< Psalmi 101 >

1 Davidov. Psalam. Da zapjevam o dobroti i pravdi, tebi, Jahve, da zasviram!
Zaburi ya Daudi. Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako; kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.
2 Razmatrat ću put savršenstva: kad li ćeš k meni doći? Hodit ću u nedužnosti srca u domu svojemu.
Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama: utakuja kwangu lini? Nitatembea nyumbani mwangu kwa moyo usio na lawama.
3 Neću stavljati pred oči svoje ništa opako. Mrzim čovjeka koji čini zlo: on neće biti uza me.
Sitaweka mbele ya macho yangu kitu kiovu. Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani; hawatashikamana nami.
4 Opako će srce biti daleko od mene; o zlu neću da znadem.
Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami; nitajitenga na kila ubaya.
5 Tko kleveće bližnjeg u potaji, toga ću pogubiti. Čovjeka oholih očiju i srca naduta ja ne podnosim.
Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri, huyo nitamnyamazisha; mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburi huyo sitamvumilia.
6 Pogled upravljam k vjernima na zemlji da sa mnom stanuju. Tko hodi putem nedužnim taj će mi služiti.
Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi, ili waweze kuishi pamoja nami; yeye ambaye moyo wake hauna lawama atanitumikia.
7 Neće prebivati u kući mojoj tko spletke snuje. Tko govori laži, neće opstati pred mojim očima.
Mdanganyifu hatakaa nyumbani mwangu, yeye asemaye kwa uongo hatasimama mbele yangu.
8 Svaki ću dan istrebljivati sve zlikovce u zemlji; iskorijenit ću iz grada Jahvina sve koji čine bezakonje.
Kila asubuhi nitawanyamazisha waovu wote katika nchi; nitamkatilia mbali kila mtenda mabaya kutoka mji wa Bwana.

< Psalmi 101 >