< Ezra 4 >

1 Ali kada su čuli Judini i Benjaminovi neprijatelji da povratnici iz sužanjstva grade svetište Jahvi, Bogu Izraelovu,
Adui za Yuda na Benyamini waliposikia kwamba watu waliorudi kutoka uhamishoni wanajenga Hekalu kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli,
2 potražiše Zerubabela, Ješuu i glavare obiteljske i rekoše im: “Mi želimo s vama graditi, jer, kao i vi, tražimo Boga vašega i njemu prinosimo žrtve od vremena Esar Hadona, asirskoga kralja, koji nas je ovamo doveo.”
wakamjia Zerubabeli na viongozi wa jamaa, nao wakasema, “Turuhusuni tuwasaidie kujenga, kwa sababu sisi tunamtafuta Mungu wenu kama ninyi na tumekuwa tukimtolea dhabihu tangu wakati wa Esar-Hadoni mfalme wa Ashuru, aliyetuleta hapa.”
3 Zerubabel, Ješua i glavari izraelskih obitelji odgovoriše im: “Nije na vama da s nama gradite Dom našemu Bogu: gradit ćemo mi sami Jahvi, Bogu Izraelovu, kako nam je naredio Kir, kralj perzijski.”
Lakini Zerubabeli, Yeshua na viongozi wengine wa jamaa ya Israeli wakawajibu, “Ninyi hamna sehemu nasi katika kujenga Hekalu la Mungu wetu. Sisi peke yetu tutajenga Hekalu kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli, kama Mfalme Koreshi, mfalme wa Uajemi alivyotuagiza.”
4 Tada je narod one zemlje plašio ljude Judeje i smetao im u gradnji.
Ndipo watu waliowazunguka wakajipanga kuwakatisha tamaa watu wa Yuda na kuwafanya waogope walipokuwa wakiendelea na ujenzi.
5 Podmitili su savjetnike da im ometaju naum: tako je bilo za vrijeme perzijskoga kralja Kira sve do perzijskoga kralja Darija. Samarijanske smetnje za Kserksove i Artakserksove vladavine
Wakaajiri washauri kuwapinga katika kazi yao, nao wakaipinga mipango yao wakati wote wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi hadi wakati wa utawala wa Dario mfalme wa Uajemi.
6 Za Kserksova kraljevanja, na početku njegove vladavine, sastaviše tužbu protiv stanovnika Judeje i Jeruzalema.
Mnamo mwanzo wa utawala wa Ahasuero, hao adui waliandika mashtaka dhidi ya watu wa Yuda na Yerusalemu.
7 I za vremena Artakserksova pisali su Bišlam, Mitredat, Tabel i ostali njihovi drugovi protiv Jeruzalema perzijskom kralju Artakserksu. Podnesak je bio pisan aramejskim pismom i jezikom.
Pia katika siku za utawala wa Artashasta mfalme wa Uajemi, Bishlamu, Mithredathi, Tabeeli pamoja na wenzao waliandika barua kwa Artashasta. Barua hiyo iliandikwa kwa mwandiko wa Kiaramu na katika lugha ya Kiaramu.
8 Zatim su upravitelj Rehum i tajnik Šimšaj napisali kralju Artakserksu slijedeće pismo protiv Jeruzalema -
Rehumu afisa msimamizi na mwandishi Shimshai waliandika barua kwa Mfalme Artashasta dhidi ya watu wa Yerusalemu kama ifuatavyo:
9 upravitelj Rehum, tajnik Šimšaj i ostali drugovi njihovi: perzijski suci, poslanici, činovnici; Arkevajci, Babilonci, Suzanci - to jest Elamci -
Rehumu afisa msimamizi na mwandishi Shimshai, pamoja na wenzao, yaani mahakimu na maafisa walio juu ya watu kuanzia Tripoli, Uajemi, Ereki na Babeli, Waelami wa Shushani,
10 i ostali narodi koje je veliki i slavni Asurbanipal bio odveo u sužanjstvo i naselio ih u gradove Samarije i druge krajeve s onu stranu Rijeke.
na watu wengine ambao mheshimiwa Asur-Banipali aliwahamisha na kuwakalisha katika mji wa Samaria na mahali pengine Ngʼambo ya Mto Frati.
11 Evo prijepisa pisma koje su mu poslali: “Kralju Artakserksu, tvoje sluge, ljudi s onu stranu Rijeke. Sada, dakle,
(Hii ndiyo nakala ya barua waliyompelekea.) Kwa Mfalme Artashasta, Kutoka kwa watumishi wako, watu wa Ngʼambo ya Mto Frati:
12 neka zna kralj da su Judejci stigli k nama od tebe; došavši u Jeruzalem, žele ponovo sagraditi odmetnički i opaki grad; podižu zidine, a temelje su već postavili.
Yapasa Mfalme ajue kuwa Wayahudi waliopanda kuja kwetu kutoka kwenu, wamekwenda Yerusalemu nao wanaujenga upya ule mji wa uasi na uovu. Wanajenga kuta upya na kukarabati misingi yake.
13 Neka zna kralj: ako ovaj grad bude sagrađen i zidovi podignuti, neće se više plaćati porez, ni danak, ni carina, i ovaj će grad biti na štetu kraljevske riznice.
Zaidi ya hayo, mfalme yampasa ajue kwamba kama mji huu ukijengwa na kuta zake zikafanywa upya, hakutakuwa na ulipaji wa kodi wala ada au ushuru, hivyo hazina za mfalme zitaathirika.
14 Budući da jedemo dvorsku sol, ne čini nam se doličnim gledati ovu sramotu nanesenu kralju. Zato, dakle, obavještavamo kralja:
Sisi sasa kwa kuwa tunawajibika kwa jumba la kifalme na kwamba siyo sawasawa kwetu kuona mfalme akidharauliwa, basi tunatuma ujumbe huu kumtaarifu mfalme,
15 neka se poduzmu istraživanja u ljetopisima tvojih očeva: u tim ćeš ljetopisima naći i utvrditi da je ovaj grad odmetnički grad, nesretan za kraljeve i pokrajine i da su se u njemu od davnine dizale bune. Zato je ovaj grad bio razoren.
ili kwamba ufanyike uchunguzi kwenye kumbukumbu ya maandishi ya waliokutangulia. Katika kumbukumbu hizi utagundua kwamba mji huu ni wa maasi, unaowataabisha wafalme na majimbo, ni mahali pa maasi tangu zamani. Ndiyo maana mji huu uliharibiwa.
16 Obavješćujemo kralja da neće biti više tvoje područje preko Rijeke ako ovaj grad bude ponovo sagrađen i zidovi podignuti!”
Tunamjulisha mfalme kwamba kama mji huu ukijengwa na kuta zake zikifanywa upya, hutabakiwa na chochote Ngʼambo ya Mto Frati.
17 Kralj je poslao ovaj odgovor: “Rehumu, upravitelju, Šimšaju, tajniku, i ostalim drugovima njihovim koji borave u Samariji i drugdje, s onu stranu Rijeke - mir! Evo,
Mfalme alirudisha jibu hili: Kwa Rehumu, afisa msimamizi, mwandishi Shimshai na wenzenu wote wanaoishi katika Samaria na penginepo Ngʼambo ya Mto Frati: Salamu.
18 podnesak koji ste mi poslali bio je preda mnom pričitan u njegovu prijevodu.
Barua mliyotutumia imesomwa na kutafsiriwa mbele yangu.
19 Po mojoj su naredbi poduzeli istraživanja i utvrdili da se taj grad dizao od davnine protiv kraljeva i da su u njemu bivali ustanci i bune.
Nilitoa amri na uchunguzi ukafanyika na imegundulika kwamba mji huu una historia ndefu ya maasi dhidi ya wafalme na pamekuwa mahali pa maasi na uchochezi.
20 I moćni su kraljevi kraljevali u Jeruzalemu, koji su gospodarili svime s onu stranu Rijeke: njima se plaćao danak, porez i carina.
Yerusalemu umepata kuwa na wafalme wenye nguvu wakitawala nchi yote iliyo Ngʼambo ya Mto Frati, wakitoza kodi, ada na ushuru huko.
21 Zapovjedite, dakle, da se prekine pothvat onih ljudi: taj se grad neće zidati dok ja o tome ne odlučim.
Kwa hiyo toeni amri kwa watu hawa wasimamishe ujenzi, ili kwamba mji huu usiendelee kujengwa hadi nitakapoagiza.
22 Čuvajte se svakog propusta u postupku, da ne bi zlo poraslo na štetu kraljeva.”
Mwe waangalifu msipuuze jambo hili. Kwa nini kuruhusu tishio hili kuendelea na kusababisha hasara kwa ufalme?
23 Pošto je prijepis otpisa kralja Artakserksa pročitan pred Rehumom, upraviteljem, Šimšajem, tajnikom, i pred njihovim drugovima, oni brzo odoše u Jeruzalem k Judejcima te im oružanom snagom zabraniše radove.
Mara waliposomewa nakala ya barua ya Mfalme Artashasta, Rehumu na Shimshai aliyekuwa mwandishi na wenzao, walikwenda mara moja kwa Wayahudi huko Yerusalemu na kuwalazimisha kwa nguvu kusimamisha ujenzi.
24 Tako su obustavljeni poslovi oko gradnje Doma Božjega u Jeruzalemu. Bili su prekinuti sve do druge godine kraljevanja Darija, perzijskoga kralja.
Hivyo kazi ya ujenzi wa nyumba ya Mungu huko Yerusalemu ikasimamishwa kabisa hadi mwaka wa pili wa utawala wa Dario mfalme wa Uajemi.

< Ezra 4 >