< Jeremija 3 >

1 “Ako muž otpusti ženu svoju i ona ide od njega te se uda za drugoga, ima li još pravo da se vrati njemu? Nije li ta žena sasvim oskvrnuta? A ti si bludničila s mnogim milosnicima, pa da se meni vratiš?” - riječ je Jahvina.
“Kama mtu akimpa talaka mkewe, naye akamwacha na akaolewa na mtu mwingine, je, huyo mume aweza kumrudia tena? Je, hiyo nchi haitanajisika kabisa? Lakini umeishi kama kahaba na wapenzi wengi: je, sasa utanirudia tena?” asema Bwana.
2 Podigni oči na goleti i pogledaj: gdje te to nisu oskvrnuli? Na putovima si ih dočekivala kao Arapin u pustinji. Ti si oskvrnula zemlju bludom i opačinom svojom,
“Inua macho utazame miinuko iliyo kame na uone. Je, pana mahali ambapo hawajalala nawe? Uliketi kando ya barabara ukiwasubiri wapenzi, ukakaa kama yeye ahamahamaye jangwani. Umeinajisi nchi kwa ukahaba wako na uovu wako.
3 zato i kiše prestadoše i kasni daždevi ne padoše. Čelo ti je kao u bludnice: ni zacrvenjela se nisi.
Kwa hiyo mvua imezuiliwa, nazo mvua za vuli hazikunyesha. Hata hivyo, una uso usio na haya kama wa kahaba; unakataa kutahayari kwa aibu.
4 Ne dovikuješ li mi sada: 'Oče moj, ti si prijatelj mladosti moje!
Je, wewe hujaniita hivi punde tu: ‘Baba yangu, rafiki yangu tangu ujana wangu,
5 Hoće li zauvijek plamtjeti, vječno tinjati gnjev tvoj?' Tako govoriš, a činiš i dalje zla koliko god možeš.”
je, utakasirika siku zote? Je, ghadhabu yako itaendelea milele?’ Hivi ndivyo unavyozungumza, lakini unafanya maovu yote uwezayo.”
6 Jahve mi reče u dane kralja Jošije: “Vidje li što učini odmetnica Izrael? Ona odlazi na svaku visoku goru i pod svako zeleno stablo i ondje se podaje bludu.
Wakati wa utawala wa Mfalme Yosia, Bwana aliniambia, “Umeona kile Israeli asiye mwaminifu amekifanya? Amepanda juu ya kila kilima kirefu, na chini ya kila mti uliotanda na amefanya uzinzi huko.
7 A ja mišljah: 'Poslije svega što učini vratit će se k meni.' Ali se ona ne vraća. I to vidje sestra njena, nevjernica Judeja.
Mimi nilifikiri kuwa baada ya kuyafanya yote haya angelinirudia, lakini hakurudi, naye dada yake Yuda mdanganyifu aliona hili.
8 A vidje i kako otpustih odmetnicu Izraela zbog svih preljuba i dadoh joj knjigu otpusnu. Ali sestra joj, nevjernica Judeja, nimalo se ne poboja, pa i ona okrenu u blud.
Nilimpa Israeli asiye mwaminifu hati yake ya talaka, na kumfukuza kwa ajili ya uzinzi wake wote. Hata hivyo nikaona kuwa Yuda dada yake mdanganyifu hakuogopa. Yeye pia alitoka na kufanya uzinzi.
9 I svojim lakoumnim bludom obeščasti zemlju; činila je preljub s kamenjem i drvljem.
Kwa sababu uasherati wa Israeli haukuwa kitu kwake, Yuda aliinajisi nchi kwa kuzini na mawe na miti.
10 I nakon svega toga nije se vratila k meni nevjernica sestra njezina, Judeja, svim srcem svojim, već samo prijetvorno” - riječ je Jahvina.
Pamoja na hayo yote, Yuda dada yake mdanganyifu hakunirudia kwa moyo wake wote, bali kwa kujifanya tu,” asema Bwana.
11 I reče mi Jahve: “Odmetnica Izrael pravednija je od Judeje nevjernice.
Bwana akaniambia, “Israeli asiye mwaminifu ana haki kuliko Yuda mdanganyifu.
12 Idi i viči prema Sjeveru ove riječi. Reci: Vrati se, odmetnice, Izraele, riječ je Jahvina. Ne gnjevi se više lice moje na vas, jer sam milostiv - riječ je Jahvina - neću se gnjeviti dovijeka.
Nenda, ukatangaze ujumbe huu kuelekea kaskazini: “‘Rudi, Israeli usiye mwaminifu,’ asema Bwana, ‘sitakutazama tena kwa uso uliokunjamana, kwa kuwa mimi ni mwenye huruma,’ asema Bwana, ‘Sitashika hasira yangu milele.
13 Samo priznaj svoju krivnju da si se odvrgla od Jahve, Boga svojega, i odlutala k tuđincima, pod svako drvo zeleno i nisi slušala glasa mojega - riječ je Jahvina.
Ungama dhambi zako tu: kwamba umemwasi Bwana Mungu wako, umetapanya wema wako kwa miungu ya kigeni chini ya kila mti unaotanda, nawe hukunitii mimi,’” asema Bwana.
14 Vratite se, sinovi odmetnici - riječ je Jahvina - jer ja sam vaš Gospodar. Uzet ću vas, po jednoga iz svakoga grada, po dvojicu od svakoga roda, da vas odvedem na Sion.
“Rudini, enyi watu msio waaminifu, kwa kuwa mimi ni mume wenu,” asema Bwana. “Nitawachagua ninyi, mmoja kutoka kwenye mji, na wawili kutoka kwenye ukoo, nami nitawaleta Sayuni.
15 I dat ću vam pastire po srcu svojemu koji će vas pasti razumno i mudro.
Kisha nitawapeni wachungaji wanipendezao moyo wangu, ambao watawaongoza kwa maarifa na ufahamu.
16 A kad se u one dane namnožite i narodite u zemlji - riječ je Jahvina - više se neće govoriti: 'Kovčeg Jahvina Saveza' i nitko neće na nj misliti, nitko ga se neće sjećati ni za njim čeznuti, niti ga ponovo graditi.
Katika siku hizo, idadi yenu itakapokuwa imeongezeka sana katika nchi, watu hawatasema tena, ‘Sanduku la Agano la Bwana,’” asema Bwana. “Halitaingia tena kwenye mawazo yao wala kukumbukwa, hawatalihitaji wala halitatengenezwa jingine.
17 U to će se vrijeme Jeruzalem zvati 'Prijestolje Gospodnje'; i svi će se narodi u njemu sabrati u ime Jahvino, i nijedan se više neće tvrdoglavo povoditi za pokvarenim srcem svojim.
Wakati huo, wataita Yerusalemu kuwa Kiti cha Enzi cha Bwana, nayo mataifa yote watakusanyika Yerusalemu kuliheshimu jina la Bwana. Hawatafuata tena ukaidi wa mioyo yao miovu.
18 U one dane slagat će se dom Judin s domom Izraelovim; i zajedno će krenuti iz Zemlje sjeverne u zemlju koju ocima vašim dadoh u baštinu.”
Katika siku hizo, nyumba ya Yuda itaungana na nyumba ya Israeli, wao kwa pamoja watakuja kutoka nchi ya kaskazini hadi nchi niliyowapa baba zenu kama urithi.
19 A ja rekoh: “Kako da te ubrojim među sinove i dam ti zemlju slasti, baštinu, najljepši biser među narodima! Pomislih: Ti ćeš me zvati 'Oče moj!' i nećeš se više odvratiti od mene.”
“Mimi mwenyewe nilisema, “‘Tazama jinsi nitakavyowatunza kwa furaha kama wana na kuwapa nchi nzuri, urithi ulio mzuri kuliko wa taifa jingine lolote.’ Nilidhani mngeniita ‘Baba,’ na msingegeuka, mkaacha kunifuata.
20 “Ali kao što se žena iznevjeri mužu svome, tako se i vi iznevjeriste meni, dome Izraelov” - riječ je Jahvina.
Lakini kama mwanamke asiye mwaminifu kwa mumewe, vivyo hivyo mmekosa uaminifu kwangu pia, ee nyumba ya Israeli,” asema Bwana.
21 Čuj! Po goletima plač se čuje, zapomaganje djece Izraelove, jer skrenuše s puta svojega. Jahvu, Boga svoga, zaboraviše.
Kilio kinasikika juu ya miinuko iliyo kame, kulia na kuomboleza kwa watu wa Israeli, kwa sababu wamepotoka katika njia zao na wamemsahau Bwana Mungu wao.
22 - Vratite se, sinovi, što se odvratiste, izliječit ću odmetništva vaša! - Evo nas, dolazimo k tebi, jer ti si Jahve, Bog naš!
“Rudini, enyi watu msio waaminifu, nami nitawaponya ukengeufu wenu.” “Naam, tutakuja kwako, kwa maana wewe ni Bwana Mungu wetu.
23 Doista, prijevarni su visovi, graja po brdima. Odista, u Jahvi, Bogu našemu, spasenje je Izraelovo!
Hakika zile ghasia za kuabudu sanamu kwenye vilima na milimani ni udanganyifu; hakika katika Bwana, Mungu wetu, uko wokovu wa Israeli.
24 Baal je proždro trud naših otaca još od mladosti naše: ovce njihove i goveda, nihove kćeri i sinove.
Tangu ujana wetu miungu ya aibu imeyala matunda ya kazi za baba zetu: makundi yao ya kondoo na ngʼombe, wana wao na binti zao.
25 Lezimo u sramotu svoju, nek' nas pokrije ruglo naše! Jer Jahvi, Bogu svome, sagriješismo mi i oci naši, od mladosti svoje do dana današnjeg, i ne slušamo glasa Jahve, Boga svojega.
Sisi na tulale chini katika aibu yetu, na fedheha yetu itufunike. Tumetenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wetu, sisi na mababa zetu; tangu ujana wetu hadi leo hatukumtii Bwana Mungu wetu.”

< Jeremija 3 >