< Marko 8 >

1 Onih se dana opet skupio silan svijet. Budući da nisu imali što jesti, dozva Isus učenike pa im reče:
Katika siku hizo, kulikuwa tena na umati mkubwa, na hawakuwa na chakula. Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia,
2 “Žao mi je naroda jer su već tri dana uza me i nemaju što jesti.
“Ninauhurumia umati huu, wameendelea kuwa nami kwa siku tatu na hawana chakula.
3 Ako ih otpravim gladne njihovim kućama, klonut će putom. A neki su od njih došli iz daleka.”
Nikiwatawanya warudi majumbani kwao bila kula wanaweza wakazimia njiani kwa njaa. Na baadhi yao wametoka mbali sana.”
4 Učenici mu odgovore: “Otkuda bi ih tko ovdje u pustinji mogao nahraniti kruhom?”
Wanafunzi wake wakamjibu, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwashibisha watu hawa katika eneo hili lililoachwa?”
5 On ih zapita: “Koliko kruhova imate?” Oni odgovore: “Sedam.”
Akawauliza, “mna vipande vingapi vya mikate?” Wakasema, “Saba”.
6 Nato zapovjedi mnoštvu da posjeda po zemlji. I uze sedam kruhova, zahvali, razlomi i davaše svojim učenicima da posluže. I poslužiše mnoštvu.
Aliuamuru umati ukae chini. Akachukua mikate saba, akamshukuru Mungu, na kuivunja. Akawapa wanafunzi wake waiweke mbele yao, nao wakaiweka mbele ya umati.
7 A imali su i malo ribica. Blagoslovi i njih te reče da i to posluže.
Pia walikuwa na samaki wadogo wachache, na baada ya kushukuru, aliwaamuru wanafunzi wake wawagawie hivi pia.
8 I jeli su i nasitili se. A od preteklih ulomaka odniješe sedam košara.
Walikula na wakatosheka. Na walikusanya vipande vilivyo baki, vikapu vikubwa saba.
9 Bilo ih je oko četiri tisuće. Tada ih otpusti,
Walikaribia watu elfu nne. Na aliwaacha waende.
10 a sam sa svojim učenicima odmah uđe u lađu i ode u kraj dalmanutski.
Mara aliingia kwenye mashua na wanafunzi wake, na wakaenda katika ukanda ya Dalmanuta.
11 Tada istupiše farizeji i počeše raspravljati s njime. Iskušavajući ga, zatraže od njega znak s neba.
Kisha Mafarisayo walitoka nje na kuanza kubishana naye. Walitaka awape ishara kutoka mbinguni, kwa kumjaribu.
12 On uzdahnu iz sve duše i reče: “Zašto ovaj naraštaj traži znak? Zaista, kažem vam, ovome se naraštaju neće dati znak.”
Akatafakari kwa kina moyoni mwake akasema, “Kwa nini kizazi hiki kinatafuta ishara? Nawaambia ninyi kweli, hakuna ishara itakayotolewa kwa kizazi hiki.”
13 Tada ih ostavi, ponovno uđe u lađu pa otiđe prijeko.
Kisha akawaacha, akaingia ndani ya mashua tena, akaondoka kuelekea upande mwingine.
14 A zaboraviše ponijeti kruha; imali su samo jedan kruh sa sobom na lađi.
Wakati huo wanafunzi walisahau kuchukua mikate. Hawakuwa na mikate zaidi ya kipande kimoja kilichokuwa kwenye mashua.
15 Nato ih Isus opomenu: “Pazite, čuvajte se kvasca farizejskog i kvasca Herodova!”
Aliwaonya na kusema, “Muwe macho na mjilinde dhidi ya chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.
16 Oni, zamišljeni, među sobom govorahu: “Kruha nemamo.”
Wanafunzi wakasemezana wao kwa wao, “Ni kwa sababu hatuna mikate.”
17 Zamijetio to Isus pa im reče: “Zašto ste zamišljeni što kruha nemate? Zar još ne shvaćate i ne razumijete? Zar vam je srce stvrdnuto?
Yesu alilitambua hili, na akawaambia, “Kwa nini mnasemezana kuhusu kutokuwa na mikate? Hamjajua bado? Hamuelewi? Mioyo yenu imekuwa miepesi?
18 Oči imate, a ne vidite; uši imate, a ne čujete? Zar se ne sjećate?
Mna macho, hamuoni? Mna masikio, hamsikii? Hamkumbuki?
19 Kad sam ono razlomio pet kruhova na pet tisuća, koliko punih košara ulomaka odnijeste?” Kažu mu: “Dvanaest.”
Nilipoigawanya mikate mitano kwa watu elfu tano, mlichukua vikapu vingapi vilivyo jaa vipande vya mikate?” Wakamjibu, “kumi na mbili.”
20 “A kada razlomih sedam na četiri tisuće, koliko punih košara ulomaka odnijeste?” Odgovore: “Sedam.”
“Na nilipoigawanya mikate saba kwa watu elfu nne, mlichukua vikapu vingapi?”
21 A on će njima: “I još ne razumijete?”
Wakasema, “Saba.” Akawaambia, “Bado hamuelewi?”
22 Dođu u Betsaidu, dovedu mu slijepca pa ga zamole da ga se dotakne.
Wakaja Bethsaida. Watu hao walimleta kwa Yesu mtu kipofu na wakamsihi Yesu amguse.
23 On uhvati slijepca za ruku, izvede ga iz sela, pljunu mu u oči, stavi na nj ruke i zapita ga: “Vidiš li što?”
Yesu akamshika kwa mkono yule kipofu, na kumwongoza nje ya kijiji. Alipotema mate juu ya macho yake na kunyosha mikono yake juu yake, alimuuliza, “Unaona chochote?”
24 Slijepac upilji pogled i reče: “Opažam ljude; vidim nešto kao drveće ... hodaju.”
Alitazama juu na kusema, “Naona watu wanaonekana kama miti inatembea.”
25 Tada mu Isus opet stavi ruke na oči i slijepac progleda i ozdravi te je mogao sve jasno na daleko vidjeti.
Ndipo akanyosha tena mikono yake juu ya macho yake, mtu yule akafungua macho yake, aliona tena, na akaona kila kitu vizuri.
26 Tada ga posla kući i reče mu: “Ne ulazi u selo.”
Yesu alimwacha aende nyumbani na akamwambia, “Usiingie mjini.”
27 I krenu Isus i njegovi učenici u sela Cezareje Filipove. Putem on upita učenike: “Što govore ljudi, tko sam ja?”
Yesu aliondoka na wanafunzi wake kwenda vijiji vya Kaiseria ya Filipi. Wakiwa njiani aliwauliza wanafunzi, “Watu wanasema mimi ni nani?”
28 Oni mu rekoše: “Da si Ivan Krstitelj, drugi da si Ilija, treći opet da si neki od proroka.”
Wakamjibu wakasema, “Yohana mbatizaji. Wengine wanasema, 'Eliya' na wengine, 'Mmoja wa Manabii.”
29 On njih upita: “A vi, što vi kažete, tko sam ja?” Petar prihvati i reče: “Ti si Pomazanik - Krist!”
Akawauliza, “Lakini ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro kamwambia, “Wewe ni Kristo.”
30 I zaprijeti im da nikomu ne kazuju o njemu.
Yesu akawaonya wasimwabie mtu yeyote kumuhusu Yeye.
31 I poče ih poučavati kako Sin Čovječji treba da mnogo pretrpi, da ga starješine, glavari svećenički i pismoznanci odbace, da bude ubijen i nakon tri dana da ustane.
Na akaanza kuwafundisha ya kuwa Mwana wa Adamu lazima ateseke kwa mambo mengi, na atakataliwa na viongozi na makuhani wakuu, na waandishi, na atauawa, na baada ya siku tatu atafufuka.
32 Otvoreno im to govoraše. Petar ga uze u stranu i poče odvraćati.
Alisema haya kwa uwazi. Ndipo Petro akamchukua pembeni na akaanza kumkemea.
33 A on se okrenu, pogleda svoje učenike pa zaprijeti Petru: “Nosi se od mene, sotono, jer ti nije na pameti što je Božje, nego što je ljudsko!”
Lakini Yesu aligeuka na kuwatazama wanafunzi wake na akamkemea Petro na kusema, “Pita nyuma yangu Shetani! Hujali mambo ya Mungu, isipokuwa mambo ya watu.”
34 Tada dozva narod i učenike pa im reče: “Hoće li tko za mnom, neka se odrekne samoga sebe, neka uzme svoj križ i neka ide za mnom.
Kisha akauita umati na wanafunzi wake pamoja, na kuwaambia, “Kama kuna mtu anataka kunifuata, ajikane mwenyewe, achukue msalaba wake, na anifuate.
35 Tko hoće život svoj spasiti, izgubit će ga; a tko izgubi život svoj poradi mene i evanđelja, spasit će ga.
Kwa kuwa yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote atakayepoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya injili, atayaokoa.
36 Ta što koristi čovjeku steći sav svijet, a životu svojemu nauditi?
Inamfaidia nini mtu, kupata ulimwengu wote, na kisha kupata hasara ya maisha yake?
37 Ta što da čovjek dadne u zamjenu za život svoj?
Mtu anaweza kutoa nini badala ya maisha yake?
38 Doista, tko se zastidi mene i mojih riječi u ovom preljubničkom i grešničkom naraštaju - njega će se stidjeti i Sin Čovječji kada dođe u slavi Oca svoga zajedno sa svetim anđelima.”
Yeyote anioneaye aibu na maneno yangu katika kizazi hiki cha wazinzi na kizazi cha wenye dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea aibu atakapokuja katika ufalme wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.

< Marko 8 >