< Psalmi 118 >

1 Aleluja! Zahvaljujte Jahvi jer je dobar, jer je vječna ljubav njegova!
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 Neka rekne dom Izraelov: “Vječna je ljubav njegova!”
Israeli na aseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
3 Neka rekne dom Aronov: “Vječna je ljubav njegova!”
Nyumba ya Aroni na iseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
4 Svi koji se Jahve boje neka reknu: “Vječna je ljubav njegova!”
Wote wamchao Bwana na waseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
5 Iz tjeskobe Jahvu ja zazvah: on me usliša i oslobodi.
Wakati wa maumivu yangu makuu nilimlilia Bwana, naye akanijibu kwa kuniweka huru.
6 Jahve je sa mnom i ja ne strahujem: što mi tko može?
Bwana yuko pamoja nami, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
7 Jahve je sa mnom, pomoć moja, i zbunjene gledam dušmane.
Bwana yuko pamoja nami, yeye ni msaidizi wangu. Nitawatazama adui zangu wakiwa wameshindwa.
8 Bolje se Jahvi uteći nego se uzdat' u čovjeka.
Ni bora kumkimbilia Bwana kuliko kumtumainia mwanadamu.
9 Bolje se Jahvi uteći nego se uzdat' u mogućnike.
Ni bora kumkimbilia Bwana kuliko kuwatumainia wakuu.
10 Pogani me okružiše: imenom ih Jahvinim uništih.
Mataifa yote yalinizunguka, lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
11 Opkoliše me odasvud: imenom ih Jahvinim uništih.
Walinizunguka pande zote, lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
12 Opkoliše me poput pčela, ubod im žeže kao trnje zapaljeno: imenom ih Jahvinim uništih.
Walinizunguka kama kundi la nyuki, lakini walikufa haraka kama miiba iteketeayo; kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
13 Gurahu me, gurahu, da me obore, ali mi Jahve pomože.
Nilisukumwa nyuma karibu kuanguka, lakini Bwana alinisaidia.
14 Jahve je moja snaga i pjesma, on mi je spasitelj.
Bwana ni nguvu yangu na wimbo wangu, yeye amefanyika wokovu wangu.
15 Čuj! Radost i spasenje odzvanja šatorima pravednika: Jahvina se proslavi desnica,
Sauti za shangwe na ushindi zinavuma hemani mwa wenye haki: “Mkono wa kuume wa Bwana umetenda mambo makuu!
16 Jahvina me uzdigne desnica, Jahvina se proslavi desnica!
Mkono wa kuume wa Bwana umeinuliwa juu, mkono wa kuume wa Bwana umetenda mambo makuu!”
17 Ne, umrijeti neću nego živjeti i kazivat ću djela Jahvina.
Sitakufa, bali nitaishi, nami nitatangaza yale Bwana aliyoyatenda.
18 Kaznom teškom kaznio me Jahve, ali me smrti ne preda.
Bwana ameniadhibu vikali, lakini hakuniacha nife.
19 Otvorite mi širom vrata pravde: ući ću, Jahvi zahvalit'!
Nifungulie malango ya haki, nami nitaingia na kumshukuru Bwana.
20 “Ovo su vrata Jahvina, na njih ulaze pravedni!”
Hili ni lango la Bwana ambalo wenye haki wanaweza kuliingia.
21 Zahvalit ću ti što si me uslišio i moj postao spasitelj.
Nitakushukuru, kwa kuwa ulinijibu, umekuwa wokovu wangu.
22 Kamen što ga odbaciše graditelji postade kamen zaglavni.
Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni.
23 Jahvino je to djelo: kakvo čudo u očima našim!
Bwana ametenda hili, nalo ni la kushangaza machoni petu.
24 Ovo je dan što ga učini Jahve: kličimo i radujmo se njemu!
Hii ndiyo siku Bwana aliyoifanya, tushangilie na kufurahi ndani yake.
25 O Jahve, spasenje nam daj! Jahve, sreću nam daj!
Ee Bwana, tuokoe, Ee Bwana, utujalie mafanikio.
26 Blagoslovljen koji dolazi u imenu Jahvinu! Blagoslivljamo vas iz Doma Jahvina!
Heri yule ajaye kwa jina la Bwana. Kutoka nyumba ya Bwana tunakubariki.
27 Obasjao nas Bog Jahve! Složite povorku s grančicama u ruci sve do rogova žrtvenika.
Bwana ndiye Mungu, naye ametuangazia nuru yake. Mkiwa na matawi mkononi, unganeni kwenye maandamano ya sikukuu hadi kwenye pembe za madhabahu.
28 Ti si Bog moj - tebi zahvaljujem: Bože moj, tebe ja uzvisujem.
Wewe ni Mungu wangu, nitakushukuru, wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza.
29 Zahvaljujte Jahvi jer je dobar, jer je vječna ljubav njegova!
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.

< Psalmi 118 >