< Jeremija 29 >

1 Evo, ovo su riječi poslanice koju prorok Jeremija iz Jeruzalema posla Ostatku izgnanstva - starješinama, svećenicima i prorocima i svemu preostalom narodu što ga Nabukodonozor iz Jeruzalema bijaše odveo u Babilon,
Haya ndiyo maneno ya ile barua ambayo nabii Yeremia aliituma kutoka Yerusalemu kwenda kwa wazee waliobaki miongoni mwa wale waliohamishwa, na kwa makuhani, manabii na watu wengine wote ambao Nebukadneza alikuwa amewachukua kwenda uhamishoni Babeli kutoka Yerusalemu.
2 pošto kralj Jekonija i kraljica-majka, dvorjanici, odličnici judejski i jeruzalemski, kovači i bravari ostaviše Jeruzalem.
(Hii ilikuwa ni baada ya Mfalme Yekonia na malkia mamaye, maafisa wa mahakama, viongozi wa Yuda na wa Yerusalemu, mafundi na wahunzi kwenda uhamishoni kutoka Yerusalemu.)
3 Poslanica je poslana po Elasi, sinu Šafanovu, i Gemarji, sinu Hilkijinu, koje Sidkija, kralj judejski, posla u Babilon Nabukodonozoru, kralju babilonskom. Evo sadržaja:
Barua ilikabidhiwa kwa Elasa mwana wa Shafani, na kwa Gemaria mwana wa Hilkia, ambao Sedekia mfalme wa Yuda aliwatuma kwa Mfalme Nebukadneza huko Babeli. Barua yenyewe ilisema:
4 “Ovako govori Jahve nad Vojskama, kralj Izraelov: 'Svima izgnanicima koje odvedoh iz Jeruzalema u Babilon!
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, awaambialo wale wote niliowapeleka kutoka Yerusalemu kwenda uhamishoni Babeli:
5 Gradite kuće i nastanite se, sadite vrtove i uživajte urod njihov!
“Jengeni nyumba na mstarehe, pandeni bustani na mle mazao yake.
6 Ženite se i rađajte sinove i kćeri! Ženite svoje sinove i udajite svoje kćeri da i oni rađaju sinove i kćeri! Množite se da se ne smanjite!
Oeni wake na mzae wana na binti, waozeni wana wenu wake, nanyi watoeni binti zenu waolewe, ili nao pia wazae wana na binti. Ongezekeni idadi yenu huko, wala msipungue.
7 Ištite mir zemlji u koju vas izagnah, molite se za nju Jahvi, jer na njezinu miru počiva i vaš mir!'
Pia tafuteni amani na mafanikio ya mji ambamo nimewapeleka uhamishoni. Mwombeni Bwana kwa ajili ya mji huo, kwa sababu ukistawi, ninyi pia mtastawi.”
8 Ovako govori Jahve nad Vojskama, Bog Izraelov: 'Ne dajte da vas obmanjuju vaši proroci koji su među vama, vaši gataoci! Ne povodite se za snovima koje oni sanjaju!
Naam, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Msikubali manabii na wabashiri walioko miongoni mwenu wawadanganye. Msisikilize ndoto ambazo mmewatia moyo kuota.
9 Jer oni vam laž prorokuju u moje ime, a ja ih nisam poslao' - riječ je Jahvina.”
Wanawatabiria ninyi uongo kwa jina langu. Sikuwatuma,” asema Bwana.
10 Jer ovako govori Jahve: 'Istom kad se Babilonu ispuni onih sedamdeset godina, ja ću vas pohoditi te vam ispuniti dobro obećanje da ću vas vratiti na ovo mjesto.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Miaka sabini itakapotimia kwa ajili ya Babeli, nitakuja kwenu na kutimiza ahadi yangu ya rehema ya kuwarudisha mahali hapa.
11 Jer ja znam svoje naume koje s vama namjeravam - riječ je Jahvina - naume mira, a ne nesreće: da vam dadnem budućnost i nadu.
Kwa maana ninajua mipango niliyo nayo kwa ajili yenu,” asema Bwana, “ni mipango ya kuwafanikisha na wala si ya kuwadhuru, ni mipango ya kuwapa tumaini katika siku zijazo.
12 Tada ćete me zazivati, dolaziti k meni, moliti mi se i ja ću vas uslišati.
Kisha mtaniita, na mtakuja na kuniomba, nami nitawasikiliza.
13 Tražit ćete me i naći me jer ćete me tražiti svim srcem svojim.
Mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.
14 I pustit ću da me nađete - riječ je Jahvina. Izmijenit ću udes vaš i sabrati vas iz svih naroda i sa svih mjesta kamo vas odagnah - riječ je Jahvina. I vratit ću vas na mjesto odakle vas u izagnanstvo odvedoh.
Nitaonekana kwenu,” asema Bwana, “nami nitawarudisha watu wenu waliotekwa. Nitawakusanya kutoka mataifa yote na mahali pote nilipokuwa nimewafukuzia, nami nitawarudisha mahali ambapo nilikuwa nimewatoa walipochukuliwa uhamishoni,” asema Bwana.
15 Istina, vi velite: 'Jahve nam podiže proroke u Babilonu.'
Mnaweza mkasema, “Bwana ameinua manabii kwa ajili yetu huku Babeli,”
16 Ovako govori Jahve kralju koji sjedi na prijestolju Davidovu, i svemu narodu koji živi u ovome gradu - braći vašoj što ne moradoše s vama u izgnanstvo.
lakini hili ndilo asemalo Bwana kuhusu mfalme aketiaye kiti cha enzi cha Daudi, na watu wa kwenu wote wanaobaki katika mji huu, ndugu zenu ambao hawakwenda pamoja nanyi uhamishoni.
17 Ovako govori Jahve nad Vojskama: “Evo šaljem na njih mač, glad i kugu; učinit ću da budu kao pokvarene smokve, tako loše da nisu za jelo.
Naam, hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Nitatuma upanga, njaa na tauni dhidi yao, nami nitawafanya kuwa kama tini dhaifu zile ambazo ni mbovu sana zisizofaa kuliwa.
18 I gonit ću ih mačem, glađu i kugom i učinit ću ih užasom svim kraljevstvima zemaljskim, prokletstvom, strahotom, ruglom i sramotom svim narodima kamo ih otjeram.
Nitawafukuza kwa upanga, kwa njaa na kwa tauni, nami nitawafanya kitu cha kuchukiza sana kwa falme zote za dunia, na kuwa kitu cha laana na cha kuogofya, cha dharau na kukemewa, miongoni mwa mataifa yote nitakakowafukuzia.
19 Jer ne poslušaše riječi mojih - riječ je Jahvina - premda sam im svejednako slao sluge svoje proroke, ali ih oni ne poslušaše - riječ je Jahvina.
Kwa kuwa hawakuyasikiliza maneno yangu,” asema Bwana, “maneno ambayo niliwatumia tena na tena kupitia watumishi wangu manabii. Wala ninyi watu wa uhamisho hamkusikiliza pia,” asema Bwana.
20 Ali vi, izgnanici, koje poslah iz Jeruzalema u Babilon, poslušajte svi riječ Jahvinu!”
Kwa hiyo, sikieni neno la Bwana, enyi nyote mlio uhamishoni, niliowapeleka Babeli kutoka Yerusalemu.
21 Ovako govori Jahve nad Vojskama, kralj Izraelov, o Ahabu, sinu Kolajinu, i o Sidkiji, sinu Maasejinu, koji vam laž prorokuje u moje ime: “Evo, predajem ih u ruke Nabukodonozora, kralja babilonskoga, da ih pogubi vama na oči.
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu Ahabu mwana wa Kolaya, na Sedekia mwana wa Maaseya, wanaowatabiria uongo kwa jina langu: “Nitawatia mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atawaua mbele ya macho yenu hasa.
22 I njima će se kao kletvom proklinjati svi izgnanici koji su u Babilonu: 'Neka Jahve učini s tobom kao sa Sidkijom i Ahabom koje kralj babilonski ispeče na vatri
Kwa ajili yao, watu wote wa uhamisho kutoka Yuda walioko Babeli watatumia laana hii: ‘Bwana na akutendee kama Sedekia na Ahabu, ambao mfalme wa Babeli aliwachoma kwa moto.’
23 jer u Izraelu počiniše sramotu čineći preljub sa ženama svojih bližnjih i govoreći u moje ime lažne riječi koje im ja nisam zapovjedio. Ja to znam, i svjedok sam tome' - riječ je Jahvina!”
Kwa kuwa wamefanya mambo maovu kabisa katika Israeli, wamezini na wake za majirani zao, tena kwa Jina langu wamesema uongo, mambo ambayo sikuwaambia kuyafanya. Nami nayajua haya, na ni shahidi wa jambo hilo,” asema Bwana.
24 A Šemaji ćeš Nehelamcu poručiti:
Mwambie Shemaya Mnehelami,
25 “Ovako govori Jahve nad Vojskama, Bog Izraelov: Ti si u svoje ime poslao pisma svemu narodu koji je u Jeruzalemu, i svećeniku Sefaniji, sinu Maasejinu, i svim ostalim svećenicima:
“Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Ulituma barua kwa jina lako mwenyewe kwa watu wote wa Yerusalemu, kwa Sefania mwana wa kuhani Maaseya na kwa makuhani wengine wote. Ulimwambia Sefania,
26 'Jahve te postavi svećenikom namjesto svećenika Jojade da paziš u Domu Jahvinu na svakog luđaka koji se gradi prorokom i da ga baciš u klade, sa željezom oko vrata.
‘Bwana amekuweka wewe uwe kuhani badala ya Yehoyada ili uwe msimamizi wa nyumba ya Bwana. Unapaswa kufunga kwa mikatale na mnyororo wa shingoni mwendawazimu yeyote anayejifanya nabii.
27 Zašto, dakle, nisi spriječio Jeremiju iz Anatota, koji se među vama gradi prorokom?
Kwa nini basi hukumkemea Yeremia Mwanathothi, aliyejifanya kama nabii miongoni mwenu?
28 TÓa on nam je poslao poruku u Babilon: Dugo će još trajati: Gradite kuće i nastanite se! Sadite vrtove i uživajte urod njihov!'”
Ametutumia ujumbe huu huku Babeli: Mtakuwako huko muda mrefu. Kwa hiyo jengeni nyumba mkakae; pandeni mashamba na mle mazao yake.’”
29 Svećenik Sefanija pročita pismo proroku Jeremiji.
Kuhani Sefania, hata hivyo, akamsomea nabii Yeremia ile barua.
30 Tada dođe riječ Jahvina Jeremiji:
Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
31 “Pošalji svim izgnanicima ovu vijest: 'Ovako govori Jahve o Šemaji Nehelamcu: Jer vam Šemaja prorokuje te vam budi varave nade, premda ga ja nisam poslao,
“Tuma ujumbe huu kwa watu wote walio uhamishoni: ‘Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu Shemaya Mnehelami: Kwa sababu Shemaya amewatabiria ninyi, hata ingawa sikumtuma, naye amewafanya kuamini uongo,
32 ovako govori Jahve: Kaznit ću Šemaju Nehelamca, njega i potomstvo njegovo: nitko mu neće preostati usred ovoga naroda da doživi sreću koju spremam narodu svojemu - riječ je Jahvina - jer je propovijedao pobunu protiv Jahve.'”
hili ndilo Bwana asemalo: Hakika nitamwadhibu Shemaya Mnehelami pamoja na uzao wake. Hapatakuwa na yeyote atakayebaki miongoni mwa watu hawa, wala hataona mema nitakayowatendea watu wangu, asema Bwana, kwa sababu ametangaza uasi dhidi yangu.’”

< Jeremija 29 >