< Mudre Izreke 12 >

1 Tko ljubi pouku, ljubi znanje, a tko mrzi ukor, lud je.
Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
2 Dobar dobiva milost od Jahve, a podmukao osudu.
Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
3 Zloćom se čovjek ne utvrđuje, a korijen se pravedniku ne pomiče.
Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
4 Kreposna je žena vijenac mužu svojemu, a sramotna mu je kao gnjilež u kostima.
Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
5 Pravedničke su misli pravične, spletke opakih prijevarne.
Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
6 Riječi opakih pogubne su zamke, a pravedne izbavljaju usta njihova.
Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
7 Opaki se ruše i nema ih više, a kuća pravednika ostaje.
Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
8 Čovjek se hvali po oštrini svoga razuma, a prezire se tko je opak srcem.
Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
9 Bolje je biti malen i imati samo jednog slugu nego se hvastati a nemati ni kruha.
Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
10 Pravednik pazi i na život svog živinčeta, dok je opakomu srce okrutno.
Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
11 Tko obrađuje svoju zemlju, sit je kruha, a tko trči za ništavilom, nerazuman je.
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
12 Čežnja je opakoga mreža od zala, a korijen pravednika daje ploda.
Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
13 Opakomu je zamka grijeh njegovih usana, a pravednik se izbavlja od tjeskobe.
Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
14 Od ploda svojih usta nasitit će se svatko obilno, a ono što je rukama učinio vratit će mu se.
Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
15 Luđaku se čini pravim njegov put, a mudar čovjek sluša savjete.
Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
16 Luđak odmah odaje svoj bijes, a pametan pokriva sramotu.
Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
17 Tko govori istinu, otkriva što je pravo, a lažljiv svjedok prijevaru.
Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
18 Nesmotren govori kao da mačem probada, a jezik je mudrih iscjeljenje.
Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
19 Istinita usta traju dovijeka, a lažljiv jezik samo za čas.
Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
20 Prijevara je u srcu onih koji snuju zlo, a veselje u onih koji dijele miroljubive savjete.
Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
21 Pravednika ne stiže nikakva nevolja, a opaki u zlu grcaju.
Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
22 Mrske su Jahvi usne lažljive, a mili su mu koji zbore istinu.
Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
23 Promišljen čovjek prikriva svoje znanje, a srce bezumničko razglašuje svoju ludost.
Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
24 Marljiva ruka vlada, a nemar vodi u podložnost.
Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
25 Briga u srcu pritiskuje čovjeka, a blaga riječ veseli ga.
Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
26 Pravednik vodi svojeg prijatelja, a opake zavodi njihov put.
Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
27 Nemaran ne ulovi svoje lovine, a marljivost je čovjeku blago dragocjeno.
Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
28 Na stazi pravice stoji život i na njezinu putu nema smrti.
Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.

< Mudre Izreke 12 >