< Ivan 12 >
1 Šest dana prije Pashe dođe Isus u Betaniju gdje bijaše Lazar koga je Isus uskrisio od mrtvih.
Siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alikwenda Bethania mahali ambako Lazaro aliyekuwa amefufuliwa na Yesu alikuwa anaishi.
2 Ondje mu prirediše večeru. Marta posluživaše, a Lazar bijaše jedan od njegovih sustolnika.
Wakaandaa karamu kwa heshima ya Yesu. Martha akawahudumia wakati Lazaro alikuwa miongoni mwa waliokaa mezani pamoja na Yesu.
3 Tada Marija uzme libru prave dragocjene nardove pomasti, pomaže Isusu noge i otare ih svojom kosom. I sva se kuća napuni mirisom pomasti.
Kisha Maria akachukua chupa ya painti moja yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa, akayamimina miguuni mwa Yesu na kuifuta kwa nywele zake. Nyumba nzima ikajaa harufu nzuri ya manukato.
4 Nato reče Juda Iškariotski, jedan od njegovih učenika, onaj koji ga je imao izdati:
Ndipo Yuda Iskariote mwana wa Simoni, mmoja wa wale wanafunzi ambaye ndiye angemsaliti Yesu, akasema,
5 “Zašto se ta pomast nije prodala za trista denara i razdala siromasima?”
“Kwa nini manukato haya hayakuuzwa kwa dinari 300 na fedha hizo wakapewa maskini?”
6 To ne reče zbog toga što mu bijaše stalo do siromaha, nego što bijaše kradljivac: kako je imao kesu, kradom je uzimao što se u nju stavljalo.
Yuda alisema hivi si kwa kuwa aliwajali maskini, bali kwa kuwa alikuwa mwizi, kwani ndiye alikuwa akitunza mfuko wa fedha akawa anaiba kile kilichowekwa humo.
7 Nato Isus odvrati: “Pusti je! Neka to izvrši za dan mog ukopa!
Yesu akasema, “Mwacheni. Aliyanunua manukato hayo ili ayaweke kwa ajili ya siku ya maziko yangu.
8 Jer siromahe imate uvijek uza se, a mene nemate uvijek.”
Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.”
9 Silno mnoštvo Židova dozna da je Isus ondje pa se okupi, ne samo zbog Isusa, već i zato da vide Lazara kojega on bijaše uskrisio od mrtvih.
Umati mkubwa wa Wayahudi walipojua kwamba Yesu alikuwa huko Bethania, walikuja si tu kwa ajili ya Yesu, lakini pia kumwona Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua.
10 A glavari svećenički odlučiše i Lazara ubiti
Kwa hiyo viongozi wa makuhani wakafanya mpango wa kumuua Lazaro pia,
11 jer su zbog njega mnogi Židovi odlazili i vjerovali u Isusa.
kwa kuwa kutokana na habari za kufufuliwa kwake Wayahudi wengi walikuwa wanamwendea Yesu na kumwamini.
12 Kad je sutradan silan svijet koji dođe na Blagdan čuo da Isus dolazi u Jeruzalem,
Siku iliyofuata umati mkubwa uliokuwa umekuja kwenye Sikukuu walisikia kwamba Yesu angekuja Yerusalemu.
13 uze palmove grančice i iziđe mu u susret. Vikahu: “Hosana! Blagoslovljen Onaj koji dolazi u ime Gospodnje! Kralj Izraelov.”
Basi wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki, huku wakipaza sauti wakisema, “Hosana!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amebarikiwa Mfalme wa Israeli!”
14 A Isus nađe magarčića i sjede na nj kao što je pisano:
Yesu akamkuta mwana-punda akampanda, kama ilivyoandikwa,
15 Ne boj se, kćeri Sionska! Evo, kralj tvoj dolazi jašuć na mladetu magaričinu!
“Usiogope, Ewe binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda!”
16 To učenici njegovi isprva ne razumješe. Ali pošto je Isus bio proslavljen, prisjetiše se da je to bilo o njemu napisano i da mu baš to učiniše.
Wanafunzi wake Yesu mwanzoni hawakuelewa mambo haya, lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka kuwa mambo haya yalikuwa yameandikwa kwa ajili yake na alitendewa yeye.
17 Mnoštvo koje bijaše s njime kad Lazara pozva iz groba i uskrisi od mrtvih pronosilo je svjedočanstvo o tome.
Wale waliokuwepo wakati Yesu alipomwita Lazaro kutoka kaburini na kumfufua kutoka kwa wafu, waliendelea kushuhudia.
18 Stoga mu je i izišao u susret silan svijet: pročulo se da je on učinio to znamenje.
Ni kwa sababu pia walikuwa wamesikia kwamba alikuwa ametenda muujiza huu ndiyo maana umati wa watu ukaenda kumlaki.
19 Farizeji nato rekoše među sobom: “Vidite da ništa ne postižete. Eno, svijet ode za njim!”
Hivyo Mafarisayo walipoona hayo wakaambiana, “Mnaona, hamwezi kufanya lolote. Angalieni, ulimwengu wote unamfuata yeye!”
20 A među onima koji su se došli klanjati na Blagdan bijahu i neki Grci.
Basi palikuwa Wayunani fulani miongoni mwa wale waliokuwa wamekwenda kuabudu wakati wa Sikukuu.
21 Oni pristupe Filipu iz Betsaide galilejske pa ga zamole: “Gospodine, htjeli bismo vidjeti Isusa.”
Hawa wakamjia Filipo, ambaye alikuwa mwenyeji wa Bethsaida huko Galilaya, wakiwa na ombi. Wakamwambia, “Tungependa kumwona Yesu.”
22 Filip ode i kaže to Andriji pa Andrija i Filip odu i kažu Isusu.
Filipo akaenda akamweleza Andrea, nao wote wawili wakamwambia Yesu.
23 Isus im odgovori: “Došao je čas da se proslavi Sin Čovječji.
Yesu akawajibu, “Saa imewadia ya Mwana wa Adamu kutukuzwa.
24 Zaista, zaista, kažem vam: ako pšenično zrno, pavši na zemlju, ne umre, ostaje samo; ako li umre, donosi obilat rod.
Amin, amin nawaambia, mbegu ya ngano isipoanguka ardhini na kufa, hubakia kama mbegu peke yake. Lakini ikifa huzaa mbegu nyingi.
25 Tko ljubi svoj život, izgubit će ga. A tko mrzi svoj život na ovome svijetu, sačuvat će ga za život vječni. (aiōnios )
Mtu yeyote anayependa maisha yake atayapoteza, naye ayachukiaye maisha yake katika ulimwengu huu atayaokoa hata kwa uzima wa milele. (aiōnios )
26 Ako mi tko hoće služiti, neka ide za mnom. I gdje sam ja, ondje će biti i moj služitelj. Ako mi tko hoće služiti, počastit će ga moj Otac.”
Mtu yeyote akinitumikia lazima anifuate, nami mahali nilipo ndipo mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu akinitumikia, Baba yangu atamheshimu.
27 “Duša mi je sada potresena i što da kažem? Oče, izbavi me iz ovoga časa? No, zato dođoh u ovaj čas!
“Sasa roho yangu imefadhaika sana. Niseme nini? ‘Baba, niokoe katika saa hii.’ Lakini ni kwa kusudi hili nimeufikia wakati huu.
28 Oče, proslavi ime svoje!” Uto dođe glas s neba: “Proslavio sam i opet ću proslaviti!”
Baba, litukuze jina lako.” Ndipo ikaja sauti kutoka mbinguni, “Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.”
29 Mnoštvo koje je ondje stajalo i slušalo govoraše: “Zagrmjelo je!” Drugi govorahu: “Anđeo mu je zborio.”
Ule umati wa watu uliokuwa mahali pale uliisikia nao ukasema, “Hiyo ni sauti ya radi,” wengine wakasema, “Malaika ameongea naye.”
30 Isus na to reče: “Ovaj glas nije bio poradi mene, nego poradi vas.”
Yesu akawaambia, “Sauti hii imesikika kwa faida yenu, wala si kwa faida yangu.
31 “Sada je sud ovomu svijetu, sada će knez ovoga svijeta biti izbačen.
Sasa ni saa ya hukumu kwa ajili ya ulimwengu huu, sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje.
32 A ja kad budem uzdignut sa zemlje, sve ću privući k sebi.”
Lakini mimi, nikiinuliwa kutoka nchi, nitawavuta watu wote waje kwangu.”
33 To reče da označi kakvom će smrću umrijeti.
Yesu aliyasema haya akionyesha ni kifo gani atakachokufa.
34 Nato mu mnoštvo odgovori: “Mi smo iz Zakona čuli da Krist ostaje zauvijek. Kako onda ti govoriš da Sin Čovječji treba da bude uzdignut? Tko je taj Sin Čovječji?” (aiōn )
Ule umati wa watu ukapiga kelele ukasema, “Tumesikia kutoka Sheria kwamba ‘Kristo adumu milele,’ wewe wawezaje kusema, ‘Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu’? Huyu ‘Mwana wa Adamu’ ni nani?” (aiōn )
35 Isus im nato reče: “Još je malo vremena svjetlost među vama. Hodite dok imate svjetlost da vas ne obuzme tama. Tko hodi u tami, ne zna kamo ide.
Ndipo Yesu akawaambia, “Bado kitambo kidogo nuru ingalipo pamoja nanyi. Enendeni maadamu mna nuru, msije mkakumbwa na giza. Mtu anayetembea gizani hajui anakokwenda.
36 Dok imate svjetlost, vjerujte u svjetlost da budete sinovi svjetlosti!” To Isus doreče, a onda ode i sakri se od njih.
Wekeni tumaini lenu katika nuru hiyo ili mpate kuwa wana wa nuru.” Baada ya kusema haya, Yesu aliondoka, akajificha wasimwone.
37 Iako je Isus pred njima učinio tolika znamenja, oni ne povjerovaše u njega,
Hata baada ya Yesu kufanya miujiza hii yote mbele yao, bado hawakumwamini.
38 da se ispuni riječ koju kaza prorok Izaija: Gospodine! Tko povjerova našoj poruci? Kome li se otkri ruka Gospodnja?
Hili lilikuwa ili kutimiza lile neno la nabii Isaya lililosema: “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu, na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?”
39 Stoga i ne mogahu vjerovati, jer Izaija dalje kaže:
Kwa hivyo hawakuamini, kwa sababu Isaya anasema mahali pengine:
40 Zaslijepi im oči, stvrdnu srca; da očima ne vide, srcem ne razumiju te se ne obrate pa ih ozdravim.
“Amewafanya vipofu, na kuifanya mioyo yao kuwa migumu, ili wasiweze kuona kwa macho yao, wala kuelewa kwa mioyo yao, wasije wakageuka nami nikawaponya.”
41 Reče to Izaija jer je vidio slavu njegovu te o njemu zborio.
Isaya alisema haya alipoona utukufu wa Yesu na kunena habari zake.
42 Ipak, mnogi su i od glavara vjerovali u njega, ali zbog farizeja nisu to priznavali: da ne budu izopćeni iz sinagoge.
Lakini wengi miongoni mwa viongozi wa Wayahudi walimwamini, lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakukiri waziwazi kwa maana waliogopa kufukuzwa katika masinagogi.
43 Jer više im je bilo do slave ljudske, nego do slave Božje.
Wao walipenda sifa za wanadamu kuliko sifa zitokazo kwa Mungu.
44 A Isus povika: “Tko u mene vjeruje, ne vjeruje u mene, nego u onoga koji me posla;
Yesu akapaza sauti akasema, “Yeyote aniaminiye, haniamini mimi peke yangu, bali yeye aliyenituma.
45 i tko vidi mene, vidi onoga koji me posla.
Yeyote anionaye mimi, amemwona yeye aliyenituma.
46 Ja - Svjetlost - dođoh na svijet da nijedan koji u mene vjeruje u tami ne ostane.
Mimi nimekuja kama nuru ulimwenguni, ili kwamba kila mtu aniaminiye asibaki gizani.
47 I sluša li tko moje riječi, a ne čuva ih, ja ga ne sudim. Ja nisam došao suditi svijetu, nego svijet spasiti.
“Mimi simhukumu mtu yeyote anayesikia maneno yangu na asiyatii, kwa maana sikuja kuuhukumu ulimwengu, bali kuuokoa.
48 Tko mene odbacuje i riječi mojih ne prima, ima svoga suca: riječ koju sam zborio - ona će mu suditi u posljednji dan.
Yuko amhukumuye yeye anikataaye mimi na kutokuyapokea maneno yangu, yaani, yale maneno niliyosema yenyewe yatamhukumu siku ya mwisho.
49 Jer nisam ja zborio sam od sebe, nego onaj koji me posla - Otac - on mi dade zapovijed što da kažem, što da zborim.
Kwa maana sisemi kwa ajili yangu mwenyewe, bali Baba aliyenituma aliniamuru ni nini cha kusema na jinsi ya kukisema.
50 I znam: zapovijed njegova jest život vječni. Što ja dakle zborim, tako zborim kako mi je rekao Otac.” (aiōnios )
Nami ninajua amri zake huongoza hadi kwenye uzima wa milele. Hivyo lolote nisemalo, ndilo lile Baba aliloniambia niseme.” (aiōnios )