< Jeremija 16 >

1 I dođe mi riječ Jahvina i reče:
Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,
2 “Ne uzimaj sebi žene; i nemaj ni sinova ni kćeri na ovome mjestu.
“Usiwe na mke, wala usiwe na wana au binti hapa.
3 Jer ovako govori Jahve o kćerima i sinovima koji će se roditi na ovome mjestu i o majkama koje će ih rađati i o očevima koji će ih imati u ovoj zemlji:
Kwa kuwa Bwana asema hivi kwa wana na binti ambao wamezaliwa hapa, kwa mama waliowabeba, na kwa baba waliowafanya wazaliwe katika nchi hii,
4 Oni će umrijeti smrću prebolnom, nitko ih neće oplakivati, niti će ih sahraniti. Pretvorit će se u gnoj za oranice, izginut će od mača i gladi, a njihova će trupla biti hrana pticama nebeskim i zvijerima zemaljskim.”
'Watakufa vifo vya magonjwa. Hawataliliwa wala kuzikwa. Watakuwa kama samadi juu ya nchi. Kwa maana wataangamizwa kwa upanga na njaa, na miili yao itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa dunia.'
5 Da, ovako govori Jahve: “Ne smiješ ući u kuću žalosti, ne idi naricati niti ih sažaljevati. Jer ja sam tom narodu uskratio mir svoj - riječ je Jahvina - ljubav i samilost.
Maana Bwana asema hivi, 'Usiingie nyumba yoyote yenye kuomboleza. Usiende kuwaombolezea, wala usihuzunike kwa ajili ya watu hawa. Kwa maana nimeondoa amani yangu, uaminifu wa agano, na huruma, kutoka kwa watu hawa! Ndivyo asemavyo Bwana;
6 Pomrijet će veliko i malo u ovoj zemlji i nitko ih neće pokopati. Nitko neće naricati nad njima, niti će zbog njih praviti ureza, niti kose šišati.
kwa hiyo wakuu na wadogo watakufa katika nchi hii. Wala hawatazikwa, wala hakuna yeyote atakayeomboleza kwa ajili yao. Hakuna mtu atakayejikata-kata au kunyoa vichwa vyao kwa ajili yao.
7 Za onog u žalosti neće kruh lomiti, da ga utješe zbog pokojnika, nitiće mu tko pružiti pehar utjehe zbog smrti njegova oca ili majke njegove.
Hakuna mtu anayepaswa kugawa chakula chochote wakati wa kuomboleza ili kuwafariji kwa sababu ya vifo, na hawatawapa kikombe cha faraja kwa baba yake au mama yake ili kuwafariji.
8 Ne ulazi u kuću slavlja da s njima sjediš i gostiš se.”
Usiende kwenye nyumba ya karamu ili ukae pamoja nao ili kula au kunywa.
9 Jer ovako govori Jahve nad Vojskama, Bog Izraelov: “Evo, učinit ću da s ovog mjesta i pred vašim očima i u ovim danima iščeznu poklici radosti i veselja i glasovi zaručnika i zaručnice.
Kwa maana Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, 'Tazama, mbele yako, siku zako na mahali hapa, nitakomesha sauti ya furaha na sherehe, sauti ya bwana na bibi arusi. '
10 A kad objaviš tom narodu sve ove riječi, pa te upitaju: 'Zašto nam Jahve zaprijeti svom ovom golemom nesrećom; u čemu je zločinstvo naše i u čemu su grijesi naši što ih počinismo protiv Jahve, Boga našega?' -
Kisha itatokea kwamba utawaambia watu hawa maneno haya yote, na watakuambia, 'Mbona Bwana amesema maafa yote haya juu yetu? Uovu wetu ni uovu gani na dhambi yetu tuliyomtendea Bwana, Mungu wetu?'
11 onda im odgovori: 'U tom što me ostaviše oci vaši - riječ je Jahvina - i trčaše za tuđim bogovima da im služe i da im se klanjaju, a mene ostaviše i Zakona se moga ne držaše.
Basi uwaambie, 'hii ndiyo ahadi ya Bwana; Kwa sababu baba zenu waliniacha, nao wakafuata miungu mingine, wakaiabudu na kuisujudia. Waliniacha na hawakuishika sheria yangu.
12 A vi još gore učiniste nego oci vaši, jer evo, svaki se povodi za okorjelošću zloga srca svoga, a mene ne sluša.
Lakini ninyi wenyewe mmeleta uovu zaidi kuliko baba zenu, kwa maana, kila mtu anaenda kwa ukaidi wa moyo wake mbaya; hakuna mtu anayenisikiliza.
13 Zato ću vas istjerati iz ove zemlje u zemlju koja vam je neznana, kao što bijaše i ocima vašim. Ondje ćete služiti tuđim bogovima danju i noću: jer neću vam se više smilovati!'”
Kwa hiyo nitawafukuza kutoka nchi hii mpaka nchi msiyoijua, wewe wala baba zako, nanyi mtaiabudu miungu mingine huko mchana na usiku, kwa maana mimi sitawapa fadhili zangu.'
14 “Zato, evo, dolaze dani - riječ je Jahvina - kad se više neće govoriti: 'Živoga mi Jahve koji sinove Izraelove izvede iz Egipta',
Kwa hiyo tazama! Siku zinakuja-hili ndilo tamko la Bwana-ambapo hawatasema tena, 'Kama Bwana aishivyo, yeye aliyewaleta wana wa Israeli kutoka nchi ya Misri.'
15 nego: 'Živoga mi Jahve koji sinove Izraelove izvede iz zemlje sjeverne i iz svih zemalja kamo ih bijaše prognao.' Vratit ću ih u zemlju njihovu koju dadoh ocima njihovim.
Kwa maana, kama Bwana aishivyo, yeye aliyewaleta wana wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini, na kutoka nchi aliyowaangamiza, nitawarudisha katika nchi niliyowapa baba zao.
16 Evo, poslat ću mnoga ribara - riječ je Jahvina - koji će ih uloviti. A zatim ću dovesti mnoge lovce koji će ih goniti sa svih gora, i sa svih brežuljaka, i iz svih pećinskih rasjeklina.
Angalia! hili ni tamko la Bwana-Nitatuma wavuvi wengi-kwa hiyo watawavua watu. Baada ya hayo nitatuma wawindaji wengi ili waweze kuwinda kati ya milima na vilima vyote, na katika miamba ya mwamba.
17 Jer moje oči prate sve njihove putove: neće mi izmaći, niti se bezakonje njihovo može sakriti od očiju mojih.
Kwa kuwa macho yangu yapo juu ya njia zao zote; hawawezi kujificha mbele yangu. Uovu wao hauwezi kufichika mbele ya macho yangu.
18 Dvostruko ću naplatiti njihovo bezakonje i grijehe njihove, jer su truplima svojih grozota oskvrnuli moju zemlju i moju baštinu ispunili gnusobama.”
Nami kwanza nitawalipa mara mbili uovu na dhambi zao kwa kuwa wameichafua nchi yangu sanamu za machukizo, na kwa kujaza urithi wangu na sanamu zao za machukizo.
19 Jahve, snago moja i moja utvrdo, utočište moje u danima nevolje! K tebi će doći narodi s krajeva zemlje. I govorit će: Samu nam laž oci namriješe, Ništavost i Nemoć.
Ee Bwana, wewe ndiwe ngome yangu, na kimbilio langu, na mahali pa usalama wangu siku ya shida. Mataifa yatakujia kwako kutoka mwisho wa dunia na kusema, 'Hakika baba zetu walirithi udanganyifu. Ubatili mtupu; hakuna faida ndani yao. Je!
20 TÓa stvara li čovjek sam sebi bogove, to nikako nisu bogovi.
Watu hufanya miungu kwa ajili yao wenyewe? Lakini wao sio miungu.
21 Učinit ću, evo, da osjete, da ovaj put zaista oćute moju ruku i snagu moju, i znat će da mi je ime Jahve.
Kwa hiyo tazama! Nitawafanya wajue wakati huu, nitawafanya watambue mkono wangu na nguvu zangu, kwa hiyo watajua kwamba Yahweh ni jina langu.”

< Jeremija 16 >