< Joel 3 >

1 “Jer, gle, u one dane i u ono vrijeme, kad okrenem udes Judeji i Jeruzalemu,
“Katika siku hizo na wakati huo, nitakaporejesha neema ya Yuda na Yerusalemu,
2 sakupit ću sve narode i povesti ih u dolinu Jošafat. Ondje ću im suditi zbog Izraela, naroda mog i moje baštine, koju rastjeraše među narode i razdijeliše moju zemlju među se.
nitayakusanya mataifa yote na kuyaleta katika Bonde la Yehoshafati Hapo nitaingia kwenye hukumu dhidi yao kuhusu urithi wangu, watu wangu Israeli, kwa kuwa waliwatawanya watu wangu miongoni mwa mataifa na kuigawa nchi yangu.
3 Baciše ždrijeb za moj narod; davali su dječake za bludnice, djevojke prodavali za vino i pili.”
Wanawapigia kura watu wangu na kuwauza wavulana ili kupata makahaba; waliwauza wasichana ili wapate kunywa mvinyo.
4 “I vi, Tire i Sidone, što hoćete od mene? I vi, filistejski kraljevi? Želite li mi se osvetiti? Ako se budete svetili meni, osveta će brzo na vaše glave.
“Sasa una nini dhidi yangu, ee Tiro na Sidoni, nanyi nchi zote za Ufilisti? Je, mnanilipiza kwa yale niliyoyafanya? Kama mnalipa, mimi nitalipiza juu ya vichwa vyenu kwa kasi na kwa haraka yale mliyoyatenda.
5 Na vas što mi oteste srebro i zlato, što odnesoste bogate mi riznice u svoje hramove,
Kwa kuwa mlichukua fedha na dhahabu yangu pia mkabeba hazina zangu nzuri sana mkapeleka kwenye mahekalu yenu.
6 na vas koji prodavaste Grcima sinove Jude i Jeruzalema da biste ih otjerali od domovine njihove.
Mliwauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kwamba mpate kuwapeleka mbali na nchi yao.
7 Gle, ja ih kanim dići s mjesta gdje god ih prodaste, i učinit ću da vam zločin vaš padne na glave.
“Tazama nitawaamsha kutoka zile sehemu mlizowauza, nami nitawalipiza juu ya vichwa vyenu kile mlichofanya.
8 Prodat ću vaše sinove i kćeri sinovima Judinim, a oni će ih prodat' Sabejcima, daleku narodu. Jer Jahve reče!”
Nitawauza wana wenu na binti zenu kwa watu wa Yuda, nao watawauza kwa Waseba, taifa lililo mbali.” Bwana amesema.
9 Razglasite ovo među narodima! Posvetite se za rat! Dižite junake! Naprijed, navalite, svi ratnici!
Tangazeni hili miongoni mwa mataifa: Jiandaeni kwa vita! Amsha askari! Wanaume wote wapiganaji wasogee karibu na kushambulia.
10 Prekujte raonike u mačeve, kosire u koplja, nek' slabić kaže: “Junak sam!”
Majembe yenu yafueni yawe panga na miundu yenu ya kukatia iwe mikuki. Aliye dhaifu na aseme, “Mimi nina nguvu!”
11 Pohitajte i dođite, svi okolni narodi, i ondje se saberite! (Jahve, onamo pošalji svoje junake!)
Njooni haraka, ninyi mataifa yote kutoka pande zote, kusanyikeni huko. Shusha wapiganaji wako, Ee Bwana!
12 “Budite se, narodi, stupajte u Dolinu Jošafat, jer ću ondje sjesti da sudim svim okolnim narodima.
“Mataifa na yaamshwe; na yasonge mbele kuelekea Bonde la Yehoshafati, kwa kuwa nitaketi mahali pale kuhukumu mataifa yote yaliyoko kila upande.
13 Hvatajte se srpa: ljetina je zrela. Ustanite, siđite: tijesak je pun, prelijevaju se kace, jer je velika zloća njihova.”
Tia mundu, kwa kuwa mavuno yamekomaa. Njooni, mkanyage zabibu, kwa kuwa shinikizo la kukamua zabibu limejaa na mapipa yanafurika: kwa kuwa uovu wao ni mkubwa!”
14 Mnoštvo, mnoštvo u Dolini Odluke! Da, blizu je dan Jahvin u Dolini Odluke!
Umati mkubwa, umati mkubwa katika bonde la uamuzi! Kwa kuwa siku ya Bwana ni karibu katika bonde la uamuzi.
15 Sunce i mjesec pomrčaše, zvijezde potamnješe.
Jua na mwezi vitatiwa giza, na nyota hazitatoa mwanga wake tena.
16 Jahve grmi sa Siona, glas diže iz Jeruzalema; nebo se i zemlja tresu. Ali je Jahve utočište svome narodu i zaštita sinovima Izraela.
Bwana atanguruma kutoka Sayuni na mshindo wa ngurumo kutoka Yerusalemu; dunia na mbingu vitatikisika. Lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake, ngome imara kwa ajili ya watu wa Israeli.
17 “Znat ćete tada da sam ja Jahve vaš Bog što stoluje na Sionu, svetoj gori svojoj. Jeruzalem će biti svetište, tuđinac više neće kroza nj proći.”
“Ndipo mtakapojua kwamba Mimi, Bwana Mungu wenu, nakaa Sayuni, mlima wangu mtakatifu. Yerusalemu utakuwa mtakatifu; kamwe wageni hawatavamia tena.
18 Kad dođe taj dan, kapat će gore moštom, iz bregova će brizgati mlijeko, kroza sva korita riječna u Judeji voda će proteći. Vrelo će šiknuti iz kuće Jahvine da natopi Dolinu sitimsku.
“Katika siku hiyo milima itadondosha divai mpya, na vilima vitatiririka maziwa; mabonde yote ya Yuda yatatiririka maji. Chemchemi itatiririka kutoka kwenye nyumba ya Bwana na kunywesha Bonde la Shitimu.
19 Egipat će opustjeti, Edom će postati beživotna pustinja zbog nasilja učinjena sinovima Judinim, jer proliše krv nevinu u njihovoj zemlji.
Lakini Misri itakuwa ukiwa, Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya jeuri waliofanya kwa watu wa Yuda, ambao katika nchi yao walimwaga damu isiyo na hatia.
20 Judeja će dovijek biti naseljena i Jeruzalem u sva koljena.
Yuda itakaliwa na watu milele na Yerusalemu itadumu vizazi vyote.
21 “Osvetit ću krv njihovu za koju se nisam još osvetio.” Jahve će dići Dom svoj na Sionu.
Hatia yao ya damu, ambayo sijasamehe, nitasamehe.”

< Joel 3 >