< Psalmi 50 >

1 Psalam. Asafov. Bog nad bogovima, Jahve, govori i zove zemlju od izlaza sunčeva do zalaza.
Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
2 Sa Siona predivnog Bog zablista:
Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
3 Bog naš dolazi i ne šuti. Pred njim ide oganj što proždire, oko njega silna bjesni oluja.
Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
4 On zove nebesa odozgo i zemlju da sudi narodu svojemu:
Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
5 “Saberite mi sve pobožnike koji žrtvom Savez sa mnom sklopiše!”
“Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
6 Nebesa objavljuju pravednost njegovu: on je Bog sudac!
Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
7 “Slušaj, narode moj, ja ću govoriti, o Izraele, svjedočit ću protiv tebe: ja, Bog - Bog tvoj!
“Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
8 Ne korim te zbog žrtava tvojih - paljenice su tvoje svagda preda mnom.
Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
9 Neću od doma tvog' uzet junca, ni jaraca iz tvojih torova:
Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
10 tÓa moje su sve životinje šumske, tisuće zvjeradi u gorama mojim.
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
11 Znam sve ptice nebeske, moje je sve što se miče u poljima.
Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
12 Kad bih ogladnio, ne bih ti rekao, jer moja je zemlja i sve što je ispunja.
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
13 Zar da ja jedem meso bikova ili da pijem krv jaraca?
Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
14 Prinesi Bogu žrtvu zahvalnu, ispuni Višnjemu zavjete svoje!
Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
15 I zazovi me u dan tjeskobe: oslobodit ću te, a ti ćeš me slaviti.”
na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
16 A grešniku Bog progovara: “Što tumačiš naredbe moje, što mećeš u usta Savez moj?
Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
17 Ti, komu stega ne prija, te riječi moje iza leđa bacaš?
Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
18 Kad tata vidiš, s njime se bratimiš i družiš se s preljubnicima.
Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
19 Svoja si usta predao pakosti, a jezik ti plete prijevare.
Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
20 U društvu na brata govoriš i kaljaš sina matere svoje.
Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
21 Sve si to činio, a ja da šutim? Zar misliš da sam ja tebi sličan? Pokarat ću te i stavit ću ti sve to pred oči.”
Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
22 Shvatite ovo svi vi koji Boga zaboraviste, da vas ne pograbim i nitko vas spasiti neće.
“Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
23 Pravo me štuje onaj koji prinosi žrtvu zahvalnu: i onomu koji hodi stazama pravim - njemu ću pokazati spasenje svoje.
Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”

< Psalmi 50 >