< Postanak 48 >

1 Poslije nekog vremena jave Josipu: “Eno ti je otac obolio.” Nato on uzme sa sobom svoja dva sina, Manašea i Efrajima.
Baada ya muda Yosefu akaambiwa kwamba, “Baba yako ni mgonjwa.” Kwa hiyo akawachukua wanawe wawili Manase na Efraimu, pamoja naye.
2 Kad Jakovu rekoše: “Evo ti je došao sin Josip”, Izrael skupi svoje snage i sjede na postelju.
Yakobo alipoambiwa, “Mwanao Yosefu amekujia kukuona,” Israeli akakusanya nguvu zake, akaketi kitandani.
3 Reče Jakov Josipu: “Bog Svemožni, El Šadaj, objavi mi se u Luzu, u zemlji kanaanskoj; blagoslov mi dade,
Yakobo akamwambia Yosefu, “Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani, huko akanibariki,
4 a potom mi reče: 'Učinit ću te rodnim i mnogobrojnim, učinit ću da postaneš skup naroda, a tvome potomstvu poslije tebe dat ću ovu zemlju u posjed zauvijek.'
naye akaniambia, ‘Nitakufanya ustawi na kuongezeka hesabu yako, nitakufanya kuwa jamii ya mataifa, nami nitakupa nchi hii uimiliki milele wewe na wazao wako baada yako.’
5 Sad, oba tvoja sina što su ti se rodila u zemlji egipatskoj, prije nego sam ja stigao k tebi u Egipat, neka budu moji - Efrajim i Manaše neka budu moji kao i Ruben i Šimun!
“Sasa basi, wanao wawili waliozaliwa kwako huku Misri kabla sijaja hapa kwako watahesabiwa kuwa ni wangu; Efraimu na Manase watakuwa wangu, kama vile Reubeni na Simeoni walivyo wangu.
6 A djeca što su ti se rodila poslije njih neka ostanu tvoja; a u svom nasljedstvu neka se zovu po imenu svoje braće.
Lakini watoto utakaowazaa baada yao watakuwa wako. Katika nchi watakayoirithi, watatambuliwa kwa jina la ndugu zao.
7 Kad sam se, naime, vraćao iz Padana, na moju žalost, tvoja majka Rahela umrije na putovanju u kanaansku zemlju, tek u maloj udaljenosti od Efrate. Sahranio sam je ondje uz put u Efratu, sadašnji Betlehem.”
Nilipokuwa ninarudi kutoka Padani, katika huzuni yangu Raheli alifariki katika nchi ya Kanaani tulipokuwa tungali tukisafiri, tukiwa karibu kufika Efrathi. Kwa hiyo nilimzika huko, kando ya njia iendayo Efrathi” (yaani Bethlehemu).
8 Opazivši Izrael Josipove sinove, zapita: “Tko su ovi?”
Wakati Israeli alipowaona wana wa Yosefu, akauliza, “Hawa ni nani?”
9 Josip odgovori svome ocu: “Sinovi su to moji koje mi je Bog dao ovdje.” “Dovedi mi ih da ih blagoslovim”, reče.
Yosefu akamjibu baba yake, “Hawa ni wana ambao Mungu amenipa nikiwa huku.” Ndipo Israeli akasema, “Walete kwangu ili niwabariki.”
10 Izraelu oči oslabile od starosti, nije vidio. Zato mu privede sinove, a on ih poljubi i zagrli.
Basi macho ya Israeli yalikuwa hayaoni vizuri kwa sababu ya uzee, naye aliona kwa shida. Kwa hiyo Yosefu akawaleta wanawe karibu na baba yake, Israeli akawabusu na akawakumbatia.
11 Potom Izrael reče Josipu: “Nisam očekivao da ću još ikada vidjeti tvoje lice; kad, evo, Bog mi dade da vidim i tvoje potomke.”
Israeli akamwambia Yosefu, “Kamwe sikutazamia kuuona uso wako tena, lakini sasa Mungu ameniruhusu kuwaona watoto wako pia.”
12 Josip ih tada skine s njegovih koljena i duboko se, sve do zemlje, nakloni.
Ndipo Yosefu akawaondoa wanawe magotini mwa Israeli naye akasujudu hadi nchi.
13 Nato ih uze Josip obojicu - Efrajima svojom desnicom, Izraelu nalijevo, a Manašea svojom ljevicom, Izraelu nadesno - te ih k njemu primače.
Yosefu akachukua wale wana wawili, Efraimu kwenye mkono wake wa kuume akimwelekeza kwenye mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kushoto akimwelekeza kwenye mkono wa kuume wa Israeli, akawaleta karibu na babu yao.
14 Ali Izrael ispruži svoju desnicu i stavi je na Efrajimovu glavu, premda je bio mlađi, a svoju ljevicu na glavu Manašeovu - tako je držao ruke unakrst - iako je Manaše bio prvorođenac.
Lakini Israeli akaupeleka mkono wake wa kuume, akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, ingawa alikuwa ndiye mdogo, na mkono wake wa kushoto akaukatisha, akauweka juu ya kichwa cha Manase, ingawa Manase alikuwa ndiye mzaliwa wa kwanza.
15 Tako je davao svoj blagoslov Josipu govoreći: “Bog, čijim su putovima hodili oci moji Abraham i Izak, Bog, koji mi je pastir bio otkako postah pa do danas,
Ndipo akambariki Yosefu akisema, “Mungu ambaye baba zangu Abrahamu na Isaki walimtii, Mungu ambaye amekuwa mchungaji wa maisha yangu yote mpaka leo hii,
16 anđeo koji me od svakog zla izbavljao - djecu ovu neka blagoslovi! Neka se ime moje i mojih pređa Abrahama i Izaka po njima spominje! U mnoštva se mnogobrojna po zemlji razmnožili!”
Malaika ambaye aliniokoa kutoka madhara yote, yeye na awabariki vijana hawa. Na waitwe kwa jina langu na kwa majina ya baba zangu Abrahamu na Isaki, wao na waongezeke kwa wingi katika dunia.”
17 Kad je Josip vidio da je njegov otac položio desnicu na Efrajimovu glavu, njegovim se očima to učini krivo; zato posegne za rukom svoga oca da je pomakne s Efrajimove glave na glavu Manašeovu.
Yosefu alipoona baba yake akiweka mkono wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, hakupendezwa, kwa hiyo akauchukua mkono wa baba yake kutoka kichwa cha Efraimu na kuuweka juu ya kichwa cha Manase.
18 “Ne tako, oče moj,” reče Josip svome ocu, “jer ovo je prvorođenac; zato stavi desnicu na njegovu glavu!”
Yosefu akamwambia, “Hapana, baba yangu, huyu ndiye mzaliwa wa kwanza; uweke mkono wako wa kuume juu ya kichwa chake.”
19 Ali njegov otac to odbije rekavši: “Znam ja, sine moj, znam; i od njega će postati narod i bit će velik. Ali njegov mlađi brat bit će veći od njega, a njegovo će potomstvo biti mnoštvo.”
Lakini baba yake akakataa, akasema, “Ninajua, mwanangu, ninajua. Yeye pia atakuwa taifa, naye pia atakuwa mkuu. Hata hivyo, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye, nao wazao wake watakuwa kundi la mataifa.”
20 Onoga ih, dakle, dana blagoslovi rekavši: “Vama nek' se Izrael blagoslivlja govoreći: Kao što je Efrajimu i Manašeu, nek' i tebi Bog učini!” Tako stavi Efrajima pred Manašea.
Akawabarikia siku ile na kusema, “Kwa jina lenu Israeli watatamka baraka hii: ‘Mungu na awafanye kama Efraimu na Manase.’” Kwa hiyo akamtanguliza Efraimu mbele ya Manase.
21 Poslije Izrael reče Josipu: “Ja ću, evo, naskoro umrijeti; no Bog će biti s vama i opet vas dovesti u zemlju vaših otaca.
Ndipo Israeli akamwambia Yosefu, “Mimi ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa pamoja nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu.
22 A tebi ostavljam Šekem, nešto više nego tvojoj braći, što sam ga svojim mačem i lukom osvojio od Amorejaca.”
Kwako wewe, kama aliye juu ya ndugu zako, ninakupa sehemu moja zaidi ya ndugu zako, lile eneo nililoteka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”

< Postanak 48 >