< Jakovljeva 1 >

1 Jakov, sluga Boga i Gospodina Isusa Krista: dvanaestorma plemena Raseljeništva pozdrav.
Yakobo, mtumwa wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo, kwa makabila kumi na mbili yaliyotawanyika, salaam.
2 Pravom radošću smatrajte, braćo moja, kad upadnete u razne kušnje
Hesabuni kuwa ni furaha zaidi, ndugu zangu, mnapopita katika matatizo mbali mbali,
3 znajući da prokušanost vaše vjere rađa postojanošću.
mkijua kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huwapa uvumilivu.
4 Ali neka postojanost bude na djelu savršena da budete savršeni i potpuni, bez ikakva nedostataka.
Acheni uvumilivu uikamilishe kazi yake, kwamba muweze kukomaa kikamilifu, bila kupungukiwa katika lolote.
5 Nedostaje li komu od vas mudrosti, neka ište od Boga, koji svima daje rado i bez negodovanja, i dat će mu se.
Lakini kama mtu kati yenu anahitaji hekima, aiombe kutoka kwa Mungu, ambaye hutoa kwa ukarimu na pasipo kukemea kwa wote wamwombao, na atawapa hekima.
6 Ali neka ište s vjerom, bez ikakva kolebanja. Jer kolebljivac je sličan morskom valovlju, uzburkanu i gonjenu.
Lakini omba kwa imani, bila shaka, kwa kuwa mwenye kutia shaka ni kama mawimbi katika bahari, huchukuliwa na upepo na kutupwa huku na huko.
7 Neka takav ne misli da će primiti što od Gospodina -
Kwa hakika mtu huyu asifikirie kwamba atapokelewa ombi lake kutoka kwa Bwana;
8 čovjek duše dvoumne, nepostojan na svim putovima svojim.
mtu huyu ana nia mbili, si imara katika njia zake zote.
9 Neka se brat niska soja ponosi svojim uzvišenjem,
Ndugu maskini anapaswa kujivuna katika kusimama kwake juu,
10 a bogataš svojim poniženjem. Ta proći će kao cvijet trave:
wakati huo huo ndugu tajiri katika unyenyekevu wake, kwa sababu atatoweka kama ua la kondeni katika shamba analopita.
11 sunce ogranu žarko te usahnu trava i cvijet njezin uvenu; dražest mu lica propade. Tako će i bogataš na stazama svojim usahnuti.
Jua huchomoza na joto la kuunguza kukausha mimea, na maua huanguka na uzuri wake hufa. Vivyo hivyo watu matajiri watachakaa katikati ya kazi zao.
12 Blago čovjeku koji trpi kušnju: prokušan, primit će vijenac života koji je Gospodin obećao onima što ga ljube.
Amebarikiwa mtu yule anayevumilia majaribu, kwa kuwa baada ya kushinda jaribu hilo, atapokea taji ya uzima, ambayo imeahidiwa kwa wale wampendao Mungu.
13 Neka nitko u napasti ne rekne: “Bog me napastuje.” Ta Bog ne može biti napastovan na zlo, i ne napastuje nikoga.
Mtu yeyote hapaswi kusema anapojaribiwa, “Jaribu hili linatoka kwa Mungu,” kwa sababu Mungu hajaribiwi na uovu, na Mungu mwenyewe hamjaribu yeyote.
14 Nego svakoga napastuje njegova požuda koja ga privlači i mami.
Kila mtu hujaribiwa na tamaa zake mbaya zinazomshawishi na kumvuta mbali.
15 Požuda zatim, zatrudnjevši, rađa grijehom, a grijeh izvršen rađa smrću.
Ndipo baada ya tamaa ya dhambi kubeba mimba, dhambi huzaliwa, na baada ya dhambi kukomaa sawasawa, huishia katika mauti.
16 Ne varajte se, braćo moja ljubljena!
Ndugu zangu wapendwa, msidanganyike.
17 Svaki dobar dar, svaki savršen poklon odozgor je, silazi od Oca svjetlila u kome nema promjene ni sjene od mijene.
Kila zawadi iliyo nzuri na kila zawadi iliyokamilika hutoka juu, hushuka chini kutoka kwa Baba wa nuru. Kamwe habadiliki kama kivuli kibadilikavyo.
18 Po svom naumu on nas porodi riječju Istine da budemo prvina neka njegovih stvorova.
Mungu alichagua kutupa sisi uzima kwa Neno la kweli, ili kwamba tuweze kuwa kama uzao wa kwanza miongoni mwa viumbe vyake.
19 Znajte, braćo moja ljubljena! Svatko neka bude brz da sluša, spor da govori, spor na srdžbu.
Mnajua hili, ndugu zangu wapendwa. Kila mmoja anapaswa kuwa mwepesi wa kusikia, siyo mwepesi wa kuongea wala kukasirika,
20 Jer srdžba čovjekova ne čini pravde Božje.
kwa kuwa hasira ya mwanadamu haiwezi kutenda haki ya Mungu.
21 Zato odložite svaku prljavštinu i preostalu zloću i sa svom krotkošću primite usađenu riječ koja ima moć spasiti duše vaše.
Kwa hiyo wekeni mbali uchafu wa dhambi na ubaya wote ulio mahali popote, na kwa unyenyekevu lipokeeni neno lililopandwa ndani yenu, ambalo lina uwezo wa kuokoa roho zenu.
22 Budite vršitelji riječi, a ne samo slušatelji, zavaravajući sami sebe.
Litiini neno, msilisikie tu, mkijidanganya nafsi zenu wenyewe.
23 Jer ako je tko slušatelj riječi, a ne i izvršitelj, sličan je čovjeku koji motri svoje rođeno lice u zrcalu:
Kwa kuwa kama yeyote alisikiaye neno bila kulitendea kazi ni sawa na mtu ajiangaliaye uso wake halisi katika kioo.
24 promotri se, ode i odmah zaboravi kakav bijaše.
Hujitathimini uso wake, na huenda zake na baada ya muda mfupi husahau anavyofanana.
25 A koji se oglÄedÄa u savršenom zakonu slobode i uza nj prione, ne kao zaboravan slušatelj nego djelotvoran izvršitelj, blažen će biti u svem djelovanju svome.
Bali mtu yule anayeiangalia kwa uangalifu sheria kamili, sheria ya uhuru, na kuendelea kuitii, si kwa sababu yeye ni msikilizaji anayesahau, huyu mtu atabarikiwa anapoitenda.
26 Smatra li se tko bogoljubnim, a ne obuzdava svoga jezika, nego zavarava srce svoje, isprazna je njegova bogoljubnost.
Ikiwa mtu yeyote atafikiri mwenyewe kuwa ni mtu wa dini, lakini hawezi kuutawala ulimi wake, huudanganya moyo wake na dini yake ni bure.
27 Bogoljubnost čista i neokaljana jest: zauzimati se za sirote i udovice u njihovoj nevolji, čuvati se neokaljanim od ovoga svijeta.
Dini iliyo safi na isiyoharibiwa mbele za Mungu wetu na Baba ni hii: kuwasaidia yatima na wajane katika mateso yao, na kujilinda wenyewe na ufisadi wa dunia.

< Jakovljeva 1 >