< Luka 3 >
1 Petnaeste godine vladanja cara Tiberija, dok je upravitelj Judeje bio Poncije Pilat, tetrarh Galileje Herod, a njegov brat Filip tetrarh Itureje i zemlje trahonitidske, i Lizanije tetrarh Abilene,
Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato akiwa mtawala wa Uyahudi, Herode akiwa mfalme wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania akiwa mfalme wa Abilene,
2 za velikog svećenika Ane i Kajfe, dođe riječ Božja Ivanu, sinu Zaharijinu, u pustinji.
nao Anasi na Kayafa wakiwa makuhani wakuu, neno la Mungu likamjia Yohana, mwana wa Zekaria huko jangwani.
3 On obiđe svu okolicu jordansku propovijedajući obraćeničko krštenje na otpuštenje grijeha
Akaenda katika nchi yote kandokando ya Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
4 kao što je pisano u Knjizi besjeda Izaije proroka: Glas viče u pustinji: Pripravite put Gospodinu, poravnite mu staze!
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.
5 Svaka dolina neka se ispuni, svaka gora i brežuljak neka se slegne! Što je krivudavo, neka se izravna, a hrapavi putovi neka se izglade!
Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitashushwa. Njia zilizopinda zitanyooshwa, na zilizoparuza zitasawazishwa.
6 I svako će tijelo vidjeti spasenje Božje.
Nao watu wote watauona wokovu wa Mungu.’”
7 Govoraše dakle mnoštvu koje je dolazilo da se krsti: “Leglo gujinje! Tko vas samo upozori da bježite od skore srdžbe?
Yohana akauambia ule umati wa watu uliokuwa unakuja ili kubatizwa naye, “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
8 Donosite dakle plodove dostojne obraćenja. I nemojte početi u sebi govoriti: 'Imamo oca Abrahama!' Jer, kažem vam: Bog iz ovog kamenja može podići djecu Abrahamovu.
Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. Wala msianze kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Kwa maana nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka mawe haya.
9 Već je sjekira položena na korijen stablima: svako dakle stablo koje ne donosi dobra roda siječe se i u oganj baca.”
Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”
10 Pitalo ga mnoštvo: “Što nam je dakle činiti?”
Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”
11 On im odgovaraše: “Tko ima dvije haljine, neka podijeli s onim koji nema. U koga ima hrane, neka učini isto tako.”
Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”
12 Dođoše krstiti se i carinici pa ga pitahu: “Učitelju, što nam je činiti?”
Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”
13 Reče im: “Ne utjerujte više nego što vam je određeno.”
Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”
14 Pitahu ga i vojnici: “A nama, što je nama činiti?” I reče im: “Nikome ne činite nasilja, nikoga krivo ne prijavljujte i budite zadovoljni svojom plaćom.”
Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?” Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”
15 Narod bijaše u iščekivanju i svi se u srcu pitahu o Ivanu nije li on možda Krist.
Watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wanajiuliza mioyoni mwao iwapo Yohana angeweza kuwa ndiye Kristo.
16 Zato im Ivan svima reče: “Ja vas, istina, vodom krstim. Ali dolazi jači od mene. Ja nisam dostojan odriješiti mu remenje na obući. On će vas krstiti Duhom Svetim i ognjem.
Yohana akawajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji. Lakini atakuja aliye na nguvu kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 U ruci mu vijača da pročisti gumno svoje i sabere žito u žitnicu svoju, a pljevu će spaliti ognjem neugasivim.”
Pepeto lake liko mkononi, tayari kusafisha sakafu yake ya kupuria na kuikusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”
18 I mnogim je drugim pobudama Ivan narodu navješćivao evanđelje.
Basi, kwa maonyo mengine mengi Yohana aliwasihi na kuwahubiria watu Habari Njema.
19 A Heroda je tetrarha Ivan prekorio zbog Herodijade, žene njegova brata i zbog svih njegovih zlodjela.
Lakini Yohana alipomkemea Mfalme Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia, mke wa ndugu yake, na maovu mengine aliyokuwa amefanya,
20 Svemu tome nadoda Herod još i ovo: zatvori Ivana u tamnicu.
Herode aliongezea jambo hili kwa hayo mengine yote: alimfunga Yohana gerezani.
21 Kad se krstio sav narod, krstio se i Isus. I dok se molio, rastvori se nebo,
Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka.
22 siđe na nj Duh Sveti u tjelesnom obličju, poput goluba, a glas se s neba zaori: “Ti si Sin moj, Ljubljeni! U tebi mi sva milina!”
Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
23 Kad je Isus nastupio, bilo mu je oko trideset godina. Bijaše - kako se smatralo - sin Josipov, Elijev,
Yesu alikuwa na umri wa miaka thelathini alipoanza huduma yake. Alikuwa akidhaniwa kuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Eli,
24 Matatov, Levijev, Malkijev, Janajev, Josipov.
Eli alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi, Lawi alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Yanai, Yanai alikuwa mwana wa Yosefu,
25 Matatijin, Amosov, Naumov, Heslijev, Nagajev,
Yosefu alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Amosi, Amosi alikuwa mwana wa Nahumu, Nahumu alikuwa mwana wa Esli, Esli alikuwa mwana wa Nagai,
26 Mahatov, Matatijin, Šimijev, Josehov, Jodin,
Nagai alikuwa mwana wa Maathi, Maathi alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Semeini, Semeini alikuwa mwana wa Yoseki, Yoseki alikuwa mwana wa Yoda,
27 Johananov, Resin, Zerubabelov, Šealtielov, Nerijev,
Yoda alikuwa mwana wa Yoanani, Yoanani alikuwa mwana wa Resa, Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli, Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli, Shealtieli alikuwa mwana wa Neri,
28 Malkijev, Adijev, Kosamov, Elmadamov, Erov,
Neri alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Adi, Adi alikuwa mwana wa Kosamu, Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu, Elmadamu alikuwa mwana wa Eri,
29 Jošuin, Eliezerov, Jorimov, Matatov, Levijev,
Eri alikuwa mwana wa Yoshua, Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri, Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu, Yorimu alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi,
30 Šimunov, Judin, Josipov, Jonamov, Elijakimov,
Lawi alikuwa mwana wa Simeoni, Simeoni alikuwa mwana wa Yuda, Yuda alikuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu, Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu, Eliakimu alikuwa mwana wa Melea,
31 Melejin, Menin, Matatin, Natanov, Davidov,
Melea alikuwa mwana wa Mena, Mena alikuwa mwana wa Matatha, Matatha alikuwa mwana wa Nathani, Nathani alikuwa mwana wa Daudi,
32 Jišajev, Obedov, Boazov, Salin, Nahšonov,
Daudi alikuwa mwana wa Yese, Yese alikuwa mwana wa Obedi, Obedi alikuwa mwana wa Boazi, Boazi alikuwa mwana wa Salmoni, Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni,
33 Aminadabov, Adminov, Arnijev, Hesronov, Peresov, Judin,
Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu, Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu, Aramu alikuwa mwana wa Hesroni, Hesroni alikuwa mwana wa Peresi, Peresi alikuwa mwana wa Yuda,
34 Jakovljev, Izakov, Abrahamov, Terahov, Nahorov,
Yuda alikuwa mwana wa Yakobo, Yakobo alikuwa mwana wa Isaki, Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu, Abrahamu alikuwa mwana wa Tera, Tera alikuwa mwana wa Nahori,
35 Serugov, Reuov, Pelegov, Eberov, Šelahov,
Nahori alikuwa mwana wa Serugi, Serugi alikuwa mwana wa Reu, Reu alikuwa mwana wa Pelegi, Pelegi alikuwa mwana wa Eberi, Eberi alikuwa mwana wa Sala,
36 Kenanov, Arpakšadov, Šemov, Noin, Lamekov,
Sala alikuwa mwana wa Kenani, Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi, Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu, Shemu alikuwa mwana wa Noa, Noa alikuwa mwana wa Lameki,
37 Metušalahov, Henokov, Jeredov, Mahalalelov, Kenanov,
Lameki alikuwa mwana wa Methusela, Methusela alikuwa mwana wa Enoki, Enoki alikuwa mwana wa Yaredi, Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli, Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani,
38 Enošev, Šetov, Adamov, Božji.
Kenani alikuwa mwana wa Enoshi, Enoshi alikuwa mwana wa Sethi, Sethi alikuwa mwana wa Adamu, Adamu alikuwa mwana wa Mungu.