< Levitski zakonik 8 >

1 Jahve reče Mojsiju:
Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
2 “Uzmi Arona, a s njim i njegove sinove; ruho, ulje pomazanja, junca žrtve okajnice, dva ovna i košaru beskvasnih kruhova
“Walete Aroni na wanawe pamoja naye, mavazi na mafuta ya upako, fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kondoo dume wawili, na kikapu cha mkate usio na hamira.
3 te skupi svu zajednicu na ulazu u Šator sastanka.”
Ita kusanyiko lote kwenye ingilio la hema la kukutania.”
4 Mojsije učini kako mu je Jahve naredio, i zajednica se sabra na ulazu u Šator sastanka.
Kwa hiyo Musa akafanya kama Yahweh alivyomwamru, nalo kusanyiko lilikuja pamoja mbele ya ingilio la hema la kukutania. Kisha Musa akaliambia kusanyiko,
5 Tada Mojsije progovori zajednici: “Ovo je Jahve zpovjedio da se učini.”
“Hivi ndivyo alivyotuamru Yahweh tutende.”
6 Izvede zatim Mojsije Arona i njegove sinove pa ih u vodi opra.
Musa akamleta Aroni na wanawe na kuwaosha kwa maji.
7 Obuče na nj haljinu, opasa ga pojasom, ogrnu ga ogrtačem i stavi mu oplećak. Zatim ga opasa tkanicom oplećka i njome pritegnu uza nj oplećak.
Akamvika Aroni kanzu ya ndani yenye urefu wa kufika magotini na kumfunga ukumbuu kiunoni mwake, akamvika joho la nje lenye mikono mirefu na kumvika kile kizibao chenye vipande viwili tumboni na mgongoni na kukifunga kuzunguka kiunoni mwake kwa mshipi uliosokotwa kwa ustadi na kukikaza mwilini mwake.
8 Stavi mu naprsnik, a u naprsnik metnu Urim i Tumim.
Kisha Musa akaweka kifuko kifuani mwa Aroni, na ndani ya kifuko hicho akaweka Urimu na Thumimu.
9 Na glavu mu stavi mitru, a sprijeda na mitru postavi zlatnu pločicu - sveti vijenac - kako je Jahve naredio Mojsiju.
Na kisha akamfunga kiremba kichwani, na juu ya kiremba kwa mbele, akaweka bamba la dhahabu; liwe taji takatifu, kama Yahweh alivyomwamru yeye.
10 Uzme zatim Mojsije ulje pomazanja te pomaže Prebivalište i sve što je u njemu da ih posveti.
Musa akayatwaa hayo mafuta ya upako, akalipaka lile hema la kukutania na kila kitu kilichokuwamo ndani yake na kuvitenga kwa ajili ya Yahweh.
11 Sedam puta poškropi njime žrtvenik te pomaže žrtvenik i sav njegov pribor, umivaonik s njegovim stalkom da ih posveti.
Akayanyunyiza hayo mafuta juu ya madhabahu mara saba, na kisha akaipaka mafuta hiyo madhabahu na vyombo vyake vyote, na sinia la kunawia na kitako chake ili kuvitenga wa ajili ya Yahweh.
12 Izlije ulja pomazanja Aronu na glavu te ga pomaže da ga posveti.
Akamimina sehemu ya mafuta ya upako juu ya kichwa cha Aroni na kisha akampaka mafuta ili kumtenga.
13 Potom Mojsije dovede Aronove sinove; na njih obuče haljine, pasovima ih opaše i poveze im zavije, kako je Jahve Mojsiju naredio.
Musa akawaleta wana wa Aroni na kuwavika kila mmoja kanzu ya ndani yenye urefu wa kufika magotini. Kila mmoja wao akamfunga kwa ukumbuu kiunoni mwake na kuwafunga vitambaa vya kitani kichwani pao, kama vile Yahweh alivyokuwa amemru Musa.
14 Dovede potom junce žrtve okajnice. Aron i njegovi sinovi stave svoje ruke na glavu juncu žrtve okajnice.
Musa akamleta huyo fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha fahali ambaye wamemelete kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
15 Zatim ga Mojsije zakolje. Onda uzme krvi pa je svojim prstom stavi na rogove oko žrtvenika. Tako žrtvenik očisti. Zatim izlije krv podno žrtvenika; posveti ga, izvršivši na njemu obred pomirenja.
Musa akamchinja, na kisha akachukua sehemu ya damu yake kwa kidole chake na kuiweka juu ya mpembe za madhabahu, akaitakasa hiyo madhabahu, na kuitenga kwa Mungu, ambapo kwa kufanya hivyo, aliisababisha madhabahu kuwa sehemu ya kufaa kwa kufanyia upatanisho.
16 Zatim Mojsije uzme sav loj što je bio oko drobine, privjesak s jetre, oba bubrega i njihov loj, pa to sažeže u kad na žrtveniku.
Akachukua mafuta yote yaliyokuwa sehemu za ndani, kile kiwambo cha ini, zile figo mbili pamoja na mafuta yake, Musa akaichoma hiyo nyama yote juu ya madhabahu.
17 A kožu od junca, njegovo meso i njegovu nečist spali u vatri izvan tabora, kako je Jahve naredio Mojsiju.
Lakini yule fahali, ngozi yake, nyama yake na kinyesi chake, akavichoma nje ya kambi, kama vile Yehweh alivyokuwa amemwamru yeye.
18 Dovede potom ovna za žrtvu paljenicu. Aron i njegovi sinovi stave svoje ruke ovnu na glavu.
Musa akamleta yule konndoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo kondoo.
19 Sad ga Mojsije zakolje. Onda krvlju zapljusne žrtvenik sa svih strana.
Musa akamchinja kondoo na kuinyunyizia damu yake kila upande wa madhabahu.
20 Pošto isiječe ovna na dijelove, Mojsije sažeže u kad glavu, dijelove i loj.
Naye akamkatakata kondoo vipande vipande na akakiteketeza kichwa chake pamoja na vile vipande na mafuta.
21 U vodi opere drobinu i noge pa u kad sažeže na žrtveniku svega ovna. Bila je to žrtva paljenica na ugodan miris - žrtva u čast Jahvi paljena - kako je Jahve naredio Mojsiju.
Akaziosha kwa maji zile sehemu za ndani pamoja na miguu na akamteketeza kandoo mzima juu ya madhabahu. Ilikuwa ni dhabihu ya kuteketezwa na ilitoa harufu ya kupendeza, sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamru Musa.
22 Zatim dovede drugoga ovna, ovna za žrtvu posvetnicu. Aron i njegovi sinovi stave svoje ruke ovnu na glavu.
Kisha Musa akamleta yule kondoo dume mwingine, kondoo wa kuwekwa wakfu, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo.
23 Mojsije ga zakolje. Onda uzme krvi pa stavi na resu Aronova desnog uha, na palac njegove desne ruke i na palac njegove desne noge.
Aroni akamchinja, naye Musa akachukua sehemu ya damu na kuiweka kwenye ncha ya sikio la Aroni la kulia, juu ya dole gumba la mkono wake wa kulia, na kwenye kidole kikumbwa cha mguu wake wa kulia.
24 Potom Mojsije dovede Aronove sinove, pa im stavi iste krvi na resu desnog uha, na palac desne ruke i na palac desne noge. Zatim Mojsije krvlju zapljusne žrtvenik sa svih strana.
Akawaleta wana wa Aroni, naye akaweka sehemu ya damu ya kondoo yule kwenye ncha ya sikio lao la kulia, kwenye dole gumba lao cha mkono wa kulia na kwenye kidole chao kikubwa cha mguu wa kulia. Kisha Musa akainyunyiza damu ya huyo kila upande wa madhabahu
25 Poslije toga uzme loj, pretili rep, loj što je bio oko drobine, privjesak s jetre, oba bubrega i njihov loj - i desno pleće;
Naye akayatwaa yale mafuta, mafuta ya mkiani, mafuta liyolikuwa sehemu za ndani, na mafuta yafunikayo ini, zile figo mbili pamoja na mafuta yake na paja la kulia.
26 a iz košare beskvasnih kruhova, što je stajala pred Jahvom, uzme jednu beskvasnu pogaču, jednu prevrtu s uljem i jedan kolač i postavi ih na loj i desno pleće.
Akachukua mkate mmoja kutoka kwenye kikapu cha mikate isiyo na hamira ambayoo ilikuwa mbele za Yahweh, akatwaa mkate moja usio na hamira, na mkate mmoja ulioandaliwa kwa mafuta, na mkate mwemba wa kaki na akaiweka juu ya mafuta na juu ya paja la kulia la kondoo.
27 Sve to položi na ruke Arona i na ruke njegovih sinova pa to prinese kao žrtvu prikaznicu pred Jahvom.
Akaiweka yote mikoni mwa Aroni na katika mikono ya wanawe na kuitikisa mbele za Yahweh kuwa sadaka ya kutikiswa
28 Potom Mojsije opet to uzme s njihovih ruku i sažeže u kad na žrtveniku povrh žrtve paljenice. Bila je to žrtva posvetnica na ugodan miris, žrtva u čast Jahvi paljena.
Kisha Musa akaichukua mikate hiyo kutoka mikononi mwao na kuiteketeza juu ya madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Zilikuwa ni sadaka ya kuwekwa wakfu na ilitoa harufu ya kupendeza. Ilikuwa sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto.
29 Naposljetku Mojsije uzme grudi i prinese ih kao žrtvu prikaznicu pred Jahvom. To je bila pristojbina Mojsiju od ovna žrtve posvetnice, kako je Jahve Mojsiju naredio.
Musa akakichukua kidari na kukitikisa kuwa sadaka ya kutikiswa kwa Yahweh. Ilikuwa ni mgao wa Musa wa kondoo wa kuwekewa mikono kwa makuhani, Kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru yeye.
30 Zatim Mojsije uze ulja za pomazanje i krvi što je bila na žrtveniku te poškropi Arona i njegove haljine, a tako i njegove sinove i njihove haljine. Tako posveti Arona i njegove haljine; njegove sinove i njihove haljine.
Musa akatwaa sehemu ya mafuta ya upako na damu iliyokuwa juu ya madhabahu; naye akayanyunyiza haya juu ya nguo za Aroni, juu ya nguo zake mwenyewe na juu ya nguo za wana wa Aruni waliokua pamoja naye. Kwa njia hii alimtenga Aroni na nguo zake, na wanawe na nguo zao kwa ajili ya Yahweh.
31 Onda reče Mojsije Aronu i njegovim sinovima: “Skuhajte to meso na ulazu u Šator sastanka i ondje ga blagujte s kruhom što je u košari za žrtvu posvetnicu, kako sam naredio. Neka ga jedu Aron i njegovi sinovi!
Kwa hiyo Musa akawambia Aruni na wanawe, “Ipikeni nyama mbele ya ingilio la hema la kukutania, na hapo mtaila pamoja na mkate ulio kwenye kikapu cha kuwekwa wakfu, kama ilivyoamriwa, kusema, 'Aroni na wanawe wataila.'
32 A što od mesa i kruha ostane, spalite na vatri.
Masalio yoyote ya nyama na mikate utayateketeza kwa moto.
33 Sedam dana ne odlazite s ulaza Šatora sastanka - do dana kad se navrši rok vašega svećeničkog posvećenja. Jer sedam dana treba za vaše posvećenje.
Na hamtatoka kwenye ingilio la hema la kukutania kwa muda wa siku saba, hata zitakapotimia siku za kuwekwa mikono kwenu. Kwa kuwa kwa muda wa siku saba, Yahweh atawaweka wakfu.
34 Kako se radilo danas, Jahve je naredio da se tako radi dalje, da se nad vama izvrši obred pomirenja.
Kilichotendeka siku hii— Yahweh ndiye amekiamru kitendekeke ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
35 Zato ostanite na ulazu Šatora sastanka sedam dana, danju i noću vršeći što je Jahve naredio, da ne pomrete. Takvu sam ja zapovijed dobio.”
Mtakaa kwenye ingilio la hema la kukutania mchana na usiku siku saba, nanyi ishikeni amri ya Yahweh ili msije mkafa, kwa sababu hivi ndivyo ilivyoamriwa.
36 Aron i njegovi sinovi učiniše sve što je Jahve naredio preko Mojsija.
Kwa hiyo Aroni na wanawe wakafanya mambo yote ambayo Yahweh alikuwa amewaamru kwa kinywa cha Musa.

< Levitski zakonik 8 >