< Job 6 >

1 A Job progovori i reče:
Kisha Ayubu akajibu:
2 “O, kad bi se jad moj izmjeriti mog'o, a nevolje moje stavit' na tezulju!
“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
3 Teže one jesu od sveg pijeska morskog, i stoga mi riječi zastraniti znaju.
Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 Strijele Svesilnoga u mojem su mesu, ljuti otrov njihov ispija mi dušu, Božje se strahote oborile na me.
Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
5 TÓa, kraj svježe trave njače li magarac, muče li goveče kraj punih jasala?
Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
6 Zar hranu bljutavu jedemo bez soli? Zar kakove slasti ima u bjelancu?
Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
7 Al' ono što mi se gadilo dotaći, to mi je sada sva hrana u bolesti.
Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
8 O, da bi se molba moja uslišala, da mi Bog ispuni ono čem se nadam!
“Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
9 O, kada bi me Bog uništiti htio, kada bi mahnuo rukom da me satre!
kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
10 Za mene bi prava utjeha to bila, klicati bih mog'o u mukama teškim što se ne protivljah odluci Svetoga.
Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
11 Zar snage imam da mogu čekati? Radi kakve svrhe da ja duže živim?
“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
12 Zar je snaga moja k'o snaga kamena, zar je tijelo moje od mjedi liveno?
Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
13 Na što se u sebi osloniti mogu? Zar mi svaka pomoć nije uskraćena?
Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
14 Tko odbija milost bližnjemu svojemu, prezreo je strah od Boga Svesilnoga.
“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
15 Kao potok me iznevjeriše braća, kao bujice zimske svoje korito.
Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
16 Od leda mutne vode im se nadimlju, 'bujaju od snijega što se topit' stao;
wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
17 al u doba sušno naskoro presahnu, od žege ishlape tada iz korita.
lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
18 Karavane zbog njih skreću sa putova, u pustinju zađu i u njoj se gube.
Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
19 Karavane temske očima ih traže, putnici iz Šebe nadaju se njima.
Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
20 A kad do njih dođu, nađu se u čudu, jer su se u nadi svojoj prevarili.
Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
21 U ovom ste času i vi meni takvi: vidjeste strahotu pa se preplašiste.
Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
22 Rekoh li vam možda: 'Darujte mi štogod, poklonite nešto od svojega blaga;
Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
23 iz šake dušmanske izbavite mene, oslobodite me silnikova jarma?'
au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
24 Vi me poučite, pa ću ušutjeti, u čem je moj prijestup, pokažite meni.
“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
25 O, kako su snažne besjede iskrene! Al' kamo to vaši smjeraju prijekori?
Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
26 Mislite li možda prekoriti riječi? TÓa u vjetar ide govor očajnikov!
Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
27 Nad sirotom kocku zar biste bacali i sa prijateljem trgovali svojim?
Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
28 U oči me sada dobro pogledajte, paz'te neću li vam slagati u lice.
“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
29 Povucite riječ! Kakve li nepravde! Povucite riječ, neporočan ja sam!
Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
30 Zar pakosti ima na usnama mojim? Zar nesreću svaku okusio nisam?
Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?

< Job 6 >