< Job 31 >
1 Sa svojim očima savez sam sklopio da pogledat neću nijednu djevicu.
Nimefanya patano na macho yangu; ni kwa namna gani tena napaswa kumtazama mwanamwali kwa tamaa?
2 A što mi je Bog odozgo dosudio, kakva mi je baština od Svesilnoga?
Ni sehemu gani kutoka kwa Mungu juu, na urithi gani kutoka kwake mwenye nguvu aliye juu?
3 TÓa nije li nesreća za opakoga, a nevolja za one koji zlo čine?
Nilikuwa nafikiri kwamba majanga ni kwa watu wasio na haki, na misiba ni kwa ajili ya watu watendao mabaya.
4 Ne proniče li on sve moje putove, ne prebraja li on sve moje korake?
Je Mungu hazioni njia zangu na kuzihesabu hatua zangu zote?
5 Zar sam ikad u društvu laži hodio, zar mi je noga k prijevari hitjela?
Kama nimetembea katika udanganyifu, kama mguu wangu umeharakisha katika uongo,
6 Nek' me na ispravnoj mjeri Bog izmjeri pa će uvidjeti neporočnost moju!
na nipimwe katika vipimo vilivyo sawa ili kwamba Mungu aujue uadilifu wangu.
7 Ako mi je korak s puta kad zašao, ako mi se srce za okom povelo, ako mi je ljaga ruke okaljala,
Kama hatua zangu zimegeuka kutoka katika njia sahihi, kama moyo wangu umetembea kwa kufuata macho yangu, na kama doa lolote la uchafu limeng'ang'ania katika mikono yangu,
8 neka drugi jede što sam posijao, neka sve moje iskorijene izdanke!
na kisha mimi nipande na mtu mwingine na ale; mavuno na yang'olewe katika shamba langu.
9 Ako mi zavede srce žena neka, ako za vratima svog bližnjeg kad vrebah,
Na kama moyo wangu umevutiwa na mwanamke mwingine, ikiwa nimelala na mke wa jirani yangu katika hali ya kusubiria katika mlango wake,
10 neka moja žena drugom mlin okreće, neka s drugim svoju podijeli postelju!
na ndipo mke wangu na asage nafaka kwa mwanaume mwingine, na wanaume wengine na walale naye.
11 Djelo bestidno time bih počinio, zločin kojem pravda treba da presudi,
Na kwa hilo litakuwa ni kosa kubwa; kwa kweli, utakuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi.
12 užego vatru što žeže do Propasti i što bi svu moju sažgala ljetinu.
Kwa kuwa ni moto ambao unateketeza kila kitu kwa uharibifu, na kwamba utaunguza mavuno yangu yote.
13 Ako kada prezreh pravo sluge svoga il' služavke, sa mnom kad su se parbili,
Ikiwa nilikataa ombi la haki kutoka kwa watumishi wangu wa kiume na wa kike wakati walipohojiana nami,
14 što ću učiniti kada Bog ustane? Što ću odvratit' kad račun zatraži?
kisha nini basi ningefanya wakati Mungu anapoinuka ili kunishitaki mimi? Atakapokuja kunihukumu, nitamjibuje?
15 Zar nas oba on ne stvori u utrobi i jednako sazda u krilu majčinu?
Je yeye aliyenifanya mimi tumboni hakuwafanya wao pia? Je yeye si yeye yule aliyetuumba sisi wote katika tumbo?
16 Ogluših li se na molbe siromaha ili rasplakah oči udovičine?
kama nimewanyima watu masikini matakwa yao, au kama nimesababisha macho ya wajane yafifie kwa kulia,
17 Jesam li kada sam svoj jeo zalogaj a da ga nisam sa sirotom dijelio?
au ikiwa kama nimekula kipande changu na sijawaruhusu wale wasio na baba kukila pia -
18 TÓa od mladosti k'o otac sam mu bio, vodio sam ga od krila materina!
kwasababu tangu ujana wangu yatima walikua pamoja nami kama kuwa na baba, nami nimemwongoza mama yake, mjane, tangu katika tumbo la mama yangu mwenyewe.
19 Zar sam beskućnika vidio bez odjeće ili siromaha kog bez pokrivača
ikiwa nimemwona yeyote akiangamia kwa kwa kukosa mavazi, au kama nimemwona mtu mhitaji akiwa hana nguo;
20 a da mu bedra ne blagosloviše mene kad se runom mojih ovaca ogrija?
ikiwa moyo wake haujanibariki kwasababu amekuwa hajatiwa joto na sufu ya kondoo zangu,
21 Ako sam ruku na nevina podigao znajuć' da mi je na vratima branitelj,
ikiwa nimeinua juu mkono wangu kinyume na watu wasio na baba kwa kuwa niliona msaada wangu katika lango la mji, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu.
22 nek' se rame moje od pleća odvali i neka mi ruka od lakta otpadne!
Ndipo bega langu na lianguake kutoka katika sehemu yake, na mkono wangu uvunjike katika kiungo chake.
23 Jer strahote Božje na mene bi pale, njegovu ne bih odolio veličanstvu.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu; kwasababu ya mawazo ya ukuu wake, nisingeweza kufanya mambo hayo.
24 Zar sam u zlato pouzdanje stavio i rekao zlatu: 'Sigurnosti moja!'
Kama ningeifanya dhahabu kuwa tumaini langu, na kama ningesema kwa dhahabu safi, 'wewe unanifanya kuwa na tumaini';
25 Zar sam se veliku blagu radovao, bogatstvima koja su mi stekle ruke?
na kama nimefurahi kwasababu ya utajiri wangu ulikuwa mkubwa, kwa kuwa mkono wangu umepata mali nyingi, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu!
26 Zar se, gledajući sunce kako blista i kako mjesec sjajni nebom putuje,
Ikiwa nimeliona jua lilipowaka, au mwezi ukitembea katika mng'ao wake,
27 moje srce dalo potajno zavesti da bih rukom njima poljubac poslao?
na kama moyo wangu umevutwa kwa siri, ili kwamba mdomo wangu umeubusu mkono wangu katika ibada yao -
28 Grijeh bi to bio što za sudom vapije, jer Boga višnjega bih se odrekao.
hili nalo pia lingekuwa ni ubaya wa kuadhibiwa na waamuzi, kwa kuwa ningekuwa nimemkana Mungu aliyejuu.
29 Zar se obradovah nevolji dušmana i likovah kad ga je zlo zadesilo,
Ikiwa nimefurahia uharibifu wa yeyote ambaye ananichukia mimi, au kuwapa hongera wakati majanga yanapowapata, ndipo ulete mashitaka dhidi yangu!
30 ja koji ne dadoh griješiti jeziku, proklinjući ga i želeći da umre?
Kwa kweli sijauruhusu hata mdomo wangu kutenda dhambi kwa kuuomba uhai wake kwa laana.
31 Ne govorahu li ljudi mog šatora: 'TÓa koga nije on mesom nasitio'?
Ikiwa watu wa hema yangu hawajasema,' Nani aweza kumpata mtu ambaye hayashibishwa na chakula cha Ayubu?
32 Nikad nije stranac vani noćivao, putniku sam svoja otvarao vrata.
(hata mgeni hajawahi kukaa katika pembe ya mji, kwa kuwa siku zote nimefungua milango yangu kwa ajili ya wasafiri), na kama haiko hivyo, ndipo mlete mashitaka kinyume nami!
33 Zar sam grijehe svoje ljudima tajio, zar sam u grudima skrivao krivicu
Ikiwa, kama binadamu nimezificha dhambi zangu kwa kuficha hatia ndani ya kanzu yangu -
34 jer sam se plašio govorkanja mnoštva i strahovao od prezira plemenskog te sam mučao ne prelazeć' svoga praga?
kwa kuwa niliogopa kusanyiko kubwa, kwasababu ya matwezo ya familia yaliniogopesha, hivyo basi nilinyamaza kimya na sikuweza kwenda nje, basi nileteni mashitaka dhidi yangu!
35 O, kad bi koga bilo da mene sasluša! Posljednju sam svoju riječ ja izrekao: na Svesilnom je sad da mi odgovori! Nek' mi optužnicu napiše protivnik,
Ee, kama nilikuwa na mtu wa kunisikiliza! Ona, hii ni saini yangu; na Mwenye nguvu na anijibu! Ikiwa nilikuwa na shitaka rasmi ambalo adui yangu ameliandika!
36 i ja ću je nosit' na svome ramenu, čelo ću njome k'o krunom uresit'.
Hakika ningelibeba hadharani juu ya bega langu; ningeliweka juu kama taji.
37 Dat ću mu račun o svojim koracima i poput kneza pred njega ću stupiti.”
Ningemweleza hesabu ya hatua zangu; na kama mwana wa mfalme mwenye kujiamini ningepanda kwenda kwake.
38 Ako je na me zemlja moja vikala, ako su s njom brazde njezine plakale;
Kama nchi yangu ingelia dhidi yangu, na matuta yake yaomboleza pamoja,
39 ako sam plodove jeo ne plativši i ako sam joj ojadio ratare,
ikiwa nimekula mavuno yake bila kulipia au kama nimesababisha wamiliki wake kupoteza maisha yao,
40 [40a] neka mjesto žita po njoj niče korov, a mjesto ječma nek' posvud kukolj raste! [40b] Konac riječi Jobovih.
ndipo miiba na iote badala ya ngano na magugu badala ya shayiri.” Maneno ya Ayubu yamemalizika.