< Psalmi 132 >

1 Hodočasnička pjesma.
Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
2 Spomeni se, o Jahve, Davida i sve revnosti njegove: kako se Jahvi zakleo, zavjetovao Snazi Jakovljevoj:
Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
3 “Neću ući u šator doma svog nit' uzaći na ležaj svoje postelje,
“Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
4 neću pustit' snu na oči nit' počinka dati vjeđama,
sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
5 dok Jahvi mjesto ne nađem, boravište Snazi Jakovljevoj.”
mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
6 Eto, čusmo za nj u Efrati, nađosmo ga u Poljima jaarskim.
Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
7 Uđimo u stan njegov, pred noge mu padnimo!
“Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
8 “Ustani, o Jahve, pođi k svom počivalištu, ti i Kovčeg sile tvoje!
inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
9 Svećenici tvoji nek' se obuku u pravednost, pobožnici tvoji nek' radosno kliču!
Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
10 Poradi Davida, sluge svojega, ne odvrati lica od svog pomazanika!”
Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
11 Jahve se zakle Davidu zakletvom tvrdom od koje neće odustati: “Potomka tvoje utrobe posadit ću na prijestolje tvoje.
Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
12 Budu li ti sinovi Savez moj čuvali i naredbe kojima ih učim, i sinovi će njini dovijeka sjedit' na tvom prijestolju.”
kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
13 Jer Jahve odabra Sion, njega zaželje sebi za sjedište.
Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
14 “Ovo mi je počivalište vječno, boravit ću ovdje jer tako poželjeh.
“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
15 Žitak ću njegov blagosloviti, siromahe nahraniti kruhom.
Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
16 Svećenike njegove u spas ću odjenuti, sveti će njegovi kliktati radosno.
Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
17 Učinit ću da ondje za Davida rog izraste, pripravit ću svjetiljku za svog pomazanika.
“Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
18 U sram ću mu obući dušmane, a na njemu će blistat' vijenac moj.”
Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”

< Psalmi 132 >