< Ivan 21 >
1 Poslije toga očitova se Isus ponovno učenicima na Tiberijadskome moru. Očitova se ovako:
Baada ya mambo hayo Yesu alijidhihirisha tena kwa wanafunzi katika Bahari ya Tiberia; hivi ndivyo alivyojidhihirisha mwenyewe:
2 Bijahu zajedno Šimun Petar, Toma zvani Blizanac, Natanael iz Kane Galilejske, zatim Zebedejevi i još druga dva njegova učenika.
Simon Petro alikuwa pamoja na Thomaso aitwaye Didimas, Nathanaeli wa kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili wa Yesu.
3 Kaže im Šimun Petar: “Idem ribariti.” Rekoše: “Idemo i mi s tobom.” Izađoše i uđoše u lađu, ali te noći ne uloviše ništa.
Simon Petro akawaambia, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Sisi, pia tutaenda nawe.” Wakaenda wakaingia kwenye mashua, lakini usiku huo wote hawakupata chochote.
4 Kad je već svanulo, stade Isus na kraju, ali učenici nisu znali da je to Isus.
Na asubuhi kulipokucha, Yesu alisimama ufukweni, nao wanafunzi hawakutambua kuwa alikuwa Yesu.
5 Kaže im Isus: “Dječice, imate li što za prismok?” Odgovoriše mu: “Nemamo.”
Kisha Yesu akawambia, “Vijana, mna chochote cha kula?” Nao wakamjibu, “Hapana.”
6 A on im reče: “Bacite mrežu na desnu stranu lađe i naći ćete.” Baciše oni i više je ne mogoše izvući od mnoštva ribe.
Akawambia, “Shusheni wavu upande wa kuume wa mashua, nanyi mtapata kiasi.” Kwa hiyo wakashusha wavu nao hawakuweza kulivuta tena kwa sababu ya wingi wa cha samaki.
7 Tada onaj učenik kojega je Isus ljubio kaže Petru: “Gospodin je!” Kad je Šimun Petar čuo da je to Gospodin, pripaše si gornju haljinu, jer bijaše gol, te se baci u more.
Basi yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akamwambia Petro, “Ni Bwana.” Naye Simon Petro aliposikia kuwa ni Bwana, akajifunga vazi lake (maana hakuwa amelivaa vizuri), kisha akajitupa baharini.
8 Ostali učenici dođoše s lađicom vukući mrežu s ribom jer ne bijahu daleko od kraja, samo kojih dvjesta lakata.
Wale wanafunzi wengine wakaja kwenye mashua (kwani hawakuwa mbali na pwani, yapata mita mia moja kutoka ufukweni), nao walikuwa wakivuta zile nyavu zilizokuwa zimejaa samaki.
9 Kad iziđu na kraj, ugledaju pripravljenu žeravicu i na njoj pristavljenu ribu i kruh.
Walipofika ufukweni, waliona moto wa mkaa pale na juu yake kulikuwa na samaki pamoja na mkate.
10 Kaže im Isus: “Donesite riba što ih sada uloviste.”
Yesu akawambia, “Leteni baadhi ya samaki mliovua sasa hivi.”
11 Nato se Šimun Petar popne i izvuče na kraj mrežu punu velikih riba, sto pedeset i tri. I premda ih je bilo toliko, mreža se ne raskinu.
Basi Simon Petro akapanda na kuukokota ule wavu uliokuwa umejaa samaki wakubwa, kiasi cha samaki 153; japo walikuwa wengi, ule wavu haukuchanika.
12 Kaže im Isus: “Hajde, doručkujte!” I nitko se od učenika ne usudi upitati ga: “Tko si ti?” Znali su da je Gospodin.
Yesu akawaambia, “Njoni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanfunzi aliyethubutu kumwuliza, “Wewe ni nani?” Walijua kuwa alikuwa ni Bwana.
13 Isus pristupi, uzme kruh i dade im, a tako i ribu.
Yesu akaja, akachukua ule mkate, kisha akawapa, akafanya vivyo hivyo na kwa wale samaki.
14 To se već treći put očitova Isus učenicima pošto uskrsnu od mrtvih.
Hii ilikuwa mara ya tatu kwa Yesu kujidhihirisha kwa wanafunzi wake baada ya kufufuka toka wafu.
15 Nakon doručka upita Isus Šimuna Petra: “Šimune Ivanov, ljubiš li me više nego ovi?” Odgovori mu: “Da, Gospodine, ti znaš da te volim.”
Baada ya kuwa wamefungua kinywa, Yesu akamwambia Simon Petro, “Simon mwana wa Yohana je, wanipenda mimi kuliko hawa?” Petro akajibu, “Ndiyo, Bwana; “Wewe wajua kuwa mimi nakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wanakondoo wangu.”
16 Kaže mu: “Pasi jaganjce moje!” Upita ga po drugi put: “Šimune Ivanov, ljubiš li me?” Odgovori mu: “Da, Gospodine, ti znaš da te volim!” Kaže mu: “Pasi ovce moje!”
Akamwambia mara ya pili, “Simon mwana wa Yona, je, wanipenda?” Petro akamwambia, “Ndiyo, Bwana; wewe wajua kuwa nakupenda. “Yesu akamwambia, “Chunga kondoo wangu.”
17 Upita ga treći put: “Šimune Ivanov, voliš li me?” Ražalosti se Petar što ga upita treći put: “Voliš li me?” pa mu odgovori: “Gospodine, ti sve znaš! Tebi je poznato da te volim.” Kaže mu Isus: “Pasi ovce moje!”
Akamwambia tena mara ya tatu, “Simon, mwana wa Yohana, Je wanipenda?” Naye Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, “Je Wewe wanipenda?” Naye akamwambia, “Bwana, unajua yote; unajua kuwa nakupenda.” Yesu akamwambia, Lisha kondoo wangu.
18 “Zaista, zaista kažem ti: Dok si bio mlađi, sam si se opasivao i hodio kamo si htio; ali kad ostariš, raširit ćeš ruke i drugi će te opasivati i voditi kamo nećeš.”
Amini, amini, nakuambia, ulipokuwa kijana ulizoea kuvaa nguo mwenyewe na kwenda kokote ulikotaka; lakini utakapokuwa mzee, utanyosha mikono yako, na mwingine atakuvalisha nguo na kukupeleka usikotaka kwenda.”
19 A to mu reče nagovješćujući kakvom će smrću proslaviti Boga. Rekavši to doda: “Idi za mnom!”
Yesu alisema haya ili kuonesha ni aina gani ya kifo ambacho Petro angemtukuza Mungu. Baada ya kuwa amesema haya, akamwambia Petro, “Nifuate.”
20 Petar se okrene i opazi da ga slijedi onaj učenik kojega je Isus ljubio i koji se za večere bijaše privio Isusu uz prsa i upitao ga: “Gospodine, tko će te to izdati?”
Petro aligeuka na kumwona yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akawafuata- Huyu ndiye aliyekuwa amajiegemeza kwenye kifua cha Yesu wakati wa chakula cha jioni na kumwuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”
21 Vidjevši ga, Petar kaže Isusu: “Gospodine, a što s ovim?”
Petro alimwona na kisha akamwuliza Yesu, “Bwana, Huyu mtu atafanya nini?”
22 Odgovori mu Isus: “Ako hoću da on ostane dok ne dođem, što je tebi do toga? Ti idi za mnom!”
Yesu akamjibu, “Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, hilo linakuhusu nini?” Nifuate.”
23 Stoga se pronese među braćom glas da onaj učenik neće umrijeti. No Isus mu nije rekao: “Neće umrijeti”, nego: “Ako hoću da on ostane dok ne dođem, što je tebi do toga?”
Kwa hiyo habari hii ikaenea miongoni mwa wale ndugu, kwamba mwanafunzi huyo hatakufa. Lakini Yesu hakumwambia Petro kuwa, mwanafunzi huyo hafi, “Kama nataka yeye abaki mpaka nitakapokuja yakuhusu nini?”
24 Taj učenik za ovo svjedoči i ovo napisa. I znamo da je istinito svjedočanstvo njegovo.
Huyu ndiye mwanafunzi atoaye ushuhuda wa mambo haya, na ndiye aliye andika mambo haya, na tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
25 A ima još mnogo toga što učini Isus i kad bi se sve redom popisalo, sav svijet, mislim, ne bi obuhvatio knjiga koje bi se napisale.
Kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu aliyafanya. Kama kila moja lingeandikwa, nadhani kwamba ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa.