< Job 13 >

1 Očima svojim sve to ja vidjeh, ušima svojim čuh i razumjeh.
“Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
2 Sve što vi znate znadem to i ja, ni u čemu od vas gori nisam.
Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
3 Zato, zborit' moram sa Svesilnim, pred Bogom svoj razlog izložiti.
Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
4 Jer, kovači laži vi ste pravi, i svi ste vi zaludni liječnici!
Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
5 Kada biste bar znali šutjeti, mudrost biste svoju pokazali!
Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
6 Dokaze mi ipak poslušajte, razlog mojih usana počujte.
Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
7 Zar zbog Boga govorite laži, zar zbog njega riječi te prijevarne?
Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
8 Zar biste pristrano branit' htjeli Boga, zar biste mu htjeli biti odvjetnici?
Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
9 Zar bi dobro bilo da vas on ispita? Zar biste ga obmanuli k'o čovjeka?
Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
10 Kaznom preteškom on bi vas pokarao poradi potajne vaše pristranosti.
Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
11 Zar vas veličanstvo njegovo ne plaši i zar vas od njega užas ne spopada?
Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
12 Razlozi su vam od pepela izreke, obrana je vaša obrana od blata.
Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
13 Umuknite sada! Dajte da govorim, pa neka me poslije snađe što mu drago.
“Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
14 Zar da meso svoje sam kidam zubima? Da svojom rukom život upropašćujem?
Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
15 On me ubit' može: nade druge nemam već da pred njim svoje držanje opravdam.
Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
16 I to je već zalog mojega spasenja, jer bezbožnik preda nj ne može stupiti.
Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
17 Pažljivo mi riječi poslušajte, nek' vam prodre u uši besjeda.
Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
18 Gle: ja sam pripremio parnicu, jer u svoje sam pravo uvjeren.
Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
19 Tko se sa mnom hoće parničiti? - Umuknut ću potom te izdahnut'.
Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
20 Dvije mi molbe samo ne uskrati da se od tvog lica ne sakrivam:
“Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
21 digni s mene tešku svoju ruku i užasom svojim ne straši me.
Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
22 Tada me pitaj, a ja ću odgovarat'; ili ja da pitam, ti da odgovaraš.
Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
23 Koliko počinih prijestupa i grijeha? Prekršaj mi moj pokaži i krivicu.
Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
24 Zašto lice svoje kriješ sad od mene, zašto u meni vidiš neprijatelja?
Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
25 Zašto strahom mučiš list vjetrom progonjen, zašto se na suhu obaraš slamčicu?
Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
26 O ti, koji mi gorke pišeš presude i teretiš mene grijesima mladosti,
Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
27 koji si mi noge u klade sapeo i koji bdiš nad svakim mojim korakom i tragove stopa mojih ispituješ!
Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
28 Život mi se k'o trulo drvo raspada, k'o haljina što je moljci izjedaju!
“Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.

< Job 13 >