< Mudre Izreke 23 >
1 Kad sjedneš blagovati s moćnikom. dobro pazi što je pred tobom;
Unapoketi kula pamoja na mtawala, angalia kwa uangalifu kilichopo mbele yako,
2 stavljaš nož sebi pod grlo ako si proždrljivac;
na kama ni mtu unayependa kula chakula sana weka kisu kooni.
3 ne poželi slastica njegovih jer su jelo prijevarno.
Usitamani vinono vyake maana ni chakula cha uongo.
4 Ne trudi se stjecati bogatstvo; okani se takve misli;
Usifanye kazi sana ili kupata mali; uwe na busara ya kutosha ili ujue wakati wa kuacha.
5 usmjeriš li oči prema njemu, njega već nema jer načini sebi krila kao orao i odleti u nebo.
Je utaruhusu macho yako yaangaze juu yake? Itaondoka, maana itawaa mabawa kama tai na kuruka angani.
6 Ne jedi jela zavidnikova, ne čezni za slasticama njegovim,
Usile chakula cha yule mwenye jicho baya- na usiwe na shauku ya vinono vyake,
7 jer on je onakav kako u sebi misli: “Jedi i pij”, veli ti, ali mu srce nije s tobom.
maana ni mtu mwenye kuhesabu gharama ya chakula. “Kula na kunywa!” anakuambia, lakini moyo wake haupo pamoja nawe.
8 Zalogaj koji si pojeo izbljuvat ćeš, uzalud ćeš prosut' svoje ljupke riječi.
Utatapika kiasi kidogo ulichokula na utakuwa umepoteza sifa zako njema.
9 Pred bezumnikom nemoj govoriti jer prezire tvoje umne riječi.
Usiongee katika usikivu wa mpumbavu, maana atadharau hekima ya maneno yako.
10 Ne pomiči prastare međe i ne prodiri u polje siročadi,
Usihamishe jiwe la mpaka wa kale au kunyang'anya mashamba ya yatima,
11 jer je moćan njihov osvetnik: branit će njihovo pravo protiv tebe.
maana Mkombozi wao ni imara na atatetea kesi yao dhidi yako.
12 Obrati pouci srce svoje i uho svoje riječima mudrim.
Elekeza moyo wako katika mafundisho na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
13 Ne uskraćuj djetetu opomene, jer, udariš li ga šibom, neće umrijeti:
Usizuie kuadilisha mtoto, maana ukimchapa kwa fimbo, hatakufa.
14 biješ ga šibom, ali mu dušu iz Podzemlja izbavljaš. (Sheol )
Ni wewe unayepaswa kumchapa kwa fimbo na kuikoa nafsi yake kuzimu. (Sheol )
15 Sine moj, kad ti je mudro srce, i ja se od srca veselim;
Mwanangu, kama moyo wako una busara, basi moyo wangu utafurahi pia;
16 i kliče sva nutrina moja kad ti usne govore što je pravo.
sehemu zangu ndani kabisa zitafurahi sana midomo yako inaponena haki.
17 Neka ti srce ne zavidi grešnicima, nego neka ti uvijek bude u strahu Gospodnjem,
Usiruhusu moyo wako kuwahusudu wenye dhambi, lakini endelea kumcha Yehova siku zote.
18 jer imat ćeš budućnost i tvoja nada neće propasti.
Hakika tumaini lako halitaondolewa na siku zako za hapo baadaye.
19 Slušaj, sine moj, i mudar budi i ravnim putem vodi srce svoje.
Sikia- wewe! - mwanangu, na uwe mwenye busara na uelekeze moyo wako katika njia.
20 Ne druži se s vinopijama ni sa žderačima mesa,
Usishirikiane pamoja na walevi, au pamoja na walaji wa nyama walafi,
21 jer pijanica i izjelica osiromaše i pospanac se oblači u krpe.
maana mlevi na mlafi wanakuwa masikini na usingizi utawavika kwa matambara.
22 Slušaj svoga oca, svoga roditelja, i ne prezri majku kad ostari.
Msikilize baba yako ambaye alikuzaa na usimdharau mama yako wakati akiwa mzee.
23 Pribavi istinu i ne prodaji je, steci mudrost, pouku i razbor.
Inunue kweli, lakini usiiuze; nunua hekima, nidhamu, na ufahamu.
24 Radovat će se otac pravednikov, i roditelj će se mudroga veseliti.
Baba yake mwenye haki atafurahia sana, na yule amzaaye mtoto mwenye busara atamfurahia.
25 Neka se veseli otac tvoj i majka tvoja, i neka se raduje roditeljka tvoja.
Mfurahishe baba yako na mama yako na yule aliyekuzaa afurahie.
26 Daj mi, sine moj, srce svoje, i neka oči tvoje raduju putovi moji.
Mwanangu, nipe moyo wako na macho yako yachunguze njia zangu.
27 Jer bludnica je jama duboka i tuđinka tijesan zdenac.
Maana malaya ni shimo refu, na mke wa mume mwingine ni kisima chembamba.
28 Ona i vreba u zasjedi kao lupež i uvećava broj bezbožnika među ljudima.
Anavizia kama mnyang'anyi na huongeza idadi ya wadanganyifu miongoni mwa wanadamu.
29 Komu: ah? komu: jao? komu: svađe? komu: uzdasi? komu: rane nizašto? komu: zamućene oči?
Nani mwenye taabu? Nani mwenye huzuni? Nani mwenye mapigano? Nani mwenye malalamiko? Nani mwenye majeraha bila sababu? Nani mwenye macho mekundu?
30 Onima što kasno sjede kod vina, koji su došli kušati vino začinjeno.
Ni wale ambao huzengea kwenye mvinyo, wale wanaojaribu kuchanganya mvinyo.
31 Ne gledaj na vino kad rujno iskri, kad se u čaši svjetlucavo prelijeva: pije se tako glatko,
Usiutazame mvinyo ukiwa mwekundu, wakati unametameta kwenye kikombe na kutelemka kwa uraini.
32 a na kraju ujeda kao zmija i žaca kao guja ljutica.
Mwisho wake unauma kama nyoka na sumu yake kama kifutu.
33 Oči će ti gledati tlapnje i srce govoriti ludosti.
Macho yako yataona vitu vigeni na moyo wako utatamka vitu vya ukaidi.
34 I bit će ti kao da ležiš na pučini morskoj ili kao da ležiš navrh jarbola.
Utakuwa kama anayelala kwenye bahari au anayelala juu ya mlingoti. “
35 “Izbiše me, ali me ne zabolje; istukoše me, ali ne osjetih; kad se otrijeznim, još ću tražiti.”
Wamenipiga,” utasema, “lakini sikuumia. Wamenichapa, lakini sikuwa na hisia. Nitaamka lini? Nitatafuta kinywaji kingine.”