< Brojevi 33 >

1 Ovo su postaje Izraelaca što ih prijeđoše kad iziđoše iz zemlje egipatske u svojim četama pod vodstvom Mojsijevim i Aronovim.
Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
2 Na zapovijed Jahvinu Mojsije je bilježio polazne točke njihova putovanja. Ovo su njihove postaje prema njihovim polaznim točkama.
Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
3 Iz Ramsesa krenuše u prvome mjesecu. Bio je petnaesti dan prvoga mjeseca - sutradan poslije Pashe - kad se Izraelci zaputiše uzdignutih pesnica i naočigled sviju Egipćana,
Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
4 dok su Egipćani pokopavali one koje je Jahve između njih pobio, to jest sve prvorođence, i tako nad njihovim božanstvima izvršio pravdu.
waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
5 Krenu dakle Izraelci iz Ramsesa i utabore se u Sukotu.
Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
6 Zatim odu iz Sukota i utabore se u Etamu, baš na rubu pustinje.
Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
7 Pođu iz Etama, a onda okrenu prema Pi Hahirotu, koji se nalazi nasuprot Baal Sefona. Tabore postave pred Migdolom.
Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
8 Krenu od Pi Hahirota i prijeđu posred mora u pustinju. Išli su tri dana pustinjom Etanom, a onda se utabore u Mari.
Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
9 Zatim odu iz Mare i stignu u Elim. U Elimu je bilo dvanaest izvor-voda i sedamdeset palma. Tu su se utaborili.
Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
10 Potom krenu iz Elima te se utabore uz Crveno more.
Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
11 A otišavši od Crvenog mora, utabore se u pustinji Sinu.
Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
12 Potom odu iz pustinje Sina i postave tabore u Dofki.
Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
13 Otišavši iz Dofke, utabore se u Alušu.
Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
14 Krenu iz Aluša i utabore se u Refidimu. Tu narod nije imao vode da pije.
Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
15 Odu iz Refidima te se utabore u Sinajskoj pustinji.
Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
16 Krenu iz Sinajske pustinje te se utabore u Kibrot Hataavi.
Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
17 Odu iz Kibrot Hataave te se utabore u Haserotu.
Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
18 Onda odu iz Haserota i utabore se u Ritmi.
Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
19 Krenu iz Ritme i utabore se u Rimon Peresu.
Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
20 Odu iz Rimon Peresa i utabore se u Libni.
Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
21 Iz Libne odu i utabore se u Risi.
Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
22 Odu iz Rise te se utabore u Kehelati.
Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
23 Odu iz Kehelate i utabore se na brdu Šeferu.
Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
24 Odu s brda Šefera i utabore se u Haradi.
Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
25 Odu iz Harade i utabore se u Makhelotu.
Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
26 Odu iz Makhelota te se utabore u Tahatu.
Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
27 Odu iz Tahata i utabore se u Tarahu.
Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
28 Iz Taraha odu i utabore se u Mitki.
Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
29 Odu iz Mitke i utabore se u Hašmoni.
Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
30 Iz Hašmone odu i utabore se u Moserotu.
Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
31 Odu iz Moserota i utabore se u Bene Jaakanu.
Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
32 Odu iz Bene Jaakana i utabore se u Hor Gidgadu.
Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
33 Odu iz Hor Gidgada i utabore se u Jotbati.
Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
34 Odu iz Jotbate i utabore se u Abroni.
Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
35 Iz Abrone odu i utabore se u Esion Geberu.
Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
36 Iz Esion Gebera odu i utabore se u pustinji Sinu, to jest u Kadešu.
Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
37 Iz Kadeša krenu te se utabore na brdu Horu, na granici zemlje edomske.
Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
38 Na zapovijed Jahvinu svećenik se Aron pope na brdo Hor i tu umre na prvi dan petoga mjeseca, u četrdesetoj godini nakon izlaska Izraelaca iz egipatske zemlje.
Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
39 Aronu je bilo stotinu dvadeset i tri godine kad je preminuo na brdu Horu.
Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
40 Aradski kralj, Kanaanac, koji je živio u kanaanskom kraju Negebu, čuo je o dolasku Izraelaca.
Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
41 S brda Hora odu te se utabore u Salmoni.
Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
42 Odu iz Salmone i utabore se u Punonu.
Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
43 Odu iz Punona i utabore se u Obotu.
Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
44 Odu iz Obota i utabore se na moapskom području u Ije-Abarimu.
Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
45 Odu iz Ije-Abarima i utabore se u Dibon Gadu.
Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
46 Iz Dibon Gada odu i utabore se u Almon Diblatajimu.
Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
47 Iz Almon Diblatajima odu i utabore se na Abarimskim bregovima, pred Nebom.
Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
48 Odu s Abarimskih bregova i utabore se na Moapskim poljanama, uz Jordan, nasuprot Jerihonu;
Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
49 taborovali su uz Jordan od Bet Haješimota sve do Abel Hašitima na Moapskim poljanama.
Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
50 Na Moapskim poljanama uz Jordan, nasuprot Jerihonu, Jahve reče Mojsiju:
Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
51 “Ovako reci Izraelcima: 'Kad prijeđete preko Jordana u zemlju kanaansku,
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
52 potjerajte ispred sebe sve stanovnike te zemlje, uništite sve njihove slike; uništite sve njihove salivene kumire i sve njihove uzvišice porušite.
wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
53 Onda zaposjednite zemlju i u njoj se nastanite, jer sam vam je predao da je zaposjednete.
Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
54 Zemlju razdijelite kockom među svoje rodove. Brojnijem povećajte dio, a manjem smanjite. Gdje god kocka padne, bilo za koga, neka je to njegovo, a prema otačkim plemenima dijelite im baštinu.
Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
55 Ako stanovnike zemlje ispred sebe ne potjerate, onda će oni koje od njih na životu ostavite biti trnje u vašim očima i bodljike u vašim bokovima; dosađivat će vam u zemlji u kojoj budete živjeli
“‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
56 i postupit ću s vama kako sam mislio postupiti s njima.'”
Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”

< Brojevi 33 >