< Psalmi 105 >
1 Hvalite Jahvu, prizivajte mu ime, navješćujte među narodima djela njegova!
Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake, wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
2 Pjevajte mu, svirajte mu, pripovijedajte sva njegova čudesa!
Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa, waambieni matendo yake yote ya ajabu.
3 Dičite se svetim imenom njegovim, neka se raduje srce onih što traže Jahvu!
Lishangilieni jina lake takatifu, mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
4 Tražite Jahvu i njegovu snagu, tražite svagda njegovo lice!
Mtafuteni Bwana na nguvu zake, utafuteni uso wake siku zote.
5 Sjetite se čudesa koja učini, njegovih čuda i sudova usta njegovih!
Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
6 Abrahamov rod sluga je njegov, sinovi Jakovljevi njegovi izabranici!
enyi wazao wa Abrahamu mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
7 On je Jahve, Bog naš; po svoj su zemlji njegovi sudovi!
Yeye ndiye Bwana Mungu wetu, hukumu zake zimo duniani pote.
8 On se uvijek sjeća svojega Saveza, riječi koju dade tisući naraštaja:
Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
9 Saveza koji sklopi s Abrahamom i zakletve svoje Izaku.
agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
10 Ustanovi je kao zakon Jakovu, Izraelu vječni Savez,
Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
11 govoreći: “Tebi ću dati kanaansku zemlju kao dio u baštinu vašu.”
“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
12 Kad ih još bješe malo na broju, vrlo malo, i kad bjehu pridošlice u njoj,
Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
13 išli su od naroda do naroda, iz jednoga kraljevstva k drugom narodu,
walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
14 ali ne dopusti nikom da ih tlači, kažnjavaše zbog njih kraljeve:
Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
15 “Ne dirajte u moje pomazanike, ne nanosite zla mojim prorocima!”
“Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
16 I on pozva glad na zemlju, sve zalihe uništi krušne.
Akaiita njaa juu ya nchi na kuharibu chakula chao chote,
17 Pred njima čovjeka posla: Josip u ropstvo bijaše prodan.
naye akatuma mtu mbele yao, Yosefu, aliyeuzwa kama mtumwa.
18 Sputaše uzama noge njegove, u gvožđe mu vrat staviše,
Walichubua miguu yake kwa minyororo, shingo yake ilifungwa kwa chuma,
19 dok se ne ispuni proroštvo njegovo, Jahvina ga riječ potvrdi.
hadi yale aliyotangulia kusema yalipotimia, hadi neno la Bwana lilipomthibitisha.
20 Kralj naredi da ga driješe, narÄodÄa poglavar oslobodi njega.
Mfalme alituma watu wakamfungua, mtawala wa watu alimwachia huru.
21 Za domaćina ga stavi kući svojoj, za nadstojnika sveg imanja svoga,
Alimfanya mkuu wa nyumba yake, mtawala juu ya vyote alivyokuwa navyo,
22 da velikaše njegove po volji uči i starce njegove mudrosti da vodi.
kuwaelekeza wakuu wa mfalme apendavyo na kuwafundisha wazee wake hekima.
23 Tad Izrael u Egipat uđe, Jakov došljak bješe u Kamovoj zemlji.
Kisha Israeli akaingia Misri, Yakobo akaishi kama mgeni katika nchi ya Hamu.
24 Narod svoj umnoži veoma, učini ga jačim od dušmana.
Bwana aliwafanya watu wake kuzaana sana, akawafanya kuwa wengi sana kuliko adui zao,
25 Okrenu im srce da zamrze narod njegov, da slugama njegovim opaki budu.
ndiye aliigeuza mioyo yao iwachukie watu wake, wakatenda hila dhidi ya watumishi wake.
26 Mojsija posla, slugu svoga, Arona, kog odabra.
Akamtuma Mose mtumishi wake, pamoja na Aroni, aliyemchagua.
27 Činjahu među njima znake njegove i čudesa u Kamovoj zemlji.
Walifanya ishara zake za ajabu miongoni mwao, miujiza yake katika nchi ya Hamu.
28 Posla tmine, i smrknu se, al' prkosiše oni riječima njegovim.
Alituma giza na nchi ikajaa giza, kwani si walikuwa wameyaasi maneno yake?
29 U krv im vode prometnu i pobi ribe njihove.
Aligeuza maji yao kuwa damu, ikasababisha samaki wao kufa.
30 Zemljom im žabe provrvješe, prodriješe i u dvore kraljevske.
Nchi yao ilijaa vyura tele, ambao waliingia hadi kwenye vyumba vya kulala vya watawala wao.
31 Reče, i muha roj doletje i komarci u sve kraje njine.
Alisema, yakaja makundi ya mainzi, na viroboto katika nchi yao yote.
32 Mjesto kiše grÓad im dade, ognjene munje po njihovoj zemlji.
Alibadilisha mvua yao ikawa mvua ya mawe, yenye umeme wa radi nchini yao yote,
33 Udari im lozu i smokve, polomi stabla u krajima njinim.
akaharibu mizabibu yao na miti ya tini, na akaangamiza miti ya nchi yao.
34 Reče, i skakavci dođoše i bezbrojne gusjenice s njima.
Alisema, nzige wakaja, tunutu wasio na idadi,
35 U zemlji im proždriješe svu bilinu, proždriješe rod njihovih njiva.
wakala kila jani katika nchi yao, wakala mazao ya ardhi yao.
36 Pobi sve prvorođene u njihovoj zemlji, sve prvine snage njihove.
Kisha akawaua wazaliwa wote wa kwanza katika nchi yao, matunda ya kwanza ya ujana wao wote.
37 Izvede ih sa srebrom i zlatom; u plemenima njinim bolesnih ne bješe.
Akawatoa Israeli katika nchi wakiwa na fedha na dhahabu nyingi, wala hakuna hata mmoja kutoka kabila zao aliyejikwaa.
38 Odlasku njihovu Egipat se obradova, jer ga od njih strah spopade.
Misri ilifurahi walipoondoka, kwa sababu hofu ya Israeli ilikuwa imewaangukia.
39 Rasprostro je oblak kao pokrov i oganj da se obnoć sja.
Alitandaza wingu kama kifuniko, na moto kuwamulikia usiku.
40 Zamoliše, i dovede prepelice, nebeskim ih kruhom tad nahrani.
Waliomba, naye akawaletea kware, akawashibisha kwa mkate wa mbinguni.
41 Hrid rascijepi, i provri voda, pustinjom poteče kao rijeka.
Alipasua mwamba, maji yakabubujika, yakatiririka jangwani kama mto.
42 Tad se sjeti svete riječi svoje što je zada sluzi svome Abrahamu.
Kwa maana alikumbuka ahadi yake takatifu, aliyompa Abrahamu mtumishi wake.
43 Puk svoj s klicanjem izvede i s veseljem izabrane svoje.
Aliwatoa watu wake kwa furaha, wateule wake kwa kelele za shangwe,
44 I dade im zemlje poganske, trud naroda baštiniše,
akawapa nchi za mataifa, wakawa warithi wa mali wengine walikuwa wameitaabikia:
45 da čuvaju naredbe njegove i zakone da mu paze. Aleluja!
alifanya haya ili wayashike mausia yake na kuzitii sheria zake. Msifuni Bwana.