< Izaija 48 >

1 Čujte ovo, kućo Jakovljeva, vi koji se zovete imenom Izraelovim i koji ste izišli iz voda Judinih! Vi koji se Jahvinim imenom kunete i slavite Boga Izraelova, ali ne u istini i pravdi.
“Sikilizeni hili, ee nyumba ya Yakobo, ninyi mnaoitwa kwa jina la Israeli, na mnaotoka katika ukoo wa Yuda, ninyi mnaoapa kwa jina la Bwana, mnaomwomba Mungu wa Israeli, lakini si katika kweli au kwa haki;
2 Jer vi se nazivate po Svetome gradu i oslanjate se na Boga Izraelova, Jahve nad Vojskama njemu je ime.
ninyi mnaojiita raiya wa mji mtakatifu, na kumtegemea Mungu wa Israeli, Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake:
3 Dogođaje prošle odavna sam navijestio, iz mojih su izišli usta i ja sam ih objavio, učinih brzo, i zbi se.
Nilitoa unabii mambo ya kwanza tangu zamani, kinywa changu kiliyatangaza na kuyafanya yajulikane; kisha ghafula nikayatenda, nayo yakatokea.
4 Jer znao sam da si tvrdokoran, da ti je šija žila gvozdena i čelo da ti je mjedeno.
Kwa kuwa nalijua jinsi ulivyokuwa mkaidi; mishipa ya shingo yako ilikuwa chuma, kipaji chako cha uso kilikuwa shaba.
5 Zato sam ti već onda navijestio, javio ti prije nego što se zbilo, da ne bi rekao: “Moj kip učini to, rezani moj lik i ljeveni kip zapovjediše tako!”
Kwa hiyo nilikuambia mambo haya tangu zamani, kabla hayajatokea nilikutangazia ili usije ukasema, ‘Sanamu zangu zilifanya hayo; kinyago changu cha mti na mungu wangu wa chuma aliyaamuru.’
6 Čuo si i vidio sve to; zar ne priznaješ? A sada navijestit ću ti nešto novo, otajno, što još ne znaš;
Umesikia mambo haya; yaangalie hayo yote. Je, hutayakubali? “Kuanzia sasa na kuendelea nitakueleza mambo mapya, juu ya mambo yaliyofichika usiyoyajua.
7 ovog je trena stvoreno, a ne odavna, o tome dosad nisi ništa čuo, da ne bi rekao: “Znao sam.”
Yameumbwa sasa, wala si tangu zamani; hukupata kuyasikia kabla ya siku ya leo. Hivyo huwezi kusema, ‘Naam, niliyajua hayo.’
8 Nisi o tome čuo ni znao, niti se uho tvoje prije otvorilo, jer znadoh da ćeš se iznevjeriti i da te od utrobe majčine zovu otpadnikom.
Hujayasikia wala kuyaelewa, tangu zamani sikio lako halikufunguka. Ninafahamu vyema jinsi ulivyo mdanganyifu, uliitwa mwasi tangu kuzaliwa kwako.
9 Radi imena svoga odgađah svoj gnjev, radi časti svoje susprezah se da te ne uništim.
Kwa ajili ya Jina langu mwenyewe ninaichelewesha ghadhabu yangu, kwa ajili ya sifa zangu nimeizuia isikupate, ili nisije nikakukatilia mbali.
10 Gle, pročistio sam te poput srebra, iskušao te u talioniku nevolje.
Tazama, nimekusafisha, ingawa si kama fedha, nimekujaribu katika tanuru ya mateso.
11 Sebe radi činih tako, sebe radi! TÓa zar da se ime moje obeščasti? Slave svoje drugome ne dam!
Kwa ajili yangu mwenyewe, kwa ajili yangu mwenyewe, nafanya hili. Jinsi gani niliache Jina langu lichafuliwe? Sitautoa utukufu wangu kwa mwingine.
12 Čuj me, Jakove, Izraele, koga sam pozvao: Ja jesam, ja sam prvi, ja sam i posljednji.
“Ee Yakobo, nisikilize mimi, Israeli, ambaye nimekuita: Mimi ndiye; mimi ndimi mwanzo na mwisho.
13 Ruka moja zemlju utemelji, desnica mi razape nebesa. Pozovem ih samo, i odmah dolaze.
Mkono wangu mwenyewe uliweka misingi ya dunia, nao mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu; niziitapo, zote husimama pamoja.
14 Saberite se svi i čujte: tko je od njih to prorekao? “Onaj koga Jahve ljubi ispunit će volju moju nad Babilonom i nad potomstvom kaldejskim.”
“Kusanyikeni, ninyi nyote, msikilize: Ni ipi miongoni mwa hizo sanamu ambayo imetabiri vitu hivi? Watu wa Bwana waliochaguliwa na kuungana watatimiza kusudi lake dhidi ya Babeli; mkono wa Mungu utakuwa dhidi ya Wakaldayo.
15 Ja rekoh i pozvah ga, vodih ga i pomogoh u naumu.
Mimi, naam, Mimi, nimenena; naam, nimemwita yeye. Nitamleta, naye atafanikiwa katika lile nililomtuma.
16 Pristupite k meni i počujte ovo: “Od početka nisam vam govorio tajno, i kad se zbivalo, bijah ondje.” - “A sada me Gospod Jahve šalje s duhom svojim.”
“Nikaribieni na msikilize hili: “Tangu tangazo la kwanza sikusema kwa siri; wakati litokeapo, nitakuwako hapo.” Sasa Bwana Mwenyezi amenituma, kwa Roho wake.
17 Ovako govori Jahve, otkupitelj tvoj, Svetac Izraelov: “Ja, Jahve, Bog tvoj, tvojem dobru te učim, vodim te putem kojim ti je ići.
Hili ndilo asemalo Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye katika njia ikupasayo kuiendea.
18 O, da si pazio na zapovijedi moje, kao rijeka sreća bi tvoja bila, a pravda tvoja kao morski valovi!
Laiti ungesikiliza kwa makini maagizo yangu, amani yako ingekuwa kama mto, haki yako kama mawimbi ya bahari.
19 Potomstva bi tvojeg bilo kao pijeska, a poroda utrobe tvoje kao njegovih zrnaca! Nikad ti se ime ne bi zatrlo niti izbrisalo preda mnom!”
Wazao wako wangekuwa kama mchanga, watoto wako kama chembe zake zisizohesabika; kamwe jina lao lisingefutiliwa mbali, wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.”
20 Izađite iz Babilona, bježite iz Kaldeje! Glasno kličući, kazujte, objavljujte, do nakraj zemlje razglasite! Govorite: “Jahve je otkupio slugu svoga Jakova!
Tokeni huko Babeli, kimbieni kutoka kwa Wakaldayo! Tangazeni hili kwa kelele za shangwe na kulihubiri. Lipelekeni mpaka miisho ya dunia; semeni, “Bwana amemkomboa mtumishi wake Yakobo.”
21 Nisu žeđali dok ih je kroz pustinju vodio; iz stijene je za njih vodu izbio, rascijepio je pećinu i potekla je voda.”
Hawakuona kiu alipowaongoza kupita jangwani; alifanya maji yatiririke kutoka kwenye mwamba kwa ajili yao; akapasua mwamba na maji yakatoka kwa nguvu.
22 “Nema mira opakima,” kaže Jahve.
“Hakuna amani kwa waovu,” asema Bwana.

< Izaija 48 >