< Psalmi 37 >

1 Davidov. ALEF Nemoj se žestiti na opake, zavidjet nemoj pakosnicima:
Usikereshwe na wafanyao maovu; usiwaonee wivu wale watendao yasiyo haki.
2 kao trava brzo se osuše, k'o mlada zelen brzo uvenu.
Kwa kuwa muda mfupi watakauka kama nyasi na kukauka kama vile mimea ya kijani ikaukavyo wakati wa kiangazi.
3 BET U Jahvu se uzdaj i čini dobro, da smiješ stanovati u zemlji i živjeti u miru.
Uwamini Mungu na kufanya yaliyo mema; uishi katika nchi na uongezeke katika imani.
4 Sva radost tvoja neka bude Jahve: on će ispuniti želje tvoga srca!
Kisha ufurahi mwenyewe katika Yahwe, naye atakupa matamanio ya moyo wako.
5 GIMEL Prepusti Jahvi putove svoje, u njega se uzdaj i on će sve voditi.
Umkabidhi njia zako Yahwe; uamini katika yeye, naye atatenda kwa niaba yako.
6 Pravda će tvoja zasjati k'o svjetlost i tvoje pravo k'o sunce podnevno.
Yeye ataidhihilisha haki yako kama mchana na usafi wako kama mwangaza wa mchana.
7 DALET Smiri se pred Jahvom i njemu se nadaj, ne žesti se na onog koji ima sreće, na čovjeka koji spletke kuje.
Uwe kumya mbele za Yahwe na umsubiri yeye kwa uvumilivu. Usikasirike ikiwa kuna mtu anafanikiwa kwa kile afanyacho, au afanyapo njama za uovu.
8 HE Stišaj svoj gnjev i ostavi se srdžbe, ne žesti se da zlo ne učiniš.
Usikasilile na kugadhabika. Usiogope. Hii huleta matatizo tu.
9 Jer će biti satrti zlikovci, a koji se u Jahvu uzdaju, baštinit će zemlju.
Watendao maovu watafutiliwa mbali, bali wale wamngojao Yahwe watairithi nchi.
10 VAU Još malo i nestat će bezbožnika: mjesto ćeš njegovo tražiti, a njega više nema.
Katika muda mfupi mtu mwovu atatoweka; wewe utatazama mahali pake, wala hautamuona.
11 Zemlju će posjedovati krotki, obilje mira oni će uživat'.
Lakini wapole watairithi nchi nao watafurahia katika mafanikio makubwa.
12 ZAJIN Bezbožnik smišlja zlo pravedniku i zubima škrguće na njega.
Mtu mwovu hupanga njama kinyume na mwenye haki na kumsagia meno.
13 A Gospod se njemu smije jer vidi da dan njegov dolazi.
Bwana humcheka, kwa maana anaona siku yake inakuja.
14 HET Mač potežu bezbošci i zapinju lukove da obore jadnika i siromaha, da pokolju one koji hode pravim putem.
Waovu wametoa nje panga zao na wametayarisha pinde zao ili kuwaangamiza wanyonge na wahitaji, na kuwaua wenye haki.
15 Mačem će vlastito srce probiti, slomit će se njihovi lukovi.
Panga zao zitawaua wenyewe, na pinde zao zitavunjika.
16 TET Bolje je i malo u pravednika no golemo blago u zlotvora:
Ni bora kuwa mwenye haki maskini kuliko tajiri mwenye mali nyingi.
17 jer će se ruke zlotvora slomiti, a Jahve je oslon pravedniku.
Kwa maana mikono ya watu waovu itavunjika, bali Yahwe huwasaidia watu wenye haki.
18 JOD Jahve se brine za život čestitih, dovijeka će trajati baština njihova.
Yahwe huwalinda watu wasio na lawama siku hadi siku, na urithi wao utakuwa wa milele.
19 Neće se postidjeti u vrijeme nevolje, bit će siti u danima gladi.
Hawata aibika siku mbaya zijapo. Wakati wa njaa ufikapo wao watakuwa na chakula cha kutosha.
20 KAF A bezbožnici će propasti, dušmani Jahvini povenut će k'o ures livada, poput dima se rasplinuti.
Bali waovu wataangamia. Maadui wa Yahwe watakuwa kama vile utukufu wa malisho; watamalizwa na kupotezwa katika moshi.
21 LAMED Bezbožnik zaima, ali ne vraća, pravednik se sažaljeva i daje.
Mtu mwovu hukopa lakini halipi, bali mtu mwenye haki ni mkarimu na hutoa.
22 Oni koje Jahve blagoslovi baštinit će zemlju, a koje prokune bit će zatrti.
Wale walio barikiwa na Mungu watairithi nchi; wale aliowalaani watafutiliwa mbali.
23 MEM Jahve vodi i učvršćuje korake čovjeku i mio mu je put njegov.
Hatua za mwanadamu zinaimarishwa na Yahwe, mtu ambaye njia zake zinakubalika machoni pa Mungu.
24 Ako i posrne, ne pada jer ga Jahve drži za ruku.
Ajapojikwaa, hataanguka chini, kwa kuwa Yahwe anamshikilia kwa mkono wake.
25 NUN Mlad bijah i ostarjeh, al' ne vidjeh pravednika napuštena ili da mu djeca kruha prose.
Nilikuwa kijana na sasa ni mzee; sijawahi kumuona mtu mwenye haki ametelekezwa wala watoto wake kuombaomba mkate.
26 Uvijek je milosrdan i u zajam daje, na njegovu je potomstvu blagoslov.
Wakati wote yeye ni mkarimu na hukopesha, nao watoto wake hufanyika baraka.
27 SAMEK Zla se kloni i čini dobro, i ostat ćeš dovijeka.
Acha uovu na ufanye yaliyo mema; ndipo utakapokuwa salama milele.
28 Jer Jahve ljubi pravdu i pobožnika svojih ne ostavlja. AJIN Zauvijek će biti zatrti zlikovci, istrijebit će se potomstvo bezbožnika.
Kwa maana Yahwe hupenda haki naye hawaachi wafuasi waaminifu. Wao hutunzwa milele, lakini uzao wa waovu utafutiliwa mabli.
29 Zemlju će posjedovati pravednici i živjet će na njoj dovijeka.
Wenye haki watairithi nchi na kuaa huko milele.
30 PE Pravednikova usta mudrost kazuju, a jezik njegov govori pravo.
Mdomo wa mwenye haki huongea hekima na huongeza haki.
31 Zakon mu je Božji u srcu, ne kolebaju se koraci njegovi.
Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake; miguu yake haitelezi.
32 SADE Bezbožnik vreba pravednoga i smišlja da ga usmrti.
Mtu mwovu humvizia mwenye haki na kutafuta kumuua.
33 Jahve ga neće ostaviti u njegovoj vlasti i neće dopustiti da ga na sudu osude.
Yahwe hatamuacha yeye kwenye mkono wa mtu mwovu wala kumlaumu atakapohukumiwa.
34 KOF U Jahvu se uzdaj i drži se puta njegova: on će te uzvisit' i baštinit ćeš zemlju; radostan ćeš gledati propast bezbožnih.
Umngoje Yahwe na uishike njia yake, naye atakuinua uimiliki nchi. Atakapo waondosha waovu wewe utaona.
35 REŠ Vidjeh obijesna zlotvora gdje se k'o cedar krošnjat širi.
Nimewaona waovu na mtu wa kutisha akienea kama mti wa kijani katika udongo wa asili.
36 Prođoh, i gle - nema ga više; potražih ga i ne nađoh.
Lakini nilipopita tana mara nyingine, hakuwepo pale. nilimtafuta, lakini sikumpata.
37 ŠIN Promatraj čestita i gledaj neporočna: mirotvorac ima potomstvo.
Uwachunguze watu waadilifu, na uwatambue wenye haki; kuna hatima nzuri kwa ajili ya mtu wa amani.
38 A grešnici bit će svi iskorijenjeni, istrijebit će se zlikovačko sjeme.
Mwenye dhambi wataharibiwa kabisa; hatima ya mtu mwovu ni kuondoshwa.
39 TAU Od Jahve dolazi spas pravednicima, on im je zaklon u vrijeme nevolje.
Wokovu wa haki unatoka kwa Yahwe; yeye huwalinda wao nyakati za shida.
40 Jahve im pomaže, on ih izbavlja: on će ih izbaviti od zlotvora i spasiti, jer u njemu traže okrilje.
Yahwe huwasaidia na kuwaokoa. Yeye huwaokoa dhidi ya watu waovu na kuwanusuru wao kwa sababu wao wamemkimbilia yeye kwa ajili ya usalama.

< Psalmi 37 >