< Job 40 >

1 I Jahve se obrati Jobu i reče mu:
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 “Zar će se s Jakim preti još kudilac? Tužitelj Božji nek' sam odgovori!”
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 A Job odgovori Jahvi i reče:
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 “Odveć sam malen: što da odgovorim? Rukom ću svoja zatisnuti usta.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 Riječ rekoh - neću više započeti; rekoh dvije - al' neću nastaviti.”
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 Nato Jahve odgovori Jobu iz oluje i reče:
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 “Bokove svoje opaši k'o junak, ja ću te pitat', a ti me pouči.
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 Zar bi i moj sud pogaziti htio, okrivio me da sebe opravdaš?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 Zar ti mišica snagu Božju ima, zar glasom grmjet' možeš poput njega?
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Ogrni se sjajem i veličanstvom, dostojanstvom se odjeni i slavom.
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Plani dÓe bijesom ognja jarosnoga, pogledom jednim snizi oholnika.
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 Ponositoga pogledaj, slomi ga, na mjestu satri svakoga zlikovca.
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 U zemlju sve njih zajedno zakopaj, u mračnu ih pozatvaraj tamnicu.
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 Tada ću i ja tebi odat' hvalu što si se svojom desnicom spasio.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 A sada, dÓe promotri Behemota! Travom se hrani poput govečeta,
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 u bedrima je, gle, snaga njegova, a krepkost mu u mišićju trbušnom.
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 Poput cedra rep podignut ukruti, sva su mu stegna ispreplele žile.
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 Mjedene cijevi kosti su njegove, zglobovi mu od željeza kvrge.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 Prvenac on je Božjega stvaranja; mačem ga je naoružao tvorac.
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 Gore mu danak u hrani donose i sve zvijerje što po njima se igra.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 Pod lotosom on zavaljen počiva, guštik močvarni i glib kriju ga.
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 Sjenu mu pravi lotosovo lišće, pod vrbama on hladuje potočnim.
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 Nabuja li rijeka, on ne strahuje: nimalo njega ne bi zabrinulo da mu u žvale i sav Jordan jurne.
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 Tko bi za oči uhvatio njega i tko bi mu nos sulicom probio?
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?

< Job 40 >