< Mudre Izreke 15 >

1 Blag odgovor ublažava jarost, a riječ osorna uvećava srdžbu.
Jawabu la upole huondoa ghadhabu, bali neno la ukatili huchochea hasira.
2 Jezik mudrih ljudi proslavlja znanje, a usta bezumnih prosipaju ludost.
Ulimi wa watu mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha wapumbavu humwaga upuuzi.
3 Oči su Jahvine na svakome mjestu i budno motre i zle i dobre.
Macho ya Yehova yapo kila mahali, yakiwatazama juu ya waovu na wema.
4 Blaga je besjeda drvo života, a pakosna je rana duhu.
Ulimi unaoponya ni mti wa uzima, bali ulimi wa udanganyifu huvunja moyo.
5 Luđak prezire pouku oca svog, a tko ukor prima, pametno čini.
Mpumbavu hudharau marudi ya baba yake, bali yeye anayejifunza kutokana na masahihisho ni mwenye hekima.
6 U pravednikovoj je kući mnogo blaga, a opaki zarađuje propast svoju.
Katika nyumba ya wale watendao haki kuna hazina kubwa, bali mapato ya watu waovu huwapa taabu.
7 Usne mudrih siju znanje, a srce je bezumnika nepostojano.
Midomo ya wenye hekima husambaza maarifa, bali mioyo ya wapumbavu haifanyi hivyo.
8 Žrtva opakog mrska je Jahvi, a mila mu je molitva pravednika.
Yehova anachukia sadaka za watu waovu, bali maombi ya watu waadilifu ndiyo furaha yake.
9 Put opakih Jahvi je mrzak, a mio mu je onaj koji ide za pravicom.
Yehova anachukia njia ya watu waovu, bali anampenda yule ambaye huandama haki.
10 Oštra kazna čeka onog tko ostavlja pravi put, a umrijet će tko mrzi ukor.
Marudi ya ukatili hungojea kwa yeyote ambaye huiacha njia na yule ambaye huchukia masahihisho atakufa.
11 I Šeol i Abadon stoje pred Jahvom, a nekmoli srca sinova ljudskih. (Sheol h7585)
Kuzimu na uharibifu vipo wazi mbele za Yehova; je si zaidi sana mioyo ya wana wa wanadamu? (Sheol h7585)
12 Podsmjevač ne ljubi onog tko ga kori: on se ne druži s mudrima.
Mwenye mzaha huchukia masahihisho; hatakwenda kwa wenye hekima.
13 Veselo srce razvedrava lice, a bol u srcu tjeskoba je duhu.
Moyo wenye furaha husababisha uchangamfu wa uso, bali huzuni huvunja moyo.
14 Razumno srce traži znanje, a bezumnička se usta bave ludošću.
Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, bali kinywa cha wapumbavu hujilisha kwenye upuuzi.
15 Svi su dani bijednikovi zli, a komu je srce sretno, na gozbi je bez prestanka.
Siku zote za watu waliokandamizwa ni taabu, bali moyo wenye furaha unakaramu daima.
16 Bolje je malo sa strahom Gospodnjim nego veliko blago i s njime nemir.
Bora kitu kidogo pamoja na kumcha Mungu kuliko hazina kubwa pamoja na ghasia.
17 Bolji je obrok povrća gdje je ljubav nego od utovljena vola gdje je mržnja.
Bora mlo wenye mboga kukiwa na upendo kuliko kuandaliwa ndama aliyenona kwa chuki.
18 Gnjevljiv čovjek zameće svađu, a ustrpljiv utišava raspru.
Mtu mwenye hasira huchochea mabishano, bali mtu ambaye hukawia kukasirika hutuliza ugomvi.
19 Put je ljenivčev kao glogov trnjak, a utrta je staza pravednika.
Mapito ya mtu goigoi ni kama sehemu yenye uwa wa miiba, bali mapito ya mtu mwadilifu ni njia kuu iliyojengwa imara.
20 Mudar sin veseli oca, a bezumnik prezire majku svoju.
Mwana mwenye busara huleta furaha kwa baba yake, bali mtu mpumbavu humdharau mama yake.
21 Ludost je veselje nerazumnomu, a razuman čovjek pravo hodi.
Upuuzi humfurahia mtu ambaye amepungukiwa akili, bali mwenye ufahamu hutembea katika njia nyofu.
22 Ne uspijevaju nakane kad nema vijećanja, a ostvaruju se gdje je mnogo savjetnika.
Mipango huharibika ambapo hakuna ushauri, bali washauri wengi wanafanikiwa.
23 Čovjek se veseli odgovoru usta svojih, i riječ u pravo vrijeme - kako je ljupka!
Mtu anapata furaha wakati anapotoa jibu la kufaa; je ni zuri kiasi gani neno kwa wakati muafaka!
24 Razumnu čovjeku put života ide gore, da izmakne carstvu smrti koje je dolje. (Sheol h7585)
Njia ya uzima huwapeleka juu watu wenye hekima, ili waondoke kutoka chini kuzimu. (Sheol h7585)
25 Jahve ruši kuću oholima, a postavlja među udovici.
Yehova hurarua urithi wa mwenye kiburi, bali huzilinda mali za mjane.
26 Mrske su Jahvi zle misli, a dobrostive riječi mile su mu.
Yehova huyachukia mawazo ya watu waovu, bali maneno ya upole ni safi.
27 Tko se grabežu oda, razara svoj dom, a tko mrzi mito, živjet će.
Mporaji huleta shida kwenye familia yake, bali yeye ambaye huchukia rushwa ataishi.
28 Pravednikovo srce smišlja odgovor, a opakomu usta govore zlobom.
Moyo wa yule atendaye haki hutafakari kabla ya kujibu, bali kinywa cha watu waovu humwanga ubaya wake wote.
29 Daleko je Jahve od opakih, a uslišava molitvu pravednih.
Yehova yupo mbali na watu waovu, bali husikia maombi ya wale watendao haki.
30 Bistar pogled razveseli srce i radosna vijest oživi kosti.
Nuru ya macho huleta furaha moyoni na habari njema ni afya kwenye mwili.
31 Uho koje posluša spasonosan ukor prebiva među mudracima.
Kama utazingatia wakati mtu anapokurekebisha jinsi ya kuishi, utabaki miongoni mwa watu wenye busara.
32 Tko odbaci pouku, prezire vlastitu dušu, a tko posluša ukor, stječe razboritost.
Yeye anayekataa karipio hujidharau mwenyewe, bali yule asikilizaye masahihisho hujipatia ufahamu.
33 Strah je Gospodnji škola mudrosti, jer pred slavom ide poniznost.
Kumcha Yehova hufundisha hekima na unyenyekevu huja kabla ya heshima.

< Mudre Izreke 15 >