< Jeremija 24 >

1 Jahve mi pokaza, i gle: dvije kotarice smokava stajahu pred Domom Jahvinim, pošto Nabukodonozor, kralj babilonski, odvede iz Jeruzalema i izagna u Babilon Jekoniju, sina Jojakimova, kralja judejskoga, zajedno s knezovima judejskim, kovačima i bravarima.
Baada ya Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na maafisa, mafundi stadi na wahunzi wa Yuda, kuchukuliwa kutoka Yerusalemu kwenda Babeli na Nebukadneza mfalme wa Babeli kwenda uhamishoni huko Babeli, Bwana akanionyesha vikapu viwili vya tini vilivyowekwa mbele ya Hekalu la Bwana.
2 U jednoj kotarici bijahu izvrsne smokve, kakve već jesu rane smokve; a u drugoj bijahu pokvarene smokve, tako rđave da se ne mogahu jesti.
Kikapu kimoja kilikuwa na tini nzuri sana, kama zile za mavuno ya kwanza. Kikapu cha pili kilikuwa na tini dhaifu sana, mbovu mno zisizofaa kuliwa.
3 I Jahve me upita: “Jeremija, što vidiš?” A ja odgovorih: “Smokve! Dobre su vrlo dobre, a loše su vrlo loše - tako loše da nisu za jelo.”
Kisha Bwana akaniuliza, “Je, Yeremia, unaona nini?” Nikamjibu, “Ninaona tini zile zilizo nzuri ni nzuri sana, lakini zilizo dhaifu ni mbovu mno zisizofaa kuliwa.”
4 I dođe mi riječ Jahvina:
Kisha neno la Bwana likanijia:
5 Ovako govori Jahve, Bog Izraelov: “Kao na ove dobre smokve, tako ću milostivo pogledati na sužnje judejske koje sam s ovoga mjesta prognao u zemlju kaldejsku.
“Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Kama zilivyo hizi tini nzuri, ndivyo ninavyowaona kuwa bora watu wa uhamisho kutoka Yuda, niliowaondoa kutoka mahali hapa kwenda katika nchi ya Wakaldayo.
6 I milostivo ću svrnuti oči na njih i vratiti ih u ovu zemlju. Ponovo ću ih podići i neću ih više uništiti; opet ću ih posaditi i neću ih više iščupati.
Macho yangu yatakuwa juu yao kwa ajili ya kuwapatia mema, nami nitawarudisha tena katika nchi hii. Nitawajenga wala sitawabomoa, nitawapanda wala sitawangʼoa,
7 I dat ću im srce da me poznaju da sam ja Jahve, da budu narod moj, a ja Bog njihov, jer će se oni svim srcem svojim opet k meni obratiti.
nitawapa moyo wa kunifahamu mimi, kwamba mimi ndimi Bwana. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao, kwa maana watanirudia kwa moyo wao wote.
8 Ali kao s lošim smokvama koje su tako loše da nisu za jelo - da, riječ je Jahvina - tako ću postupiti i sa Sidkijom, kraljem judejskim, s njegovim knezovima i sa svim Jeruzalemcima što preostadoše u ovoj zemlji i s onima što se u Egiptu nastaniše.
“‘Lakini kama zilivyo zile tini dhaifu, ambazo ni mbovu mno zisizofaa kuliwa,’ asema Bwana, ‘ndivyo nitakavyomtendea Sedekia mfalme wa Yuda, maafisa wake na mabaki wengine kutoka Yerusalemu, wawe wamebaki katika nchi hii, au wanaishi Misri.
9 Učinit ću da budu na užas svim kraljevstvima zemaljskim, na sramotu i porugu, na ruglo i kletvu posvuda kamo ih protjeram.
Nitawafanya kuwa chukizo kabisa na kitu cha kulaumiwa katika mataifa yote ya dunia, watakuwa aibu na kitu cha kudharauliwa, chombo cha dhihaka na kulaaniwa, popote nitakapowafukuzia.
10 I poslat ću na njih mač, glad i kugu dok se ne istrijebe sa zemlje koju dadoh njima i ocima njihovim.”
Nitautuma upanga, njaa na tauni dhidi yao hadi wawe wameangamia kutoka nchi niliyowapa wao na baba zao.’”

< Jeremija 24 >