< Jošua 12 >

1 Ovo su zemaljski kraljevi što su ih pobijedili Izraelci i osvojili njihovu zemlju s onu stranu Jordana k istoku, od potoka Arnona do gore Hermona, sa svom Arabom na istoku:
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:
2 Sihon, kralj amorejski, koji je stolovao u Hešbonu; njegovo se kraljevstvo protezalo od Aroera, koji leži na rubu doline potoka Arnona, sredinom doline i polovinom Gileada pa do potoka Jaboka, gdje je graničilo s Amoncima;
Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
3 i na istoku mu bila Araba do Keneretskog mora s jedne strane i sve do Arabskog ili Slanog mora prema Bet Haješimotu; i dalje na jugu do obronaka Pisge.
Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.
4 Međašio s njime Og, kralj bašanski, jedan od posljednjih Refaimaca; stolovao je u Aštarotu i Edreju.
Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
5 A vladao je gorom Hermonom i Salkom, čitavim Bašanom sve do gešurske i maakadske međe te drugom polovinom Gileada sve do granice Sihona, kralja hešbonskoga.
Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
6 Mojsije, sluga Jahvin, i sinovi Izraelovi sve su ih pobili i predao je Mojsije, sluga Jahvin, tu zemlju u posjed plemenu Rubenovu i Gadovu plemenu te polovini plemena Manašeova.
Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
7 A ovo su zemaljski kraljevi što su ih pobijedili Jošua i sinovi Izraelovi s ovu stranu Jordana k zapadu, od Baal Gada u libanonskoj ravnici pa do gore Halaka, koja se diže prema Seiru, a tu je zemlju Jošua dao u baštinu plemenima Izraelovim prema njihovim dijelovima,
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:
8 u Gorju, u Šefeli, u Arabi i po obroncima, u Pustinji te u Negebu: zemlju hetitsku, amorejsku i kanaansku, perižansku, hivijsku i jebusejsku:
nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):
9 jerihonski kralj, jedan; kralj Aja kod Betela, jedan;
mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja
10 jeruzalemski kralj, jedan; hebronski kralj, jedan;
mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja
11 jarmutski kralj, jedan; lakiški kralj, jedan;
mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja
12 eglonski kralj, jedan; gezerski kralj, jedan;
mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja
13 debirski kralj, jedan; gederski kralj, jedan;
mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja
14 hormski kralj, jedan; aradski kralj, jedan;
mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja
15 kralj Libne, jedan; adulamski kralj, jedan;
mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja
16 makedski kralj, jedan; betelski kralj, jedan;
mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja
17 kralj Tapuaha, jedan; heferski kralj, jedan;
mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja
18 afečki kralj, jedan; šaronski kralj, jedan;
mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja
19 madonski kralj, jedan; hasorski kralj, jedan;
mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja
20 šimron-meronski kralj, jedan; ahšafski kralj, jedan;
mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja
21 tanaački kralj, jedan; megidski kralj, jedan;
mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja
22 kedeški kralj, jedan; kralj Jokneama na Karmelu, jedan;
mfalme wa Kedeshi mmoja mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja
23 dorski kralj u pokrajini dorskoj, jedan; gojski kralj u Gilgalu, jedan;
mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) mmoja mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja
24 tirški kralj, jedan. U svemu trideset i jedan kralj.
mfalme wa Tirsa mmoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.

< Jošua 12 >