< Postanak 46 >

1 Tako Izrael krene na put sa svim što bijaše njegovo i stigne u Beer Šebu te prinese žrtvu Bogu svoga oca Izaka.
Hivyo Israeli akaondoka na vyote vilivyokuwa mali yake, naye alipofika Beer-Sheba, akamtolea dhabihu Mungu wa Isaki baba yake.
2 U noćnom viđenju zovne Bog Izraela: “Jakove! Jakove!” On odgovori: “Evo me!”
Mungu akanena na Israeli katika maono usiku na kusema, “Yakobo! Yakobo!” Akajibu, “Mimi hapa.”
3 “Ja sam Bog, Bog tvoga oca. Ne boj se sići u Egipat, jer ću ondje od tebe proizvesti velik narod.
Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa baba yako, usiogope kushuka Misri, kwa maana huko nitakufanya taifa kubwa.
4 Ja ću sići u Egipat s tobom i sam ću te vratiti ovamo; a Josip će ti svojom rukom oči zaklopiti.”
Nitashuka Misri pamoja nawe, nami hakika nitakurudisha tena Kanaani. Mikono ya Yosefu mwenyewe ndiyo itakayofunga macho yako.”
5 I Jakov krene iz Beer Šebe. Sinovi Izraelovi postave svoga oca Jakova, svoju djecu i svoje žene u kola što ih je faraon poslao da ga prevezu.
Ndipo Yakobo akaondoka Beer-Sheba nao wana wa Israeli wakamchukua baba yao Yakobo na watoto wao na wake zao katika magari ya kukokotwa yale Farao aliyokuwa amempelekea kumsafirisha.
6 Uzmu sa sobom svoje blago i dobra što ih bijahu stekli u zemlji kanaanskoj te stignu Jakov i sve njegovo potomstvo u Egipat.
Wakachukua pia mifugo yao na mali walizokuwa wamezipata Kanaani, Yakobo na uzao wake wote wakashuka Misri.
7 Sa sobom je u Egipat poveo svoje sinove i unuke, svoje kćeri i kćeri svojih sinova, sve svoje potomstvo.
Akawachukua wanawe na binti zake, wajukuu wake wa kiume na wa kike, yaani uzao wake wote mpaka Misri.
8 Ovo su imena Izraelaca - Jakova i njegovih potomaka - koji su stigli u Egipat: Jakovljev prvorođenac Ruben.
Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli (Yakobo na wazao wake), waliokwenda Misri: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo.
9 Rubenovi sinovi: Henok, Falu, Hesron i Karmi.
Wana wa Reubeni ni: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
10 Sinovi Šimunovi: Jemuel, Jamin, Ohad, Jakin, Sohar i Šaul, sin Kanaanke.
Wana wa Simeoni ni: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani.
11 Sinovi Levijevi: Geršon, Kehat i Merari.
Wana wa Lawi ni: Gershoni, Kohathi na Merari.
12 Sinovi Judini: Er, Onan, Šela, Peres i Zerah. Er i Onan umrli su u zemlji kanaanskoj. Peresovi sinovi bili su Hesron i Hamul.
Wana wa Yuda ni: Eri, Onani, Shela, Peresi na Zera (lakini Eri na Onani walifariki katika nchi ya Kanaani). Wana wa Peresi ni: Hesroni na Hamuli.
13 Sinovi Jisakarovi: Tola, Fuva, Jašub i Šimron.
Wana wa Isakari ni: Tola, Puva, Yashubu na Shimroni.
14 Sinovi Zebulunovi: Sered, Elon i Jahleel.
Wana wa Zabuloni ni: Seredi, Eloni na Yaleeli.
15 To su sinovi koje je Lea imala s Jakovom u Padan Aramu i još kćerka Dina. U svemu je, dakle, imao sinova i kćeri trideset i troje.
Hawa ndio wana wa Lea aliomzalia Yakobo huko Padan-Aramu pamoja na binti yake Dina. Jumla ya wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
16 Sinovi Gadovi: Sifjon, Hagi, Šuni, Esbon, Eri, Arodi i Areli.
Wana wa Gadi ni: Sefoni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi na Areli.
17 Sinovi Ašerovi: Jimna, Jišva, Jišvi, Berija i sestra im Serah. Sinovi Berijini: Heber i Malkiel.
Wana wa Asheri ni: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera. Wana wa Beria ni: Heberi na Malkieli.
18 To su bili potomci Zilpe, koju je Laban darovao svojoj kćeri Lei. Ona je tako rodila Jakovu šesnaest duša.
Hawa ndio watoto Zilpa aliomzalia Yakobo, ambao Labani alimpa binti yake Lea; jumla yao walikuwa kumi na sita.
19 Sinovi Jakovljeve žene Rahele: Josip i Benjamin.
Wana wa Raheli mke wa Yakobo ni: Yosefu na Benyamini.
20 Josipu su se u egipatskoj zemlji rodili Manaše i Efrajim. Rodila mu ih je kći onskog svećenika Poti-Fere.
Huko Misri, Asenathi binti wa Potifera, aliyekuwa kuhani wa mji wa Oni, alimzalia Yosefu wana wawili, Manase na Efraimu.
21 Sinovi Benjaminovi: Bela, Beker, Ašbel, Gera, Naaman, Ehi, Roš, Mupim, Hupim i Ard.
Wana wa Benyamini ni: Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu na Ardi.
22 To su bili potomci Rahelini koje je rodila Jakovu - u svemu njih četrnaest.
Hawa ndio wana wa Raheli aliomzalia Yakobo; jumla yao ni kumi na wanne.
23 Danov je sin Hušim.
Mwana wa Dani ni: Hushimu.
24 Sinovi Naftalijevi: Jahseel, Guni, Jeser i Šilem.
Wana wa Naftali ni: Yaseeli, Guni, Yeseri na Shilemu.
25 To su bili potomci Bilhe, koju je Laban dao svojoj kćeri Raheli. Ona je Jakovu rodila sedam potomaka.
Hawa walikuwa wana wa Bilha aliomzalia Yakobo, ambaye Labani alikuwa amempa Raheli binti yake; jumla yao walikuwa saba.
26 Tako je sve Jakovljeve čeljadi što je od njega poteklo i u Egipat doselilo - ne uključujući žena Jakovljevih sinova - u svemu šezdeset i šest osoba.
Wote waliokwenda Misri pamoja na Yakobo, waliokuwa wazao wake hasa pasipo kuhesabu wakwe zake, walikuwa watu sitini na sita.
27 I k tome dva sina Josipova što su mu se rodila u Egiptu. Prema tome, sve čeljadi Jakovljeva doma što se naseli u Egiptu bijaše sedamdeset duša.
Pamoja na wana wawili waliozaliwa na Yosefu huko Misri, jumla yote ya jamaa ya Yakobo, waliokwenda Misri, walikuwa sabini.
28 Izrael posla Judu naprijed k Josipu da se pred njim pojavi u Gošenu. Kad stignu u gošenski kraj,
Basi Yakobo akamtanguliza Yuda aende kwa Yosefu ili amwelekeze njia ya Gosheni. Walipofika nchi ya Gosheni,
29 Josip upregne svoja kola i zaputi se u Gošen - u susret svome ocu Izraelu. Stupivši preda nj, pade mu oko vrata i dugo je tako plakao.
gari kubwa zuri la Yosefu liliandaliwa, naye akaenda Gosheni kumlaki baba yake Israeli. Mara Yosefu alipofika mbele yake, alimkumbatia baba yake, akalia kwa muda mrefu.
30 Onda Izrael reče Josipu: “Sada, pošto sam rođenim očima vidio da si još živ, mogu umrijeti.”
Israeli akamwambia Yosefu, “Sasa niko tayari kufa, kwa kuwa nimejionea mwenyewe kwamba bado uko hai.”
31 Zatim Josip reče svojoj braći i očevoj obitelji: “Otići ću i obavijestiti faraona; reći ću mu: 'Moja braća i obitelj moga oca, koji su bili u zemlji kanaanskoj, došli su k meni.
Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake na watu wa nyumbani mwa baba yake, “Nitapanda kwa Farao na kumwambia, ‘Ndugu zangu na watu wa nyumbani mwa baba yangu, waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, wamekuja kwangu.
32 Oni su ljudi pastiri, uvijek su se bavili stočarstvom; dotjerali su sa sobom svoja stada i sve što im pripada.'
Watu hao ni wachunga mifugo, huchunga mifugo, wamekuja na makundi ya kondoo, mbuzi na ngʼombe pamoja na kila kitu walicho nacho.’
33 Tako, kad vas faraon pozove i zapita: 'Čime se bavite?'
Farao atakapowaita na kuwaulizeni, ‘Kazi yenu ni nini?’
34 odgovorite: 'Ljudi smo, sluge tvoje, koji se od početka do sad bavimo stočarstvom; i mi i naši preci', tako da se možete naseliti u gošenskom kraju. Svi su, naime, pastiri Egipćanima mrski.”
Mjibuni, ‘Watumwa wako wamekuwa wachunga mifugo tangu ujana wetu mpaka sasa, kama baba zetu walivyofanya.’ Ndipo mtakaporuhusiwa kukaa katika nchi ya Gosheni, kwa kuwa wachunga mifugo wote ni chukizo kwa Wamisri.”

< Postanak 46 >