki na anijuaye. Na sasa anijuaye pekee ni giza.

< Psalmi 88 >