< Mudre Izreke 31 >

1 Riječ Lemuela, kralja Mase, kojima ga je učila majka njegova.
Maneno ya mfalme Lemueli - mausia aliyofundishwa na mama yake.
2 Ne, sine moj! Ne, sine srca mog! Ne, sine zavjeta mojih!
Mwanangu nini? Na ni nini mwana wa tumbo langu? Na ni nini mwana wa nadhiri zangu?
3 Ne daj snage svoje ženama ni putova svojih zatiračima kraljeva.
Nguvu zako usiwape wanawake; au wenye kuharibu wafalme njia zako.
4 Nije za kraljeve, Lemuele, ne pristaje kraljevima vino piti, ni glavarima piće opojno,
Lemueli, kunywa divai, siyo kwa ajili ya wafalme, wala kwa watawala kuuliza, “kileo kikali kiko wapi?”
5 da u piću ne zaborave zakona i prevrnu pravo nevoljnicima.
Kwa sababu kama watakunywa, watasahau sheria ni nini, na kupotosha haki za wote walioonewa.
6 Dajte žestoko piće onomu koji će propasti i vino čovjeku komu je gorčina u duši:
Wape kileo kikali watu wanaopotea na mvinyo kwa wale wenye kutaabika kwa uchungu.
7 on će piti i zaboraviti svoju bijedu i neće se više sjećati svoje nevolje.
Atakunywa na kusahau umasikini wake na hataikumbuka taabu yake.
8 Otvaraj usta svoja za nijemoga i za pravo sviju nesretnika što propadaju.
Ongea kwa ajili yao wasioweza kuongea, kwa madai ya wote wanaopotea.
9 Otvaraj usta svoja, sudi pravedno i pribavi pravo siromahu i nevoljniku.
Ongea na uhukumu kwa vipimo vya haki na utetee dai la masikini na watu wahitaji.
10 Tko će naći ženu vrsnu? Više vrijedi ona nego biserje.
Mke hodari ni nani anaweza kumpata? Thamani yake ni zaidi kuliko vito.
11 Muževljevo se srce uzda u nju i blagom neće oskudijevati.
Moyo wa mume wake humwamini, na hatakuwa masikini.
12 Ona mu čini dobro, a ne zlo, u sve dane vijeka svojeg.
Humtendea mambo mema na wala si mabaya siku zote za maisha yake.
13 Pribavlja vunu i lan i vješto radi rukama marnim.
Huchagua sufu na kitani, na hufanya kazi yake ya mikono kwa furaha.
14 Ona je kao lađa trgovačka: izdaleka donosi kruh svoj.
Yupo kama meli za wafanyabiashara; huleta chakula chake kutoka mbali.
15 Još za noći ona ustaje, hrani svoje ukućane i određuje posao sluškinjama svojim.
Huamka wakati wa usiku na kuwapa chakula watu wa kaya yake, na kugawa kazi kwa watumishi wake wa kike.
16 Opazi li polje, kupi ga; plodom svojih ruku sadi vinograd.
Hulifikiria shamba na kulinunua, kwa tunda la mikono yake hupanda shamba la mizabibu.
17 Opasuje snagom bedra svoja i živo miče rukama.
Yeye mwenyewe hujivika nguvu na kuimarisha mikono yake.
18 Vidi kako joj posao napreduje: noću joj se ne gasi svjetiljka.
Huangalia ni kipi kitaleta faida nzuri kwake; usiku wote taa yake haizimishwi.
19 Rukama se maša preslice i prstima drži vreteno.
Mikono yake huiweka kwenye mpini wa kisokotea nyuzi na hushikilia kisokotea nyuzi.
20 Siromahu dlan svoj otvara, ruke pruža nevoljnicima.
Mkono wake huwafikia watu masikini; mikono yake huwafikia watu wahitaji.
21 Ne boji se snijega za svoje ukućane, jer sva čeljad ima po dvoje haljine.
Haogopi theluji kwa ajili ya kaya yake, kwa maana nyumba yake yote imevika kwa nguo nyekundu.
22 Sama sebi šije pokrivače, odijeva se lanom i purpurom.
Hutengeneza matandiko ya kitanda chake, na huvaa nguo za kitani ya dhambarau safi.
23 Muž joj je slavan na Vratima, gdje sjedi sa starješinama zemaljskim.
Mume wake anajulikana malangoni, anapoketi na wazee wa nchi.
24 Platno tka i prodaje ga i pojase daje trgovcu.
Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza, na naleta mishipi kwa wafanyabiashara.
25 Odjevena je snagom i dostojanstvom, pa se smije danu budućem.
Amevaa nguvu na heshima, na wakati ujao huucheka.
26 Svoja usta mudro otvara i pobožan joj je nauk na jeziku.
Anafumbua kinywa chake kwa hekima na sheria ya ukarimu ipo kwenye ulimi wake.
27 Na vladanje pazi ukućana i ne jede kruha besposlice.
Huangalia njia za nyumba yake na hawezi kula mkate wa uvivu.
28 Sinovi njezini podižu se i sretnom je nazivaju, i muž njezin hvali je:
Watoto wake huinuka na kumwita heri na mume wake humsifia, akisema,
29 “Mnoge su žene bile vrsne, ali ti ih sve nadmašuješ.”
“Wanawake wengi wamefanya vizuri, lakini wewe umewapita wote.”
30 Lažna je ljupkost, tašta je ljepota: žena sa strahom Gospodnjim zaslužuje hvalu.
Madaha ni udanganyifu, uzuri ni ubatili; bali mwanamke amchaye Yehova, atasifiwa.
31 Plod joj dajte ruku njezinih i neka je na Vratima hvale djela njezina!
Mpeni tunda la mikono yake na kazi zake zimsifu katika malango.

< Mudre Izreke 31 >