< Izaija 26 >

1 U onaj dan pjevat ću ovu pjesmu u zemlji Judinoj: “Tvrd grad mi imamo: za obranu nam On podiže zidove i predziđa.
Siku hiyo wimbo huu utaimbwa katika nchi ya Yuda: Tuna mji imara; Mungu amefanya wokovu katika kuta na ngome zake.
2 Otvorite vrata! Nek' uđe narod pravedni koji čuva vjernost,
Fungua lango, ili mataifa yenye haki yaweze na yenye kutunza imani yaweze kuingia ndani.
3 čiji je značaj čvrst, koji čuva mir jer se u te uzda.
Akili mlionayo, mtamuhifadhi yeye katika amani kamili, maana anawamini ninyi.
4 Uzdajte se u Jahvu dovijeka, jer Jahve je Stijena vječna;
Mwamini Yahwe daima; maana Yaha, Yahwe, ni mwamba wa milele.
5 on obara one koji obitavahu visoko, razvaljuje tvrđu visoku, ruši u prah, sravnjuje sa zemljom,
Maana atawashusha wale wote wenye kiburi; mji ulio juu atushusha chini, ataushusha chini kwenye aridhi; na ataulinganisha na mavumbi.
6 te je gaze noge, noge ubogih i koraci nevoljnih.”
Utakanyagwakanyagwa chini na miguu ya walio masikini na wahitaji.
7 Put je pravednikov prav, ti ravniš stazu pravednom.
Mapito ya mwenye haki yamenyooka, Wenye haki; mapito ya wenye haki umeyanyoosha.
8 Da, na stazi tvojih sudova željno te, Jahve, čekamo; ime tvoje i spomen tvoj duša nam žudi.
Ndio, kaika mapito ya hukumu yako, Yahwe, tunakusubiri wewe; jina lako na sifa zako ni matamanio yetu.
9 Dušom svojom žudim tebe noću i duhom svojim u sebi te tražim. Jer kad se na zemlji pojave tvoji sudovi, uče se pravdi stanovnici kruga zemaljskoga.
Nimekutamani wewe wakati wa usiku; ndio, roho iliyo ndani yangu ina kutafuta kwa bidii. Pindi hukumu yako itakapokuja duniani, wenyeji wa duniani watajua kuhusu haki.
10 Ako se pomiluje opaki, on se ne uči pravednosti. U zemlji pravednosti on čini bezakonje i ne obazire se na veličanstvo Jahvino.
Na tuonyeshe upendeleo kwa waovu, lakini hawatajifunza haki. katika nchi ya wanyofu anatenda maovu na haoni ukuu wa Yahwe.
11 Jahve, ruka je tvoja podignuta, a oni je ne vide. Nek' vide i postide se, nek' ih proguta revnost za narod, nek' ih proždre oganj pripravljen dušmanima tvojim.
Yahwe, mkono wako umenyanyuliwa juu, lakini hawapati hizo taarifa. Lakini wataona bidii kwa watu na wataona aibu, kwa sababu idadi ya maadui watawatafuna.
12 Jahve, ti mir nama daješ, jer ti si tvorac svih djela naših.
Yahwe, utaleta amani kwetu, maana kweli, umekamilisha kazi zetu zote.
13 Jahve, Bože naš, gospodarili su nama osim tebe drugi gospodari, ali tebe jedinog, ime tvoje, častimo.
Yahwe Mungu wetu, viongozi wengine badala yako wametutawala sisi; Lakini tunalitukuza jina lako.
14 Mrtvi neće oživjeti, sjene neće uskrsnuti, jer ti si ih kaznio i uništio i zatro svaki spomen na njih!
Wamekufa, hawataishi tena; ni maremu hao, hawatafufuka tena. Kweli, umekuja kuwahukumu na kuwaharibu wao, na umefanya kila kumbukumbu kutoweka.
15 Umnožio si narod, Jahve, umnožio si narod, proslavio se, proširio sve granice zemlje!
Umeliongeza taifa, Yahwe, umeliongeza taifa; umeheshimiwa; umeinuliwa katika mipaka yote ya nchi.
16 Jahve, tražili su te u nevolji; izlijevali tihu molitvu, kad ih je stigla tvoja kazna.
Yahwe, katika mateso yao walikuangalia wewe; walipatwa na wasiwasi katika maombi yao maana adhabu yako ilikuwa juu yao.
17 Kao što se trudna žena pred porođajem grči i viče u bolovima, takvi smo, Jahve, pred tobom.
Kama mwanamke mjamzito anayekaribia kujifungua, hupatwa na uchungu na hulia kwa uchungu, hivyo ndivyo tulivyokuwa kabla, Bwana.
18 Zatrudnjeli smo, u mukama smo kao da rađamo, nismo donijeli duha spasenja zemlji nit' se rodiše stanovnici svijeta.
Tulikuwa wajawazito, tumekuwa katika mateso, lakini ni kama tumeshajifungua katika akili zetu. Hatujauleta wokovu duniani, na wakazi wa duniani hawakuanguka.
19 Tvoji će mrtvi oživjeti, uskrsnut će tijela. Probudite se i kličite, stanovnici praha! Jer rosa je tvoja - rosa svjetlosti, i zemlja će sjene na svijet dati.
Wafu wenu wataishi; watu wenu walio kufa watafufuka. Amka na uimbe kwa furaha, njie muishio mavumbini; maana umande wenu ni umande wa mwanga, na dunia itawaleta mbele wafu wake.
20 Hajde, narode moj, uđi u sobe i vrata za sobom zatvori. Sakrij se časkom dok jarost ne prođe.
Enendeni, watu wangu, ingieni katika vyumba vyenu na mfunge mlango nyuma yenu; jificheni kwa mda mfupi, mpaka hasira itakapopita.
21 Jer, gle, izići će Jahve iz svog prebivališta da stanovnike zemljine kazni što se o njeg' ogriješiše. Izbacit će zemlja svu krv što je na njoj prolivena i neće više kriti onih koji su na njoj poklani.
Maana, angalia, Yahwe anakaribia kutoka katika eneo lake kuwahadhibu watu waishio duniani kwa ajili ya makosa yao; dunia itaachia umwagaji wa damu, na hawatawaficha tena waliokufa.

< Izaija 26 >