< Psalmi 24 >
1 Psalam. Davidov. Jahvina je zemlja i sve na njoj, svijet i svi koji na njemu žive.
Nchi ni ya Yahwe, na vyote viijazavyo, dunia, na wote wakaao ndani yake.
2 On ga na morima utemelji i na rijekama učvrsti.
Kwa kuwa yeye aliianzisha juu ya bahari na kuiimarisha juu ya mito.
3 Tko će uzići na Goru Jahvinu, tko će stajati na svetom mjestu njegovu?
Ni nani atakaye panda mlima wa Yahwe? Ni nani atakaye simama patakatifu pake?
4 Onaj u koga su ruke čiste i srce nedužno: duša mu se ne predaje ispraznosti, i ne kune se varavo.
Yeye ambaye ana mikono misafi na moyo safi; ambaye hajauinua uongo, na haja apa kiapo ili kudanganya.
5 On blagoslov prima od Jahve i nagradu od Boga, Spasitelja svoga.
Yeye atapokea baraka kutoka kwa Yahwe na haki kutoka kwa Mungu wa wokovu wake.
6 Takav je naraštaj onih koji traže njega, koji traže lice Boga Jakovljeva.
Kizazi cha wale wamtafutao Mungu ni kama hiki, wale ambao wanautafuta uso wa Mungu wa Yakobo.
7 “Podignite, vrata, nadvratnike svoje, dižite se, dveri vječne, da uniđe Kralj slave!”
Inueni vichwa vyenu, ninyi malango; muinuliwe juu, milango ya milango ya kudumu, ili kwamba Mfalme wa utukufu aweze kuingia!
8 “Tko je taj Kralj slave?” “Jahve silan i junačan, Jahve silan u boju!”
Huyu Mfalme wa utukufu ni nani? Yahwe, mwenye nguvu na uweza; Yahwe, mwenye uweza katika vita.
9 “Podignite, vrata, nadvratnike svoje dižite se, dveri vječne, da uniđe Kralj slave!”
Inueni vichwa vyenu, ninyi malango; muinuliwe juu, milango ya kudumu, ili kwamba Mfalme wa utukufu aweze kuingia!
10 “Tko je taj Kralj slave?” “Jahve nad Vojskama - on je Kralj slave!”
Huyu Mfalme wa utukufu ni nani? Yahwe wa majeshi, yeye ni Mfalme wa utukufu.