< Malahija 2 >

1 A sad vas opominjem, svećenici!
“Sasa onyo hili ni kwa ajili yenu, enyi makuhani.
2 Ako ne budete poslušali, ako ne budete k srcu uzeli da proslavite Ime moje - govori Jahve nad Vojskama - kletvu ću na vas svaliti i proklet ću vaš blagoslov. I već ga prokleh jer to niste k srcu uzeli.
Kama hamtasikiliza, na kama hamtaki kuielekeza mioyo yenu kuheshimu Jina langu, nitatuma laana juu yenu, nami nitalaani baraka zenu. Naam, nimekwisha kuzilaani, kwa sababu hamkuielekeza mioyo yenu kuniheshimu mimi,” Asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
3 I slomit ću vam ruku, bacit ću vam u lice izmetine, izmetine vaših svetkovina, i s njima ću vas splaviti.
“Kwa sababu yenu nitawakatilia mbali wazao wenu. Nitazipaka nyuso zenu mavi, mavi ya dhabihu zenu. Nanyi mtafukuzwa pamoja nazo mtoke mbele zangu.
4 Po tom ćete znati: to je bila moja opomena da ostane Savez moj s Levijem - govori Jahve nad Vojskama.
Nanyi mtajua kuwa nimewapelekea onyo hili ili kwamba Agano langu na Lawi lipate kuendelea,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
5 A moj Savez s njim, to bijaše život i mir - ja sam mu ih dao: bijaše to strah - i on me se bojao, Imena se moga plašio.
“Agano langu lilikuwa pamoja naye, agano la uhai na amani, nami nilimpa yote, ili aniche na kuniheshimu, naye akaniheshimu na kusimama akilicha Jina langu.
6 Zakon istine bijaše u njegovim ustima i pakost mu ne kaljaše usana; u miru i pravičnosti hodio je sa mnom i mnoge je od grijeha odvratio.
Fundisho la kweli lilikuwa kinywani mwake, wala hakuna uongo wowote uliopatikana katika midomo yake. Alitembea nami katika amani na unyofu, naye akawageuza wengi kutoka dhambini.
7 Da, usne svećenikove treba da čuvaju znanje, a iz njegovih usta treba tražiti Zakon: ta on je glasnik Jahve nad Vojskama.
“Kwa maana yapasa midomo ya kuhani kuhifadhi maarifa. Tena kutoka kinywani mwake watu wangepaswa kutafuta mafundisho, kwa sababu yeye ni mjumbe wa Bwana Mwenye Nguvu Zote.
8 Ali vi ste s puta zašli, učinili ste da se mnogi o Zakon spotiču, raskinuli ste Savez Levijev - govori Jahve nad Vojskama.
Lakini mmegeuka mkaiacha njia, na kwa mafundisho yenu mmesababisha wengi kujikwaa. Mmevunja agano na Lawi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
9 Zato učinih da vas preziru i ponizuju svi narodi jer se putova mojih vi držali niste, nego ste bili pristrani primjenjujuć Zakon.
“Kwa hiyo nimewasababisha ninyi kudharauliwa na kufedheheshwa mbele ya watu wote, kwa sababu hamkufuata njia zangu, bali mmeonyesha upendeleo katika mambo ya sheria.”
10 Nemamo li svi jednog Oca? Nije li nas jedan Bog stvorio? Zašto smo onda jedan drugome nevjerni te skvrnimo Savez svojih otaca?
Je, sote hatuna Baba mmoja? Hatukuumbwa na Mungu mmoja? Kwa nini basi tunalinajisi Agano la baba zetu kwa kukosa uaminifu kila mmoja kwa mwenzake?
11 Iznevjerio se Juda: učinili su sramotu u Izraelu i Jeruzalemu, jer Juda je oskvrnuo Svetinju, Jahvi dragu, i ženi se kćerju tuđega božanstva.
Yuda amevunja uaminifu. Jambo la kuchukiza limetendeka katika Israeli na katika Yerusalemu: Yuda amepanajisi mahali patakatifu apendapo Bwana, kwa kuoa binti wa mungu mgeni.
12 Svakog tko tako učini, ma tko bio on, nek iskorijeni Jahve iz šatora Jakovljevih i izmeđ onih koji prinose žrtvu Jahvi nad Vojskama!
Kwa maana kwa mtu yeyote atendaye jambo hili, Bwana na amkatilie mbali kutoka hema za Yakobo, hata kama huwa anamletea Bwana Mwenye Nguvu Zote sadaka.
13 I ovo još vi činite: zalijevate suzama Jahvin žrtvenik tužeći i ridajući, jer on više neće da se žr tvi prikloni, iz ruke mu vaše ona nije ugodna.
Kitu kingine mnachokifanya: Mnaifurikisha madhabahu ya Bwana kwa machozi. Mnalia na kuugua kwa sababu yeye haziangalii tena sadaka zenu wala hazikubali kwa furaha kutoka mikononi mwenu.
14 I vi pitate: “Zašto?” Zato što je Jahve bio svjedok između tebe i žene mladosti tvoje kojoj si nevjeran premda ti drugarica bijaše i žena tvoga saveza.
Mnauliza, “Kwa nini?” Ni kwa sababu Bwana ni shahidi kati yako na mke wa ujana wako, kwa sababu umevunja uaminifu naye, ingawa yeye ni mwenzako, mke wa agano lako la ndoa.
15 Nije li On načinio jedno jedino biće dahom životnim obdareno? A što to jedino biće traži? Božanski naraštaj! Poštuj dakle život svoj i ne budi nevjeran ženi svoje mladosti.
Je, Bwana hakuwafanya wao kuwa mmoja? Katika mwili na katika roho wao ni wa Mungu. Kwa nini wawe mmoja? Kwa sababu Mungu alikuwa akitafuta mzao mwenye kumcha Mungu. Kwa hiyo jihadharini wenyewe katika roho zenu, mtu asivunje uaminifu kwa mke wa ujana wake.
16 Jer ja mrzim otpuštanje žena - govori Jahve, Bog Izraelov - i onog koji nevjerom haljine svoje kalja - govori Jahve nad Vojskama! Poštujte dakle život svoj, ne budite nevjerni!
“Ninachukia kuachana,” asema Bwana, Mungu wa Israeli, “pia nachukia mtu anayejivika jeuri kama vazi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. Kwa hiyo jihadharini wenyewe katika roho zenu, wala msije mkavunja uaminifu.
17 Dosađujete Jahvi svojim riječima, a pitate: “U čemu mu dosađujemo?” Time što govorite: “Svi koji zlo čine dobro su viđeni u očima Jahvinim i takvi su mu mili!” ili: “Gdje je Bog pravde?”
Mmemchosha Bwana kwa maneno yenu. Nanyi mnauliza, “Tumemchosha kwa namna gani?” Mmemchosha kwa kusema, “Wote watendao mabaya ni wema machoni pa Bwana, naye anapendezwa nao” au “Mungu wa haki yuko wapi?”

< Malahija 2 >