< Job 5 >

1 Ded zazivlji! Zar će ti se tko odazvat'? Kojem li se svecu misliš sad obratit'?
“Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
2 Doista, budalu njegov bijes ubija, luđaka će sasvim skončat ljubomora.
Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
3 Bezumnika vidjeh kako korijen pušta, al' prokletstvo skoro na kuću mu pade.
Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
4 Njegovi su sinci daleko od spasa, njih nezaštićene na Vratima tlače.
Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
5 Ljetinu njihovu pojedoše gladni, sam Bog ju je njima oteo iz usta, a žedni hlepe za njihovim dobrima.
Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
6 Ne, opačina ne izbija iz zemlje, nit' nevolja iz tla može nići sama,
Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
7 nego čovjek rađa muku i nevolju kao što let orlov teži u visinu.
Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
8 Al' ja bih se ipak Bogu utekao i pred njime stvar bih svoju razložio.
“Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
9 Nedokučiva on djela silna stvori, čudesa koja se izbrojit' ne mogu.
Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
10 On kišom rosi po svem licu zemljinu i vodu šalje da nam polja natapa.
Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
11 Da bi ponižene visoko digao, da bi ojađene srećom obdario,
Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
12 redom ruši ono što lukavci smisle, što god započeli, on im izjalovi.
Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
13 On hvata mudre u njihovu lukavstvu, naume spletkara obraća u ništa.
Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
14 Posred bijela dana zapadnu u tamu, pipaju u podne kao usred noći.
Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
15 On iz njinih ralja izbavlja jadnika, iz silničkih ruku diže siromaha.
Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
16 Tako se pokaže nada nevoljniku, i nepravda mora zatvoriti usta.
Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
17 Da, blago čovjeku koga Bog odbaci! Stoga ti ne prezri karanje Svesilnog!
“Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
18 On ranjava, ali i ranu povija, udara i svojom zacjeljuje rukom.
Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
19 Iz šest će nevolja tebe izbaviti, ni u sedmoj zlo te dotaknuti neće.
Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
20 U gladi, od smrti on će te spasiti, a u ratu, oštru će te otet maču.
Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
21 Biču zla jezika uklonit će tebe, ispred otimača bez straha ćeš biti.
Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
22 Suši i studeni ti ćeš se smijati i od divljih zvijeri strahovati nećeš.
Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
23 Sklopit' ti ćeš savez s kamenjem na njivi, zvjerad divlja s tobom u miru će biti.
Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
24 U šatoru svome mir ćeš uživati, dom svoj kad pohodiš netaknut će stajat.
Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
25 Koljeno ćeš svoje gledat' gdje se množi i potomstvo gdje ti kao trava raste.
Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
26 U grob ti ćeš leći kada budeš zreo, kao što se žito snosi kad dozori.
Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
27 Sve motrismo ovo: istina je živa! zato sve za dobro svoje ti poslušaj.”
“Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”

< Job 5 >