< Psalmi 78 >
1 Poučna pjesma. Asafova. Poslušaj, narode moj, moju nauku, prikloni uho riječima usta mojih!
Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 Otvorit ću svoja usta na pouku, iznijet ću tajne iz vremena davnih.
Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
3 Ono što čusmo i saznasmo, što nam kazivahu oci,
Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
4 nećemo kriti djeci njihovoj, predat ćemo budućem koljenu: slavu Jahvinu i silu njegovu i djela čudesna što ih učini.
Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
5 Svjedočanstvo podiže on u Jakovu, Zakon postavi u Izraelu, da ono što naredi ocima našim oni djeci svojoj objave,
Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
6 da sazna budući naraštaj, i sinovi koji će se roditi da djeci svojoj kazuju
Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
7 da u Boga ufanje svoje stave i ne zaborave djela Božjih, već da vrše zapovijedi njegove,
Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
8 kako ne bi bili, kao oci njihovi, naraštaj buntovan, prkosan - naraštaj srcem nestalan i duhom Bogu nevjeran.
Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
9 Sinovi Efrajimovi, ratnici s lukom, u dan bitke okrenuše leđa.
Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
10 Saveza s Bogom ne održaše i ne htjedoše hoditi po Zakonu njegovu.
Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
11 Zaboraviše na djela njegova, na čudesa koja im pokaza.
Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
12 Pred njihovim ocima činio je znakove u Egiptu, u Soanskom polju.
Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
13 On more razdijeli i njih prevede, vode kao nasip uzdiže.
Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
14 Danju ih vodio oblakom, a svu noć ognjem blistavim.
Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
15 U pustinji hrid prolomi i napoji ih obilno kao iz bezdana.
Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
16 Iz stijene izbi potoke te izvede vode k'o velike rijeke.
Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
17 A oni jednako griješiše, prkosiše Višnjem u pustinji.
Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
18 Boga su kušali u srcima svojim ištuć' (jela) svojoj pohlepnosti.
Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
19 Prigovarali su Bogu i pitali: “Može li Gospod stol u pustinji prostrti?
Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
20 Eno, udari u hrid, i voda poteče i provreše potoci: a može li dati i kruha, i mesa pružiti svome narodu?”
Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
21 Kad to začu Jahve, gnjevom usplamtje: oganj se raspali protiv Jakova, srdžba se razjari protiv Izraela,
Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
22 jer ne vjerovaše Bogu niti se u njegovu pomoć uzdaše.
kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
23 Pa ozgo naredi oblaku i otvori brane nebeske,
Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
24 k'o kišu prosu na njih mÓanu da jedu i nahrani ih kruhom nebeskim.
Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
25 Čovjek blagovaše kruh Jakih; on im dade hrane do sitosti.
Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
26 Probudi na nebu vjetar istočni i svojom silom južnjak dovede.
Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
27 Prosu na njih mesa k'o prašine i ptice krilatice k'o pijeska morskoga.
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
28 Padoše usred njihova tabora i oko šatora njihovih.
Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
29 Jeli su i nasitili se, želju njihovu on im ispuni.
Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
30 Još nisu svoju utažili pohlepu i jelo im još bješe u ustima,
Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
31 kad se srdžba Božja na njih raspali: pokosi smrću prvake njihove i mladiće pobi Izraelove.
Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
32 Uza sve to griješiše dalje i ne vjerovaše u čudesna djela njegova.
Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33 I skonča im dane jednim dahom i njihova ljeta naglim svršetkom.
Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34 Kad ih ubijaše, tražiše ga i opet pitahu za Boga;
Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
35 spominjahu se da je Bog hridina njihova i Svevišnji njihov otkupitelj.
Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
36 Ali ga opet ustima svojim varahu i jezikom svojim lagahu njemu.
Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
37 Njihovo srce s njime ne bijaše, nit' bijahu vjerni Savezu njegovu.
Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
38 A on im milosrdno grijeh praštao i nije ih posmicao; često je gnjev svoj susprezao da ne plane svom jarošću.
Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
39 Spominjao se da su pÓut i dah koji odlazi i ne vraća se više.
Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
40 Koliko mu prkosiše u pustinji i žalostiše ga u samotnom kraju!
Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
41 Sve nanovo iskušavahu Boga i vrijeđahu Sveca Izraelova
Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
42 ne spominjuć' se ruke njegove ni dana kad ih od dušmana izbavi,
Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
43 ni znakova njegovih u Egiptu, ni čudesnih djela u polju Soanskom.
alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
44 U krv im pretvori rijeke i potoke, da ne piju.
Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
45 Posla na njih obade da ih žderu i žabe da ih more.
Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
46 I predade skakavcu žetvu njihovu, i plod muke njihove žderaču.
Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
47 Vinograde im tučom udari, a mrazom smokvike njihove.
Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
48 I predade grÓadu njihova goveda i munjama stada njihova.
Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
49 Obori na njih svu žestinu gnjeva svog, jarost, bijes i nevolju: posla na njih anđele nesreće.
Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
50 I put gnjevu svojem otvori: ne poštedje im život od smrti, životinje im izruči pošasti.
Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
51 Pobi u Egiptu sve prvorođeno, prvence u šatorju Hamovu.
Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
52 I povede narod svoj kao ovce i vođaše ih kao stado kroz pustinju.
Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
53 Pouzdano ih je vodio te se nisu bojali, a more je prekrilo dušmane njihove.
Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
54 U Svetu zemlju svoju on ih odvede, na bregove što mu ih osvoji desnica.
Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
55 Pred njima istjera pogane, konopom im podijeli baštinu, pod šatorjem njihovim naseli plemena izraelska.
Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
56 A oni iskušavali i gnjevili Boga Višnjega i nisu držali zapovijedi njegovih.
Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
57 Otpadoše, iznevjeriše se k'o oci njihovi, k'o luk nepouzdan oni zatajiše.
Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
58 Na gnjev ga nagnaše svojim uzvišicama, na ljubomor navedoše kumirima svojim.
Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59 Bog vidje i gnjevom planu, odbaci posve Izraela.
Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60 I napusti boravište svoje u Šilu, Šator u kojem prebivaše s ljudima.
Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61 Preda u ropstvo snagu svoju i svoju diku u ruke dušmanske.
Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
62 Narod svoj prepusti maču, raspali se na svoju baštinu.
Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
63 Mladiće njihove oganj proguta, ne udaše se djevice njihove.
Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
64 Svećenici njihovi padoše od mača, ne zaplakaše Óudove njihove.
Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
65 Tad se k'o oda sna trgnu Gospodin, k'o ratnik vinom savladan.
Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
66 Udari otraga dušmane svoje, sramotu im vječitu zadade.
Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
67 On odbaci šator Josipov i Efrajimovo pleme ne odabra,
Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68 već odabra pleme Judino i goru Sion koja mu omilje.
Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
69 Sagradi Svetište k'o nebo visoko, k'o zemlju utemelji ga dovijeka.
Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
70 Izabra Davida, slugu svojega, uze ga od torova ovčjih;
Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
71 odvede ga od ovaca dojilica da pase Jakova, narod njegov, Izraela, baštinu njegovu.
Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
72 I pasao ih je srcem čestitim i brižljivim rukama vodio.
Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.