< Psalmi 33 >

1 Pravednici, Jahvi kličite! Hvaliti ga pristoji se čestitima.
Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
2 Slavite Jahvu na harfi, na liri od deset žica veličajte njega!
Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
3 Pjesmu novu zapjevajte njemu i glazbala skladna popratite poklicima.
Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
4 Jer prÓava je riječ Jahvina i vjernost su sva djela njegova.
Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
5 On ljubi pravdu i pravo: puna je zemlja dobrote Jahvine.
Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
6 Jahvinom su riječju nebesa sazdana i dahom usta njegovih sva vojska njihova.
Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
7 Vodu morsku on sabire kao u mješinu i bezdane stavlja u spremišta.
Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
8 Zemlja sva neka pred Jahvom strepi, neka ga se boje svi stanovnici svijeta!
Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
9 Jer on reče - i sve postade, naredi - i sve se stvori.
Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
10 Jahve razbija nakane pucima, mrsi namjere narodima.
Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
11 Naum Jahvin dovijeka ostaje i misli srca njegova od koljena do koljena.
Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
12 Blago narodu kojemu je Jahve Bog, Narodu koji on odabra sebi za baštinu!
Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
13 Gospodin motri s nebesa i gleda sve sinove čovječje.
Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
14 Iz svoga prebivališta motri sve stanovnike zemaljske:
kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
15 on je svima srca stvorio i pazi na sva djela njihova.
yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
16 Ne spasava kralja vojska mnogobrojna, ne spasava velika (sila) junaka.
Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
17 Isprazno se od konja nadati spasenju, jačina njegova ne izbavlja.
Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
18 Oko je Jahvino nad onima koji ga se boje, nad onima koji se uzdaju u milost njegovu:
Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
19 da im od smrti život spasi, da ih hrani u danima gladi.
ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
20 Naša se duša Jahvi nada, on je pomoć i zaštita naša.
Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
21 Srce nam se u njemu raduje, u njegovo sveto ime mi se uzdamo.
Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
22 Neka dobrota tvoja, o Jahve, bude nad nama, kao što se mi u tebe uzdamo!
Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.

< Psalmi 33 >