< Psalmi 68 >

1 Zborovođi. Davidov. Psalam. Pjesma. Bog nek' ustane! Razbježali se dušmani njegovi! Svi mrzitelji njegovi pobjegli pred njim!
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
2 Kao što dim iščezava, i njih neka nestane! Kako se vosak topi na ognju, nek' nestane grešnika pred licem Božjim!
Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
3 Pravedni neka se raduju, neka klikću pred Bogom, neka kliču od radosti.
Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
4 Pjevajte Bogu, slavite mu ime! Poravnajte put onome koji ide pustinjom - kojemu je ime Jahve - i kličite pred njim!
Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
5 Otac sirota, branitelj udovica, Bog je u svom svetom šatoru.
Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
6 Napuštene okućit će Jahve, sužnjima pružit' sretnu slobodu: buntovnici samo ostaše u sažganoj pustinji.
Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
7 Kad si stupao, Bože, pred narodom svojim, dok si prolazio pustinjom,
Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
8 tresla se zemlja, nebo se rosilo pred Bogom, Sinaj drhtao pred Bogom, Bogom Izraela.
dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
9 Blagoslovljen dažd pustio si, Bože, na baštinu svoju, okrijepio je umornu.
Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
10 Stado se tvoje nastani u njoj, u dobroti, Bože, ti je spremi siromahu.
Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
11 Jahve riječ zadaje, veliko je mnoštvo radosnih vjesnika:
Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
12 kraljevi vojska bježe te bježe, domaćice plijen dijele.
“Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
13 Dok vi počivaste među stadima, krila golubice zablistaše srebrom, a njeno perje žućkastim zlatom:
Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
14 ondje Svemogući razbijaše kraljeve, a ona poput snijega zablista na Salmonu.
Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
15 Božanska je gora gora bašanska vrletna.
Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
16 Zašto vi, gore vrletne, zavidno gledate na goru gdje se svidje Bogu prebivati? Jahve će na njoj boraviti svagda!
Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
17 Božja su kola bezbrojna, tisuću tisuća: Jahve sa Sinaja u Svetište dolazi!
Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
18 Na visinu uzađe vodeći sužnje, na dar si ljude primio, pa i one što ne žele prebivati kod Boga.
Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
19 Blagoslovljen Jahve dan za danom, nosi nas Bog, naš Spasitelj.
Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
20 Bog naš jest Bog koji spasava, Jahve od smrti izbavlja.
Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
21 Zaista, Bog će satrti glave dušmana svojih, kuštravo tjeme onog što hodi u grijesima.
Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
22 Reče Gospodin: “Iz Bašana ću ih dovesti, dovest ću ih iz dubine mora,
Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
23 da okupaš nogu u krvi, da jezici tvojih pasa imadnu dio od dušmana.”
ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
24 Ulazak ti, Bože, gledaju, ulazak moga Boga i Kralja u Svetište:
Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
25 sprijeda pjevači, za njima svirači, u sredini djevojke s bubnjićima.
Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
26 “U svečanim zborovima slavite Boga, slavite Jahvu, sinovi Izraelovi!”
Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
27 Predvodi ih najmlađi, Benjamin, koji ide pred njima, ondje su knezovi Judini sa četama svojim, knezovi Zebulunovi i knezovi Naftalijevi.
Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
28 Pokaži, Bože, silu svoju, silu kojom se, Bože, boriš za nas
Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
29 iz Hrama svojega u Jeruzalemu! Nek' ti kraljevi darove donose!
Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
30 Ukroti neman u trsci, stado bikova s teladi naroda! Neka se prostru pred tobom sa srebrnim žezlima: rasprši narode koji se ratu vesele!
Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
31 Nek' dođu velikani iz Egipta, Etiopija nek' pruži ruke Bogu!
Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
32 Sva kraljevstva svijeta, pjevajte Bogu, slavite Jahvu,
Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
33 koji se vozi po nebu, po nebu iskonskom! Čuj, glasom grmi, glasom svojim silnim:
mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
34 “Priznajte silu Božju!” Nad Izraelom veličanstvo njegovo, u oblacima (sila) njegova!
Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
35 Strašan je Bog iz svojega Svetišta. Bog Izraelov daje moć i silu narodu svojemu. Blagoslovljen Bog!
Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!

< Psalmi 68 >