< Brojevi 18 >

1 Tada Jahve reče Aronu: “Ti, tvoji sinovi i tvoj pradjedovski dom s tobom bit ćete odgovorni za grijehe u Svetištu; ti i tvoji sinovi s tobom bit ćete odgovorni za grijehe svoga svećeništva.
Bwana akamwambia Aroni, “Wewe, wanao na jamaa ya baba yako mtawajibika kwa makosa dhidi ya mahali patakatifu, na wewe na wanao peke yenu ndio mtakaowajibika kwa makosa dhidi ya ukuhani.
2 Pridruži k sebi i svoju braću od Levijeva plemena - tvoga pradjedovskog doma - neka ti se priključe da ti poslužuju, tebi i tvojim sinovima s tobom, pred Šatorom svjedočanstva.
Walete Walawi wenzako kutoka kabila la baba zako ili waungane nanyi na kuwasaidia wakati wewe na wanao mnapohudumu mbele ya Hema la Ushuhuda.
3 Neka stoje na službu tebi i svemu Šatoru, ali neka se ne približuju pokućstvu u Svetištu niti žrtveniku, da ne poginu i oni i vi.
Watawajibika kwenu na watafanya kazi zote za Hema, lakini kamwe wasisogelee vifaa vya patakatifu au madhabahu, la sivyo wao na ninyi mtakufa.
4 Neka su, dakle, tebi pridruženi i neka preuzmu brigu za Šator sastanka, svaku službu oko Šatora. I neka se ni jedan svjetovnjak ne približuje vama,
Watajiunga nanyi na watawajibika kwa utunzaji wa Hema la Kukutania, yaani kazi zote kwenye Hema, wala hakuna mtu mwingine yeyote atakayeweza kusogea karibu hapo mlipo.
5 a vi vršite službu u Svetištu i službu oko žrtvenika da se više ne izlijeva gnjev na Izraelce.
“Mtawajibika katika utunzaji wa mahali patakatifu na madhabahu, ili kwamba ghadhabu isiwaangukie Waisraeli tena.
6 Uzeh, evo, vašu braću levite između Izraelaca vama za dar; kao darovani pripadaju Jahvi da obavljaju službu oko Šatora sastanka.
Mimi mwenyewe nimewachagua Walawi wenzenu kutoka miongoni mwa Waisraeli kama zawadi kwenu, waliowekwa wakfu kwa Bwana ili kufanya kazi katika Hema la Kukutania.
7 Ti i tvoji sinovi s tobom preuzmite svećeničke poslove oko svega što spada na žrtvenik i iza zavjese. Službu koju dajem na dar vašem svećeništvu vi obavljajte. A svjetovnjak koji se primakne neka se pogubi.”
Lakini ni wewe tu na wanao mtakaoweza kutumika kama makuhani kuhusiana na kila kitu kwenye madhabahu na ndani ya pazia. Ninawapa utumishi wa ukuhani kama zawadi. Mtu mwingine yeyote atakayekaribia mahali patakatifu ni lazima auawe.”
8 Još reče Jahve Aronu: “Tebi, evo, povjeravam brigu o onom što se meni prinosi. Sve što Izraelci posvećuju dodjeljujem tebi i tvojim sinovima kao baštinu trajnim zakonom.
Kisha Bwana akamwambia Aroni, “Mimi mwenyewe nimekuweka kuwa mwangalizi wa sadaka zote zitakazotolewa kwangu; matoleo yote matakatifu Waisraeli wanayonipa ninakupa wewe na wanao kama sehemu yenu na fungu lenu la kawaida.
9 Ovo neka pripadne tebi od svetinja nad svetinjama: od paljenih žrtava svi njihovi darovi, za sve njihove prinosnice, za sve njihove okajnice i za sve njihove naknadnice što ih budu meni uzvraćali; ta vrlo sveta stvar neka pripadne tebi i tvojim sinovima!
Mtachukua sehemu ya yale matoleo matakatifu sana ambayo hayateketezwi kwa moto. Kutoka kwa matoleo yote wanayoniletea kama sadaka takatifu sana, ziwe za nafaka, au za dhambi, au za makosa, sehemu ile itakuwa yako na wanao.
10 Blagujte ih kao najveće svetinje! Svaki muškarac može ih jesti. Neka ti budu svete!
Mtaila kama kitu kilicho kitakatifu sana; kila mwanaume ataila. Ni lazima mtaiheshimu kama takatifu.
11 I ovo neka bude za te: ono što se uzima od izraelskih prinosa da se prinese kao prikaznica - trajnim zakonom predajem tebi, tvojim sinovima i tvojim kćerima s tobom. Svatko tko u tvome domu bude čist može od toga jesti.
“Hiki pia ni chako: chochote kilichotengwa kutoka kwenye matoleo yote ya sadaka za kuinuliwa za Waisraeli. Ninakupa wewe haya, wana na binti zako kama sehemu yenu ya kawaida. Kila mmoja wa nyumba yako ambaye ni safi kwa taratibu za ibada anaweza kuyala.
12 Najbolje od novoga ulja i najbolje od novoga vina i žita - prvine koje se prinose Jahvi - predajem tebi.
“Ninawapa mafuta ya zeituni yaliyo bora kuliko yote, na divai mpya iliyo bora kuliko zote na nafaka wanazompa Bwana kama malimbuko katika mavuno yao.
13 Prvi rodovi svega u njihovoj zemlji što ih budu donosili Jahvi neka budu tvoji. Tko je god čist u tvome domu može ih jesti.
Malimbuko yote ya nchi ambayo wanamletea Bwana yatakuwa yenu. Kila mmoja nyumbani kwako ambaye ni safi kwa taratibu za Ibada anaweza kula.
14 Sve što u Izraelu bude određeno za 'herem' neka je tvoje.
“Kila kitu katika Israeli ambacho kimetolewa kwa Bwana ni chenu.
15 Svako prvorođenče svih bića - kako ljudi tako i životinja - što se prinose Jahvi neka bude tvoje. Samo pusti da se otkupi prvenac od ljudi i prvenče od nečiste stoke.
Kila mzaliwa wa kwanza wa mwanadamu na wa mnyama, ambaye ametolewa kwa Bwana ni wenu. Lakini ni lazima mtamkomboa kila mwana mzaliwa wa kwanza na kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa wanyama wasio safi.
16 Kad budu stari mjesec dana, pusti da ih otkupljuju. A njihovu otkupnu cijenu odredi: pet srebrnih šekela, prema hramskom šekelu, a to je dvadeset gera.
Watakapokuwa na umri wa mwezi mmoja, ni lazima mtawakomboa kwa bei ya ukombozi iliyowekwa, kwa shekeli tano za fedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, yenye uzito wa gera ishirini.
17 Ali prvenče kravlje, prvenče ovčje i prvenče kozje neka se ne otkupljuje. Oni su svetinja. Krv njihovu izlij na žrtvenik, a pretilinu njihovu sažeži u kad kao žrtvu spaljenu na ugodan miris Jahvi.
“Lakini kamwe usimkomboe mzaliwa wa kwanza wa maksai, kondoo au mbuzi; hawa ni watakatifu. Nyunyizia damu yao juu ya madhabahu na uchome mafuta yao kama sadaka itolewayo kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
18 Njihovo meso neka pripadne tebi; kao i grudi žrtve prikaznice i desno pleće.
Nyama zao zitakuwa chakula chenu, kama ilivyokuwa kidari cha kuinuliwa na paja la mguu wa kulia.
19 Sve posvećene prinose što ih Izraelci podižu Jahvi predajem trajnim zakonom tebi, tvojim sinovima i tvojim kćerima s tobom. To je savez osoljen, trajan pred Jahvom, tebi i tvome potomstvu s tobom.”
Chochote kitakachotengwa kutoka sadaka takatifu ambazo Waisraeli wanamtolea Bwana, ninakupa wewe, wanao na binti zako kama fungu lenu la kawaida. Ni Agano la milele la chumvi mbele za Bwana kwako na watoto wako.”
20 “Nemoj imati baštine u zemlji njihovoj”, reče Jahve Aronu, “niti sebi stječi posjeda među njima! Ja sam tvoj dio i tvoja baština među Izraelcima.”
Bwana akamwambia Aroni, “Hutakuwa na urithi wowote katika nchi yao, wala hutakuwa na sehemu miongoni mwao; Mimi ni fungu lako na urithi wako miongoni mwa Waisraeli.
21 “Levijevim sinovima, evo, predajem u baštinu sve desetine u Izraelu za njihovu službu - za službu što je obavljaju u Šatoru sastanka.
“Ninawapa Walawi zaka yote katika Israeli kama urithi wao kuwa kama malipo kwa kazi wanayoifanya wakati wanapohudumu katika Hema la Kukutania.
22 A Izraelci neka se više ne primiču Šatoru sastanka, da ne navuku na se grijeh i ne poginu.
Kuanzia sasa, kamwe Waisraeli wasisogelee karibu na Hema la Kukutania, la sivyo watabeba matokeo ya dhambi zao, nao watakufa.
23 Neka samo leviti obavljaju službu u Šatoru sastanka; i neka oni budu odgovorni za svoj grijeh. Trajna je to odredba za vaše naraštaje; među Izraelcima neka nemaju posjeda,
Ni Walawi watakaofanya kazi katika Hema la Kukutania na kubeba wajibu wa makosa dhidi yake. Hili ni agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo. Hawatapokea urithi wowote miongoni mwa Waisraeli.
24 jer ja im predajem u posjed desetine što ih Izraelci prinose na dar Jahvi. Stoga sam za njih rekao: neka oni nemaju posjeda među Izraelcima.”
Badala yake, ninawapa Walawi zaka zote zinazotolewa na Waisraeli kama sadaka kwa Bwana kuwa urithi wao. Hiyo ndiyo sababu nimesema hivi kuhusu wao: ‘Hawatakuwa na urithi miongoni mwa Waisraeli.’”
25 Jahve reče Mojsiju:
Bwana akamwambia Mose,
26 “Levitima govori i reci im: 'Kad od Izraelaca primate desetinu, koju ja od njih dajem vama u baštinu, od toga onda vi prinesite podizanicu Jahvi: desetinu od desetine.
“Sema na Walawi na uwaambie: ‘Mtakapopokea zaka kutoka kwa Waisraeli ambayo ninawapa kama urithi wenu kutoka kwao, ni lazima mtoe sehemu ya kumi ya hiyo zaka kama sadaka kwa Bwana, iwe zaka ya hiyo zaka.
27 Prinos će vam biti zaračunan kao da je prinos s gumna i Óotoka iz badnja.
Sadaka yenu itahesabiwa kwenu kama nafaka kutoka sakafu ya kupuria, au divai kutoka kwenye shinikizo la kukamulia zabibu.
28 Tako isto prinosite podizanicu Jahvi i od svih svojih desetina što ih primate od Izraelaca. Od toga davajte podizanicu Jahvinu svećeniku Aronu.
Kwa njia hii, ninyi pia mtatoa sadaka kwa Bwana kutoka zaka zote mtakazopokea kutoka kwa Waisraeli. Kutoka kwenye zaka hizi, ni lazima mtoe sehemu ya Bwana kwa Aroni, kuhani.
29 Od svih darova koje budete primali podižite podizanicu Jahvi; od svega ono najbolje - onaj dio koji treba posvećivati.'
Ni lazima mtoe kama sehemu ya Bwana iliyo nzuri sana tena ile sehemu iliyo takatifu sana kuliko zote ya kile kitu mlichopewa.’
30 Još im reci: 'Pošto od toga prinesete najbolji dio, neka se to levitima uračuna kao prihod s gumna i prihod iz badnja.
“Waambie Walawi: ‘Mtakapotoa sehemu zilizo bora sana, itahesabiwa kwenu kama mazao ya sakafu ya kupuria nafaka, au ya shinikizo la kukamulia zabibu.
31 Na svakome ga mjestu možete jesti, i vi i vaši ukućani, jer to vam je nagrada za vašu službu u Šatoru sastanka.
Ninyi na watu wa nyumbani mwenu mnaweza kula sehemu iliyobaki mahali popote, kwani ndio ujira wenu kwa ajili ya kazi yenu katika Hema la Kukutania.
32 Pošto prinesete njegov najbolji dio, nećete navući na se grijeha; svetinja Izraelaca nećete oskvrnjivati te nećete ginuti.'”
Kwa kutoa sehemu zake zilizo bora sana, hamtakuwa na hatia katika jambo hili; ndipo hamtatia unajisi sadaka takatifu za Waisraeli, nanyi hamtakufa.’”

< Brojevi 18 >