< Mudre Izreke 10 >

1 Mudar sin veseli oca, a lud je sin žalost majci svojoj.
Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
2 Ne koristi krivo stečeno blago, dok pravednost izbavlja od smrti.
Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
3 Ne dopušta Jahve da gladuje duša pravednika, ali odbija pohlepu opakih.
Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
4 Lijena ruka osiromašuje čovjeka, a marljiva ga obogaćuje.
Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
5 Tko sabira ljeti, razuman je sin, a tko hrče o žetvi, navlači sramotu.
Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
6 Blagoslovi su nad glavom pravedniku, a usta opakih kriju nasilje.
Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
7 Pravednikov je spomen blagoslovljen, a opakom se ime proklinje.
Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
8 Tko je mudra srca, prima zapovijedi, dok brbljava luda propada.
Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
9 Tko nedužno živi, hodi bez straha, a tko ide krivim putovima, poznat će se.
Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
10 Tko žmirka okom, zadaje tugu, a tko ludo zbori, propada.
Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
11 Pravednikova su usta izvor života, a opakomu usta kriju nasilje.
Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
12 Mržnja izaziva svađu, a ljubav pokriva sve pogreške.
Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
13 Na usnama razumnoga nalazi se mudrost, a batina je za leđa nerazumna čovjeka.
Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
14 Mudri kriju znanje, a luđakova su usta blizu propasti.
Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
15 Blago je bogatomu tvrdi grad, a ubogima je propast njihovo siromaštvo.
Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
16 Pravednik prirađuje za život, a opaki prirađuje za grijeh.
Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
17 Tko se naputka drži, na putu je života, a zabluđuje tko se na ukor ne osvrće.
Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
18 Lažljive usne kriju mržnju, a tko klevetu širi, bezuman je!
Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
19 Obilje riječi ne biva bez grijeha, a tko zauzdava svoj jezik, razuman je.
Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
20 Pravednikov je jezik odabrano srebro, a razum opakoga malo vrijedi.
Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
21 Pravednikove su usne hrana mnogima, a luđaci umiru s ludosti svoje.
Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
22 Gospodnji blagoslov obogaćuje i ne prati ga nikakva muka.
Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
23 Bezumniku je radost učiniti sramotno djelo, a razumnu čovjeku biti mudar.
Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
24 Čega se opaki boji, ono će ga stići, a pravednička se želja ispunjava.
Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
25 Kad oluja prohuja, opakoga nestane, a pravednik ima temelj vječni.
Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
26 Kakav je ocat zubima i dim očima, takav je ljenivac onima koji ga šalju.
Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 Strah Gospodnji umnaža dane, a opakima se prekraćuju godine.
Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
28 Pravedničko je ufanje puno radosti, a opakima je nada uprazno.
Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
29 Gospodnji je put okrilje bezazlenu, a propast onima koji čine zlo.
Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
30 Pravednik se neće nikad pokolebati, a opakih će nestati s lica zemlje.
Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
31 Pravednikova usta rađaju mudrošću, a opak jezik čupa se s korijenom.
Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
32 Pravednikove usne znaju što je milo, dok usta opakih poznaju zloću.
Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.

< Mudre Izreke 10 >