< Psalmi 80 >

1 Zborovođi. Po napjevu “Ljiljan svjedočanstva”. Asafov. Psalam. Pastiru Izraelov, počuj, ti što vodiš Josipa k'o stado ovaca! Ti što sjediš nad kerubima, zablistaj
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
2 pred Efrajimom, Benjaminom, Manašeom: probudi silu svoju, priteci nam u pomoć!
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
3 Bože, obnovi nas, razvedri lice svoje i spasi nas!
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
4 Jahve, Bože nad Vojskama, dokle ćeš plamtjeti, premda se moli narod tvoj?
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
5 Dokle ćeš nas hraniti kruhom suza i obilno pojiti suzama?
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
6 Dokle će se oko nas svađat' susjedi i rugat' nam se naši dušmani?
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
7 Bože nad Vojskama, obnovi nas, razvedri lice svoje i spasi nas!
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
8 Ti prenese čokot iz Egipta, pogane istjera, a njega zasadi.
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9 Ti mu tlo pripravi, i on pusti korijenje i napuni zemlju.
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10 Sjena mu prekri bregove, lozje mu k'o Božji cedrovi.
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11 Mladice svoje ispruži do mora i svoje ogranke do Rijeke.
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
12 Zašto si mu srušio ogradu da ga beru svi što putem prolaze,
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
13 da ga pustoši vepar iz šume, da ga pasu poljske zvijeri?
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
14 Vrati se, Bože nad Vojskama, pogledaj s neba i vidi, obiđi ovaj vinograd:
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
15 zakrili što zasadi desnica tvoja, sina kog za se odgoji!
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
16 Oni koji ga spališe i posjekoše nek' izginu od prijetnje lica tvojega!
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
17 Tvoja ruka nek' bude nad čovjekom desnice tvoje, nad sinom čovječjim kog za se odgoji!
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
18 Nećemo se više odmetnuti od tebe; poživi nas, a mi ćemo zazivati ime tvoje.
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
19 Jahve, Bože nad Vojskama, obnovi nas, razvedri lice svoje i spasi nas!
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.

< Psalmi 80 >