< Galačanima 3 >
1 O bezumni Galaćani, tko li vas opčara? A pred očima vam je Isus Krist bio ocrtan kao Raspeti.
Ninyi Wagalatia wajinga! Ni nani aliyewaroga? Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele yenu kwamba amesulubiwa.
2 Ovo bih samo htio doznati od vas: jeste li primili Duha po djelima Zakona ili po vjeri u Poruku?
Nataka nijifunze neno moja kutoka kwenu: Je, mlipokea Roho wa Mungu kwa kushika sheria, au kwa kuyaamini yale mliyosikia?
3 Tako li ste bezumni? Započeli ste u Duhu pa da sada u tijelu dovršite?
Je, ninyi ni wajinga kiasi hicho? Baada ya kuanza kwa Roho, je, sasa mwataka kumalizia katika mwili?
4 Zar ste toliko toga uzalud doživjeli? A kad bi doista bilo uzalud!
Je, mlipata mateso kiasi hicho bure? Ni kama kweli yalikuwa bure!
5 Onaj dakle koji vam daje Duha i čini među vama silna djela, čini li to zbog djela Zakona ili zbog vjere u Poruku?
Je, Mungu huwapa Roho wake na kufanya miujiza katikati yenu kwa sababu mnatii sheria, au kwa sababu mnaamini kile mlichosikia?
6 Tako Abraham povjerova Bogu i uračuna mu se u pravednost.
Kama vile “Abrahamu alimwamini Mungu na ikahesabiwa kwake kuwa haki.”
7 Shvatite dakle: oni od vjere, to su sinovi Abrahamovi.
Fahamuni basi kwamba wale walio na imani, hao ndio watoto wa Abrahamu.
8 A Pismo, predvidjevši da Bog po vjeri opravdava pogane, unaprijed navijesti Abrahamu: U tebi će blagoslovljeni biti svi narodi.
Maandiko yakitabiri kwamba Mungu angewahesabia haki watu wa Mataifa kwa imani, alitangulia kumtangazia Abrahamu Injili akisema kwamba, “Kwa kupitia kwako mataifa yote yatabarikiwa.”
9 Tako: oni od vjere blagoslivlju se s vjernikom Abrahamom.
Kwa sababu hii, wale wote wanaoamini wanabarikiwa pamoja na Abrahamu, mtu wa imani.
10 Doista, koji su god od djela Zakona, pod prokletstvom su. Ta pisano je: Proklet tko se god ne drži i tko ne vrši svega što je napisano u Knjizi Zakona.
Kwa maana wote wanaotumainia matendo ya sheria wako chini ya laana, kwa kuwa imeandikwa, “Alaaniwe kila mtu asiyeshikilia kutii mambo yote yaliyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.”
11 A da se pred Bogom nitko ne opravdava Zakonom, očito je jer: Pravednik će od vjere živjeti.
Basi ni dhahiri kwamba hakuna mtu anayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa kushikilia sheria, kwa maana, “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
12 Zakon pak nije od vjere, nego veli: Tko ga vrši, u njemu će naći život.
Lakini sheria haitegemei imani. Kinyume chake, “Mtu atendaye matendo hayo ataishi kwa hayo.”
13 Krist nas otkupi od prokletstva Zakona, postavši za nas prokletstvom - jer pisano je: Proklet je tko god visi na drvetu -
Kristo alitukomboa kutoka laana ya sheria kwa kufanyika laana kwa ajili yetu, kwa maana imeandikwa, “Amelaaniwa yeye aangikwaye juu ya mti.”
14 da u Kristu Isusu na pogane dođe blagoslov Abrahamov: da Obećanje, Duha, primimo po vjeri.
Alitukomboa ili kwamba baraka aliyopewa Abrahamu ipate kuwafikia watu wa Mataifa kwa njia ya Kristo Yesu, ili kwa imani tupate kupokea ile ahadi ya Roho.
15 Braćo, po ljudsku govorim: već i ljudski valjan savez nitko ne poništava niti mu što dodaje.
Ndugu zangu, nataka nitoe mfano kutoka maisha ya kila siku. Kama vile hakuna mtu awezaye kutangua au kuongeza kitu katika agano la mtu ambalo limekwisha kuthibitishwa, vivyo hivyo kwa hali kama hii.
16 A ova su obećanja dana Abrahamu i potomstvu njegovu. Ne veli se: “i potomcima” kao o mnogima, nego kao o jednomu: I potomstvu tvojem, to jest Kristu.
Ahadi zilinenwa kwa Abrahamu na kwa mzao wake. Maandiko hayasemi “kwa wazao,” likimaanisha watu wengi, bali “kwa mzao wako,” yaani mtu mmoja, ndiye Kristo.
17 Ovo hoću kazati: Saveza koji je Bog valjano sklopio ne obeskrepljuje Zakon, koji je nastao četiri stotine i trideset godina poslije, i ne dokida obećanja.
Ninachotaka kusema ni kwamba, sheria, ambayo ilitolewa miaka 430 baadaye, haitangui Agano lililothibitishwa na Mungu ili kuibatilisha ahadi ile.
18 Doista, ako se baština zadobiva po Zakonu, ne zadobiva se po obećanju. A Abrahama je Bog po obećanju obdario.
Kwa maana kama urithi hupatikana kwa sheria, basi hautegemei tena ahadi, lakini Mungu kwa neema yake alimpa Abrahamu urithi kwa njia ya ahadi.
19 Čemu onda Zakon? Dometnut je poradi prekršaja dok ne dođe potomstvo komu je namijenjeno obećanje; sastavljen je po anđelima preko posrednika.
Kwa nini basi iwepo sheria? Sheria iliwekwa kwa sababu ya makosa mpaka atakapokuja yule Mzao wa Abrahamu, ambaye alitajwa katika ile ahadi. Sheria iliamriwa na malaika kwa mkono wa mpatanishi.
20 Posrednika pak nema gdje je samo jedan. A Bog je jedan.
Basi mpatanishi huhusisha zaidi ya upande mmoja, lakini Mungu ni mmoja.
21 Zar je dakle Zakon protiv obećanja Božjih? Nipošto! Jer da je dan Zakon koji bi mogao oživljavati, pravednost bi doista proizlazila iz Zakona.
Je basi, sheria inapingana na ahadi za Mungu? La hasha! Kwa maana kama sheria iliyotolewa ingeweza kuwapa watu uzima, basi haki ingepatikana kwa njia ya sheria.
22 Ali je Pismo sve zatvorilo pod grijeh da se, po vjeri u Isusa Krista, obećano dade onima koji vjeruju.
Lakini Maandiko yamefanya vitu vyote vifungwe chini ya nguvu ya dhambi, ili yale yaliyoahidiwa kwa njia ya imani katika Yesu Kristo yapate kupewa wale wanaoamini.
23 Prije dolaska vjere, pod Zakonom zatvoreni, bili smo čuvani za vjeru koja se imala objaviti.
Kabla imani hii haijaja tulikuwa tumewekwa chini ya sheria, tumefungwa mpaka ile imani ifunuliwe.
24 Tako nam je Zakon bio nadzirateljem sve do Krista da se po vjeri opravdamo.
Hivyo, sheria ilikuwa kiongozi kutufikisha kwa Kristo, ili tupate kuhesabiwa haki kwa imani.
25 A otkako je nadošla vjera, nismo više pod nadzirateljem.
Lakini sasa kwa kuwa ile imani imekuja, hatusimamiwi tena na sheria.
26 Uistinu, svi ste sinovi Božji, po vjeri u Kristu Isusu.
Kwa maana ninyi nyote mmekuwa watoto wa Mungu katika Kristo Yesu kwa njia ya imani.
27 Doista, koji ste god u Krista kršteni, Kristom se zaodjenuste.
Kwa maana wote mliobatizwa ndani ya Kristo, mmemvaa Kristo.
28 Nema više: Židov - Grk! Nema više: rob - slobodnjak! Nema više: muško - žensko! Svi ste vi Jedan u Kristu Isusu!
Wala hakuna tena Myahudi au Myunani, mtumwa au mtu huru, mwanaume wala mwanamke, maana nyote mmekuwa wamoja ndani ya Kristo Yesu.
29 Ako li ste Kristovi, onda ste Abrahamovo potomstvo, baštinici po obećanju.
Nanyi mkiwa ni mali ya Kristo, basi ninyi ni wa uzao wa Abrahamu na warithi sawasawa na ile ahadi.