< Postanak 34 >

1 Dina, kći koju je Lea rodila Jakovu, iziđe da posjeti neke žene onoga kraja.
Basi Dina, Binti wa Lea aliyemzalia Yakobo, akaenda kuwaona wasichana wa nchi.
2 Opazi je Hivijac Šekem, sin Hamora, poglavice kraja, pa je pograbi i na silu s njom leže.
Shekemu mwana wa Hamori Mhivi, mwana mfalme wa nchi, akamwona na akamkamata kwa nguvu na kulala naye.
3 Njegovo srce prione za Dinu, Jakovljevu kćer, i on se u djevojku zaljubi. Nastojao je pridobiti djevojčino srce.
Akavutiwa na Dina, binti Yakobo. Akampenda msichana na kuongea naye kwa upole.
4 Šekem je govorio i svom ocu Hamoru: “Onu mi djevojku uzmi za ženu!”
Shekemu akamwambia Hamori baba yeke, kusema, “Nipe msichana huyu kuwa mke wangu.”
5 Jakov sazna da je Šekem obeščastio njegovu kćer Dinu. Ali kako su njegovi sinovi bili uz blago na polju, Jakov nije poduzimao ništa dok oni ne dođu.
Basi Yakobo akasikia kwamba alikuwa amemchafua Dina binti yake. Wanawe walikuwa pamoja na wanyama uwandani, hivyo Yakaobo akawangoja hata walipokuja.
6 Uto dođe k Jakovu Šekemov otac Hamor da se s njim sporazumije,
Hamori baba wa Shekemu akaenda kuongea na Yakobo.
7 upravo kad su se Jakovljevi sinovi vraćali iz polja. Kad su čuli vijest, ljudi su bili ojađeni i vrlo ljuti. Što je Šekem učinio - legavši s Jakovljevom kćeri - u Izraelu je bila sramota. To se nije smjelo trpjeti.
Wana wa Yakobo waliposikia neno hili wakaja kutoka uwandani. Watu hawa walichukizwa sana. Walikasirika sana kwa sababu alikuwa amemwaibisha Israeli kwa kumlazimisha binti wa Yakobo, kwa maana jambo kama hilo halikupasa kutendeka.
8 Hamor im reče. “Moj se sin Šekem svom dušom zaljubio u vašu kćer. Dajte mu je za ženu!
Hamori akaongea nao, akisema, “Shekemu mwanangu anampenda binti yenu. Tafadhari mpeni kuwa mke wake.
9 Oprijateljite se s nama: dajite nam svoje kćeri, a naše kćeri uzimajte sebi!
Mwoane nasi, tupeni binti zenu, na mjichukulie binti zetu kwa ajili yenu wenyewe.
10 Tako možete živjeti među nama; zemlja je pred vama da se naselite, u njoj se slobodno krećete i stječete imovinu!”
Mtaishi nasi, na nchi itakuwa wazi kwa ajili yenu kufanya biashara humo, na kupata mali.”
11 Potom Šekem reče njezinu ocu i njezinoj braći: “Da nađem milost u vašim očima, dat ću vam što zatražite.
Shekemu akamwambia baba yake na ndugu zake, “Na nione kibari machoni penu, na chochote mtakachoniambia nitatoa.
12 Tražite od mene koliko hoćete: sve što god zapitate dat ću, samo mi dajte djevojku za ženu.”
Niambieni kiasi kikubwa chochote cha mahari na zawadi kama mtakavyo, nami nitatoa chochote msemacho, lakini mnipe msichana kuwa mke wangu.”
13 Jakovljevi sinovi odgovore Šekemu i njegovu ocu Hamoru - govorili su s prijevarom jer je obeščastio njihovu sestru Dinu -
Wana wa Yakobo wakamjibu Shekemu na Hamori baba yake kwa hila, kwa sababu Shekemu alikuwa amemnajisi Dina dada yao.
14 te im rekoše: “Ne možemo pristati da svoju sestru damo čovjeku koji nije obrezan, jer bi to za nas bila sramota.
Wakawambia, “Hatuwezi kufanya jambo hili, kumpa dada yetu mtu yeyote ambaye hajatailiwa; kwani hiyo ni aibu kwetu.
15 Jedino ćemo je dati ako postanete kao i mi, ako obrežete sve svoje muškarce.
Kwa sharti hili peke yake tutakubaliana nanyi: iwapo mtatailiwa kama sisi, ikiwa kila mtu mme miongoni mwenu atatailiwa.
16 Onda vam možemo davati svoje kćeri i uzimati vaše sebi, s vama se naseliti i biti jedan rod.
Ndipo tutakapowapa binti zetu, nasi tutachukua binti zenu kwetu sisi wenyewe, na tutaishi nanyi na kuwa wamoja.
17 A ako ne pristajete na obrezanje, uzet ćemo svoju kćer i otići.”
Lakini kama hamtusikilizi na kutailiwa, ndipo tutakapomchukua dada yetu na kuondoka.
18 Hamoru i Šekemu, Hamorovu sinu, njihov se zahtjev učini povoljan.
Maneno yao yakawafurahisha Hamori na Shekemu mwanaye.
19 Mladić nije časio da zahtjev izvrši, jer je čeznuo za Jakovljevom kćeri; a bio je najuvaženiji od svih u očevu domu.
Kijana hakukawia kufanya walichokisema, kwa maana alipendezwa na binti Yakobo, na kwa sababu alikuwa mtu aliyeheshimiwa sana katika nyumba ya babaye.
20 Tako Hamor i njegov sin Šekem dođu u svoje gradsko vijeće i obrate se svojim sugrađanima ovako:
Hamori na Shekemu mwanaye wakaenda katika lango la mji wao na kuongea na watu wa mji, kusema,
21 “Ovaj je svijet prijazan; neka se među nama u zemlji nasele; neka se po njoj slobodno kreću; ima dosta prostora u zemlji za njih; možemo uzimati njihove kćeri sebi za žene, a njima davati svoje.
“Watu hawa wanaamani nasi, hivyo na waishi katika nchi na kufanya biashara humo kwa maana, kweli, nchi ni kubwa ya kuwatosha. Haya na tuwachukue binti zao kuwa wake, nasi tuwape binti zetu.
22 No ljudi će pristati da među nama žive i s nama budu jedan rod samo ako se svi naši muškarci obrežu kao što su oni obrezani.
Kwa shariti hili pekee watu hawa wanakubali kuishi nasi na kuwa wamoja: ikiwa kila mwanamme miongoni mwetu atatailiwa, kama wao.
23 Zar tako ne bi stoka koju su stekli, sve njihovo blago - bilo naše? Pristanimo, pa neka se među nama nasele!”
Je wanyama wao na vitu vyao - wanyama wao wote kuwa wetu? Haya na tukubaliane nao, nao wataishi kati yetu.”
24 Svi odrasli muškarci koji imaju pravo izaći na gradska vrata poslušaše Hamora i njegova sina Šekema, pa bude obrezan svaki muškarac - svaki koji ima pravo izaći na gradska vrata.
Watu wote wa mji wakamsikiliza Hamori na Shekemu, mwanaye. Kila mwanamme akatailiwa.
25 A trećega dana, dok su oni još bili u bolovima, dva Jakovljeva sina, Šimun i Levi, Dinina braća, pograbe svaki svoj mač i nesmetano dođu u grad te poubijaju sve muškarce.
Katika siku ya tatu, walipokuwa katika maumivu bado, wawili wa wana wa Yakobo (Simoni na Lawi, kaka zake Dina), wakachukua kila mmoja upanga wake na kuushambulia mji ambao ulikuwa na uhakika wa ulinzi wake, nao wakauwa wanamme wote.
26 Sasijeku mačem Hamora i njegova sina Šekema, uzmu Dinu iz Šekemove kuće i odu.
Wakamwua Hamori na Shekemu kwa makali ya upanga. Wakamchukua Dina kutoka nyumba ya Shekemu na kuondoka.
27 Ostali Jakovljevi sinovi dođu na ubijene i opustoše grad što je njihova sestra bila obeščašćena.
Wale wana wengine wa Yakobo wakaja kwa maiti na kuuteka nyara mji, kwa sababu watu wale walikuwa wamemnajisi dada yao.
28 Što je bilo krupne i sitne stoke i magaradi, u gradu i u polju, otjeraju;
Wakachukua makundi yao ya kondoo, mbuzi, punda, na kila kitu ndani ya mji na viunga vyake
29 opljačkaju sva njihova dobra, a svu im djecu i žene - sve što je bilo po kućama - odvedu u roblje.
utajiri wote. Watoto na wake zao wote, wakawachukua. Hata wakachukua kila kitu kilichokua katika nyumba.
30 Jakov reče Šimunu i Leviju: “Uveli ste me u nepriliku omrazivši me stanovnicima zemlje, Kanaancima i Perižanima. Ako se ujedine protiv mene i napadnu me, dok je nas ovako malo na broj, istrijebit će me s mojim domom.”
Yakobo akawambia Simoni na Lawi, “Mmeleta shida juu yangu, kunifanya ninuke kwa wenyeji wa nchi, Wakanaani na Waperizi. Mimi nina watu wachache. Ikiwa watajikusanya pamoja kinyume changu na kunishambulia.”
31 Oni odgovore: “Zar da prema našoj sestri postupaju kao prema kakvoj bludnici?”
Lakini Simoni na Lawi wakasema, “Je Shekemu alipaswa kumtendea dada yetu kama kahaba?”

< Postanak 34 >