< Jošua 17 >

1 Ždrijebom je dopao i dio plemenu Manašeovu, jer je Manaše bio prvenac Josipov. Makiru, prvencu Manašeovu, ocu Gileadovu - bijaše on ratnik bez premca - pripade Gilead i Bašan.
Huu ndio mgawo wa kabila la Manase kama mzaliwa wa kwanza wa Yosefu, yaani kwa ajili ya Makiri, mzaliwa wa kwanza wa Manase. Makiri alikuwa baba wa Wagileadi, ambao walipokea Gileadi na Bashani kwa sababu Wamakiri walikuwa askari wakuu.
2 Dobili su svoj dio i ostali sinovi Manašeovi po svojim porodicama: sinovi Abiezerovi, sinovi Helekovi, sinovi Asrielovi; sinovi Šekemovi, sinovi Heferovi i sinovi Šemidini. To su muški potomci Manašea, sina Josipova, po svojim porodicama.
Kwa hiyo mgawo huu ulikuwa kwa ajili ya watu wa Manase waliokuwa wamebaki, ambao ni koo za Abiezeri, Heleki, Asirieli, Shekemu, Heferi na Shemida. Hawa ndio wanaume wale wengine wa uzao wa Manase mwana wa Yosefu kwa koo zao.
3 A Selofhad, sin Hefera, sina Gileada, sina Makira, sina Manašeova, nije imao sinova nego samo kćeri. Evo im imena: Mahla, Noa, Hogla, Milka i Tirsa.
Basi Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase hakuwa na wana waume ila mabinti tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.
4 One dođoše pred svećenika Eleazara i pred Jošuu, sina Nunova, i pred glavare govoreći: “Jahve je zapovjedio Mojsiju da se i nama dade baština među našom braćom.” I dadoše im po Jahvinoj zapovijedi baštinu među braćom njihova oca.
Wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi, wakasema: “Bwana alimwagiza Mose atupatie urithi miongoni mwa ndugu zetu.” Kwa hiyo Yoshua akawapa urithi pamoja na ndugu wa baba yao, kufuatana na agizo la Bwana.
5 Tako je dopalo Manašeu deset dijelova, povrh gileadske i bašanske zemlje, koje su s onu stranu Jordana.
Fungu la Manase lilikuwa na sehemu kumi za nchi, licha ya Gileadi na Bashani mashariki mwa Yordani,
6 Kćeri Manašeove dobiše baštinu među njegovim sinovima, a zemlja gileadska pripala je drugim sinovima Manašeovim.
kwa sababu wale binti za kabila la Manase walipokea urithi miongoni mwa wana wa kiume. Nchi ya Gileadi ilikuwa mali ya wazao wa Manase waliobaki.
7 Međa je Manašeova išla od Ašera do Mikmetata, koji leži nasuprot Šekemu, a zatim zavijala desno prema Jašibu na izvoru Tapuahu.
Eneo la Manase lilienea kuanzia Asheri hadi Mikmeta mashariki mwa Shekemu. Mpaka ule ulielekea upande wa kusini kutoka pale kujumuisha watu walioishi En-Tapua.
8 Pokrajina Tapuah pripadaše Manašeu, ali sam Tapuah na međi Manašeovoj pripadaše sinovima Efrajimovim.
(Nchi ya Tapua ilikuwa mali ya Manase, lakini Tapua yenyewe iliyo mpakani mwa nchi ya Manase ilikuwa ya Waefraimu.)
9 Međa je silazila do potoka Kane. Južno od potoka bili su i ovi gradovi što su Efrajimovim sinovima pripadali između Manašeovih gradova; a zemlja se Manašeova nalazila na sjeveru i izbijala na more.
Kisha mpaka ule uliendelea kuelekea kusini hadi Bonde la Kana. Kulikuwepo miji ya Efraimu iliyokuwa miongoni mwa miji ya Manase, lakini mpaka wa Manase ulikuwa upande wa kaskazini wa lile bonde na kuishia kwenye bahari.
10 Područje s juga pripadalo je Efrajimu, na sjeveru Manašeu, a more im bi međa; na sjeveru su graničili s Ašerom, a s Jisakarom na istoku.
Nchi ya kusini ilikuwa ya Efraimu, na ile iliyokuwa upande wa kaskazini ilikuwa ya Manase. Eneo la Manase lilifika bahari na ikapakana na Asheri upande wa kaskazini, na Isakari upande wa mashariki.
11 Manašeu pripadahu u Jisakaru i Ašeru: Bet-Šean sa svojim selima, Jibleam sa svojim selima, stanovnici Dora sa svojim selima, stanovnici En-Dora sa svojim selima, stanovnici Taanaka sa svojim selima, stanovnici Megida sa svojim selima; dakle: tri područja.
Katika Isakari na Asheri Manase alikuwa na miji pia: Beth-Shani, Ibleamu na watu wa Dori, Endori, Taanaki na Megido, pamoja na vijiji vyote vinavyohusika na miji hiyo (ya tatu katika orodha ni Nafothi).
12 Ali Manašeovi sinovi nisu mogli osvojiti te gradove i zato su Kanaanci ostali u tom kraju.
Lakini Wamanase hawakuweza kuimiliki miji hii, kwa kuwa Wakanaani walikazana kuishi katika maeneo hayo.
13 Ali kad su ojačali sinovi Izraelovi, nametnuše Kanaancima tlaku, ali ih nisu uspjeli protjerati.
Hata hivyo, Waisraeli walivyoendelea kupata nguvu waliwatumikisha Wakanaani na kuwatia katika kazi za kulazimishwa, lakini hawakuwafukuza kabisa.
14 Obrate se tada Josipovi sinovi Jošui i upitaju: “Zašto si nam dao u baštinu prema jednom ždrijebu, samo jedan dio, kad smo mnogobrojni i Jahve nas dosad blagoslivljao?”
Watu wa Yosefu wakamwambia Yoshua, “Kwa nini umetupa sisi mgawo mmoja tu na sehemu moja tu kuwa urithi? Sisi tu watu wengi sana, na Bwana ametubariki kwa wingi.”
15 Jošua im odgovori: “Kad ste narod mnogobrojan, pođite u šumu i krčite ondje sebi zemlje u periškoj i refaimskoj krajini, ako vam je pretijesna gora Efrajimova.”
Yoshua akajibu, “Kama ninyi ni wengi sana, na kama nchi ya vilima ya Efraimu ni ndogo sana kwenu, pandeni msituni mkafyeke eneo kwa ajili yenu wenyewe huko kwenye nchi ya Waperizi na Warefai.”
16 A sinovi Josipovi rekoše: “Gora nam ova neće biti dosta, a svi Kanaanci koji žive u ravnici imaju željezna kola, oni što su u Bet-Šeanu i selima njegovim i oni koji su u dolini jizreelskoj.”
Watu wa Yosefu wakajibu, “Hiyo nchi ya vilima haitutoshi, nao Wakanaani wote wanaoishi katika tambarare wanayo magari ya vita ya chuma, wote wa Beth-Shani na miji yake, na wale walio katika Bonde la Yezreeli.”
17 Tada odgovori Jošua domu Josipovu, i Efrajimu i Manašeu: “Vi ste brojan narod i imate silnu snagu. Zato nećeš dobiti samo jedan ždrijeb:
Lakini Yoshua akanena na nyumba ya Yosefu, yaani Efraimu na Manase: “Ninyi ni wengi sana na wenye nguvu sana. Hamtakuwa na mgawo mmoja tu,
18 neka gora bude tvoja. Ako je šumovita, iskrči je pa će obronci biti posjed doma tvoga. Istjerat ćeš sigurno Kanaance ako i imaju željezna kola, ako i jesu jaki.”
bali pia nchi hii ya kilima yenye msitu. Ifyekeni, nayo mipaka yake itakuwa yenu umbali mtakaoweza kufika. Ingawa Wakanaani wana magari ya chuma, nao wana nguvu, mwaweza kuwafukuza humo.”

< Jošua 17 >