< Job 35 >
1 Elihu nastavi svoju besjedu i reče:
Aidha, Elihu aliendelea kusema,
2 “Zar ti misliš da pravo svoje braniš, da pravednost pred Bogom dokazuješ,
“Je unadhani hii ni sawa unaposema, 'Haki yangu mbele ya Mungu?
3 kada mu kažeš: 'Što ti je to važno, i ako griješim, što ti činim time?'
Kwa kuwa unauliza, 'Inafaa nini kwangu' na 'Ingekuwa nzuri kwangu kama ningekuwa nimetenda dhambi?'
4 Na sve to ja ću odgovorit' tebi i prijateljima tvojim ujedno.
Nitakujibu, wewe pamoja na marafiki zako.
5 Po nebu se obazri i promatraj! Gledaj oblake: od tebe su viši!
Tazama juu angani, na ulione; angalia anga, ambalo liko juu sana kuliko wewe.
6 Ako griješiš, što si mu uradio, prijestupom svojim što si mu zadao?
Kama umetenda dhambi, ni madhara gani huwa unayafanya kwa Mungu? Ikiwa makosa yako yameongezeka zaidi, je huwa unafanya nini kwake?
7 Ako si prav, što si dodao njemu i što iz ruke tvoje on dobiva?
Kama wewe ni mwenye haki, unaweza kumpa nini? Je atapokea nini mkononi mwako?
8 Opakost tvoja tebi slične pogađa i pravda tvoja čovjeku koristi.
Uovu wako waweza kuwaumiza mtu, kama ulivyo wewe ni mtu, na haki yako yaweza kumnufaisha mwana mwingine wa mtu.
9 Ali kad ispod teškog stenju jarma, kad vapiju na nasilje moćnika,
Watu wanalia kwasababu ya matendo mengi ya unyanyasaji; wanaomba msaada katika mikono ya watu wenye nguvu.
10 nitko ne kaže: 'Gdje je Bog, moj tvorac, koji noć pjesmom veselom ispunja,
Lakini hakuna hata mmoja asemaye, ' Mungu Muumba wangu yuko wapi, ambaye hutoa nyimbo wakati wa usiku,
11 umnijim nas od zvijeri zemskih čini i mudrijima od ptica nebeskih?'
ambaye hutufundisha sisi zaidi anavyowafundisha wanyama wa dunia, na ambaye hutufanya sisi kuwa wenye hekima kuliko ndege wa angani?
12 Tad vapiju, al' on ne odgovara poradi oholosti zlikovaca.
Huko wanalia, lakini Mungu hawajibu kwasababu ya kibriu ya watu waovu.
13 Ali kako je isprazno tvrditi da Bog njihove ne čuje vapaje, da pogled na njih ne svraća Svesilni!
Kwa hakika Mungu hatasikia kilio cha kipumbavu; Mwenye nguvu wala hatajali.
14 A kamoli tek kada ti govoriš: 'On ne vidi mene, parnica moja pred njime stoji, a ja na nj još čekam.'
Ni kwa namna gani atakujibu ikiwa unasema haumwoni, na ya kwamba hoja yako iko mbele yake, na ya kuwa unamngojea yeye!
15 Ili: 'Njegova srdžba ne kažnjava, nimalo on za prijestupe ne mari.'
Ni kwa jinsi gani atakujibu kama unasema kwamba hamwadhibu yeyote kwa hasira, na ya kwamba hajishughulishi na kiburi cha watu.
16 Isprazno tada otvara Job usta i besjede gomila nerazumne.”
Basi Ayubu hufumbua kinywa chake tu ili kusema upumbavu; huongeza maneno bila maarifa.”