< Psalmi 48 >
1 Pjesma. Psalam. Sinova Korahovih. Velik je Jahve, hvale predostojan u gradu Boga našega.
Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
2 Sveto brdo njegovo, brijeg veličanstven, radost je zemlji svoj. Gora Sion, na krajnjem sjeveru, grad je Kralja velikog.
Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
3 Bog u kulama njegovim jakom se pokaza utvrdom.
Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
4 Jer gle, složiše se kraljevi, navališe zajedno.
Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
5 Čim vidješe, zapanjiše se i zbunjeni u bijeg nagnuše.
Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
6 Ondje ih trepet obuze kao muka porodilje,
Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
7 kao kad vjetar istočni razbija brodove taršiške.
Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
8 Što smo čuli, sada vidimo: grad Jahve nad Vojskama, grad Boga našega - Bog ga utvrdi dovijeka.
Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
9 Spominjemo se, Bože, tvoje dobrote usred Hrama tvojega.
Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
10 Kao ime tvoje, Bože, tako i slava tvoja do nakraj zemlje doseže. Puna je pravde desnica tvoja; neka se raduje brdo sionsko!
Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
11 Neka kliču gradovi Judini zbog tvojih sudova!
Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
12 Obiđite Sion i prođite njime, prebrojite kule njegove!
Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
13 Pogledajte dobro bedeme njegove, promotrite mu potanko dvorove: da biste kazivali budućem koljenu:
mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
14 “Takav je Bog, Bog naš zasvagda i dovijeka! On neka nas vodi!”
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.