< Postanak 30 >

1 Vidjevši Rahela da Jakovu ne rađa djece, postade zavidna svojoj sestri pa reče Jakovu: “Daj mi djecu! Inače ću svisnuti!”
Raheli alipoona kwamba hamzalii Yakobo watoto, Raheli akamwonea wivu dada yake. Akamwambia Yakobo, “Nipe watoto, sivyo nitakufa.”
2 Jakov se razljuti na Rahelu te reče. “Zar sam ja namjesto Boga koji ti je uskratio plod utrobe?”
Hasira ya Yakobo ikawaka juu ya Raheli. Akasema, “Mimi ni badala ya Mungu, aliyekuzuilia usipate watoto?
3 A ona odgovori: “Evo moje sluškinje Bilhe: uđi k njoj, pa neka rodi na mojim koljenima, da tako i ja steknem djecu po njoj.”
Akasema, “Tazama, kuna mjakazi wangu Bilha. Lala naye, hivyo aweze kuzaa watoto magotini pangu, nami nitapata watoto kwake.
4 Dade mu dakle svoju sluškinju Bilhu za ženu, i Jakov priđe k njoj.
Hivyo akampa Bilha mjakazi kama mke wake, na Yakobo akalala naye.
5 Bilha zače te Jakovu rodi sina.
Bilha akashika mimba na kumzalia Yakobo mwana.
6 Tada Rahela reče: “Jahve mi je dosudio pravo. Uslišao je moj glas i dao mi sina.” Stoga mu nadjenu ime Dan.
Kisha Raheli akasema, “Mungu ameamua kwa faida yangu. Ameyasikiliza maombi yangu na kunipa mwana.” Kwa sababu hiyo akamwita jina lake Dani
7 Rahelina sluškinja Bilha opet zače i rodi Jakovu drugoga sina.
Bilha, mjakazi wa Raheli, akashika mimba tena na kumzalia Yakobo mwana wa pili.
8 Tada Rahela reče: “Žestoko sam se borila sa sestrom, ali sam pobijedila.” Tako mu nadjenu ime Naftali.
Raheli akasema, “Kwa mashindano yenye nguvu nimeshindana na dada yangu na kushinda.” Akamwita jina lake Naftali.
9 A vidjevši Lea da je prestala rađati, uzme svoju sluškinju Zilpu pa je dade Jakovu za ženu.
Lea alipoona kwamba ameacha kuzaa, akamchukua Zilpa, mjakazi wake, na kumpa Yakobo kama mke wake.
10 I kad je Leina sluškinja Zilpa rodila Jakovu sina,
Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana.
11 Lea uskliknu: “Koje sreće!” Tako mu nadjenu ime Gad.
Lea akasema, “Hii ni bahati njema!” Hivyo akamwita jina lake Gadi.
12 Leina sluškinja Zilpa rodi Jakovu i drugog sina,
Kisha Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana wa pili.
13 i Lea opet uskliknu: “Blago meni! Žene će me zvati blaženom!” Tako mu nadjenu ime Ašer.
Lea akasema, “Nina furaha! Kwa maana mabinti wataniita furaha.” Hivyo akamwita jina lake Asheri.
14 Jednoga dana, u vrijeme pšenične žetve, namjeri se Ruben u polju na ljubavčice te ih donese svojoj majci Lei. I Rahela reče Lei: “Daj mi od ljubavčica svoga sina!”
Siku za mavuno ya ngano Rubeni akaenda shambani na kuona tunguja. Akazileta kwa mama yake. Kisha Raheli akamwambia Lea, “Nipe baadhi ya tunguja za mwanao.”
15 A Lea odgovori: “Zar ti nije dosta što si mi oduzela muža pa još hoćeš da od mene uzmeš i ljubavčice moga sina?” Rahela odgovori: “Pa dobro, neka s tobom noćas leži u zamjenu za ljubavčice tvog sina.”
Lea akamwambia, “Je ni jambo dogo kwako, kumchukua mme wangu? Je na sasa unataka kuchukua tunguja za mwanangu pia? Raheli akasema, “Kisha atalala nawe leo usiku, kwa kubadilishana na tunguja za mwanao.
16 Kad je Jakov navečer stigao iz polja, Lea mu iziđe u susret pa reče: “Treba da dođeš k meni, jer sam te unajmila za ljubavčice moga sina.” One je noći on s njom ležao.
Jioni Yakobo akaja kutoka uwandani. Lea akaenda kumlaki na kusema, “Leo usiku utalala nami, kwani nimekuajiri kwa tunguja za mwanangu.” Hivyo Yakobo akalala na Lea usiku huo.
17 Bog usliša Leu; ona zače te Jakovu rodi petog sina.
Mungu akamsikia Lea, na akashika mimba na kumzalia Yakobo mwana wa tano.
18 Onda Lea reče: “Bog mi je uzvratio nagradom što sam ustupila svoju sluškinju svome mužu.” Stoga sinu nadjenu ime Jisakar.
Lea akasema, “Mungu amenipa ujira wangu, kwa sababu nilimpa mme wangu mjakazi wangu.” Akamwita jina lake Isakari.
19 Lea opet zače i rodi Jakovu šestoga sina.
Lea akashika mimba tena na kuzaa mwana wa tano kwa Yakobo.
20 Onda Lea reče: “Bog me obdari dragocjenim darom; sada će mi moj muž dati darove: tÓa rodila sam mu šest sinova.” Tako mu nadjenu ime Zebulun.
Lea akasema, “Mungu amenipa zawadi njema. Sasa mme wangu ataniheshimu, kwa sababu nimemzalia wana sita.” Akamwita jina lake Zabuloni.
21 Zatim rodi kćer te joj nadjenu ime Dina.
Baadaye akazaa binti na kumwita jina lake Dina.
22 Uto se Bog sjeti Rahele: Bog je usliša i otvori njezinu utrobu.
Mungu akamkumbuka Raheli na kumsikiliza. Akampa kushika mimba.
23 Ona zače i rodi sina te reče: “Ukloni Bog moju sramotu!”
Akashika mimba na kuzaa mwana. Akasema, “Mungu ameiondoa aibu yangu.”
24 Nadjene mu ime Josip, rekavši: “Neka mi Jahve pridoda drugog sina!”
Akamwita jina lake Yusufu, akisema, Yahwe ameniongeza mwana mwingine.”
25 Pošto je Rahela rodila Josipa, Jakov reče Labanu: “Pusti me da idem u svoj zavičaj!
Baada ya Raheli kumzaa Yusufu, Yakobo akamwambia Labani, “Niache niande, ili kwamba niende nyumbani kwetu na katika nchi yangu.
26 Daj mi moje žene za koje sam te služio i moju djecu da mogu otići: tÓa dobro znaš kako sam te služio.”
Nipe wake zangu na watoto wangu niliokutumikia kwa ajili yao, na uniache niondoke, kwani unafahamu nilivyokutumikia.
27 A Laban mu odgovori: “Ne idi, ako si mi prijatelj. Znam da me Jahve blagoslivljao zbog tebe.”
Labani akamwambia, “Ikiwa nimepata kibali machoni pako, subiri, kwa sababu nimejifunza kwa kutumia uaguzi kwamba Yahwe amenibariki kwa ajili yako.”
28 I nadoda: “Odredi plaću koju želiš od mene, i dat ću ti.”
Kisha akasema, “Taja ujira wako, nami nitalipa.”
29 On mu odgovori: “Ti dobro znaš što je moja služba značila za te i kako je tvome blagu bilo sa mnom.
Yakobo akamwambia, “Unajua nilivyokutumikia, na jinsi ambavyo mifugo wako wamekuwa nami.
30 Malenkost što si je imao prije nego sam ja došao povećala se vrlo mnogo, jer kuda god sam prolazio Jahve te blagoslivljao na mojim koracima. A sad je vrijeme da poradim i za svoj dom.”
Kwani walikuwa wachache kabla sijaja, na wameongezeka kwa wingi. Popote nilipokutumikia Mungu amekubariki. Je ni lini mimi nitaandaa kwa ajili ya nyumba yangu pia?”
31 On upita: “Koliko da ti platim?” Jakov odgovori: “Nemoj mi platiti ništa! Ako mi učiniš ovo, opet ću na pašu goniti i čuvati tvoje stado.
Hivyo Labani akasema, “Je nikulipe nini? Yakobo akasema, 'Usinipe chochote. Ikiwa utafanya jambo hili kwa ajili yangu, nitawalisha tena kondoo wako na kuwatunza.
32 Daj da prođem danas kroz tvoje stado i od njega izlučim svaku garavu ovcu i svaku šarenu ili napruganu kozu! Neka to bude moja plaća!
Niache nipite kati ya kundi lako lote leo, kwa kuondoa kila kondoo mwenye milia na mabaka, na kila kondoo mweusi kati yao, na kati ya wenye mabaka na milia katika mbuzi. Hawa watakuwa ujira wangu.
33 A ubuduće kad budeš svojim očima provjeravao moju naplatu, moje će poštenje biti svjedok za mene: nađe li se među mojim kozama ijedna koja ne bude šarena ili naprugana, ili među ovcama koja ne bi bila garava, neka se smatra ukradenom!”
Uadilifu wangu utashuhudia kwa ajili yangu hapo baadaye, utakapokuja kuangalia ujira wangu. Kila ambaye hana milia na hana madoa miongoni mwa mbuzi, na mweusi kati ya kondoo, ikiwa wataonekana kwangu, watahesabiwa kuwa wameibwa.”
34 Laban reče: “Dobro, neka bude kako si kazao.”
Labani akasema, “Nakubali. Na iwe kama yalivyo maneno yako.”
35 Ali toga dana Laban izluči naprugane i šarene jarce i sve riđaste i šarene koze - svaku koja je na sebi imala bijelo - i sve garave ovce pa ih preda svojim sinovima.
Siku hiyo Labani akaondoa mabeberu yaliyokuwa na milia na madoa, na majike ya mbuzi yaliyokuwa na milia na madoa, kila aliyekuwa mweupe, na weusi wote katika mbuzi, akawakabidhi katika mikono ya wanaye.
36 I odande gdje je Jakov pasao ostatak Labanova stada udalji se za koja tri dana hoda.
Pia Labani akaweka safari ya siku tatu kati yake na Yakobo. Hivyo Yakobo akabaki kuchunga wale kondoo wa Labani waliosalia.
37 A Jakov uzme zelenih mladica od topola, badema i platana; na njima izreza bijele pruge, otkrivši bjeliku na mladicama.
Yakobo akachukua matawi mabichi yaliyokatwa ya mipopla, mlozi na mwaramoni mbichi akatoa maganda ili michilizi myeupe ionekane, na akaifanya sehemu nyeupe ya ndani ya mti iliyokuwa ndani ya fito ionekane.
38 Pruće tako isprugano postavi u korita, u pojila iz kojih se stoka napajala. A kako se stoka parila kad je na vodu dolazila,
Kisha akaziweka fito alizokuwa amezibambua mbele ya makundi ya kondoo, mbele ya mabirika yakunyweshea walipokuja kunywa maji. Wakashika mimba walipokuja kunywa maji.
39 to su se jarci parili uz pruće, pa su koze kozile prugaste, riđaste i šarene kozliće.
Wanyama wakapandana mbele ya fito; nao wakazaa watoto wenye milia, mabaka na wenye madoa.
40 Tako je i ovce Jakov bio izlučio i glave im okrenuo prema prugastima ili posve garavima što su bile u Labanovu stadu. Tako je za se namicao posebna stada koja nije miješao s Labanovim stadima.
Yakobo akawatenga hawa wanakondoo, lakini akawafanya waliosalia kuelekea wanyama wenye milia na kondoo weusi wote katika kundi la Labani. Kisha akayatenga makundi yake mwenyewe pekee na hakuwaweka pamoja na wale wa Labani.
41 Osim toga, kad bi se god dobro uzrasla stoka parila, Jakov bi stavio pruće u korita, baš pred oči živine, tako da se pari pred prućem.
Pindi kondoo wenye nguvu katika kundi walipopandana, Yakobo alilaza fito katika mabirika ya maji mbele ya macho ya kundi, ili kwamba washike mimba kati ya fito.
42 Ali ga pred kržljavu marvu nije stavljao. Tako je kržljava zapadala Labana, a dobro razvijena Jakova.
Lakini wakati waliodhaifu walipokuja, hakuweka fito mbele yao. Hivyo wanyama dhaifu wakawa wa Labani, na wenye nguvu wakawa wa Yakobo.
43 Čovjek se tako silno obogatio, stekao mnogu stoku, sluge i sluškinje, deve i magarad.
Mtu huyo akastawi sana. Akawa na kundi kubwa la kondoo, wajakazi na wajoli, ngamia na punda.

< Postanak 30 >