< Ezekiel 40 >

1 Godine dvadeset i pete za našega izgnanstva, početkom godine, prvoga mjeseca, desetoga dana, a četrnaest godina otkako pade Grad, upravo onoga dana spusti se na me ruka Jahvina.
Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
2 I odvede me u božanskom viđenju u zemlju Izraelovu te me postavi na veoma visoku goru: Na njoj, s južne strane, bijaše nešto kao sazidan grad.
Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
3 Povede me onamo, i gle: čovjek, sjajan kao mjed, stajaše na vratima, s lanenim užetom i mjeračkom trskom u ruci.
Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
4 I taj mi čovjek reče: “Sine čovječji, gledaj svojim očima i slušaj svojim ušima, popamti sve što ću ti pokazati, jer si doveden ovamo da ti pokažem. Objavi domu Izraelovu sve što ovdje vidiš.”
Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
5 I gle, zdanje sve uokolo opasano zidom. Čovjek držaše u ruci mjeračku trsku od šest lakata, a svaki lakat bijaše za jedan dlan duži od običnoga lakta. On izmjeri zdanje. Širina: jedna trska, visina: jedna trska.
Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
6 Zatim pođe k vratima što bijahu okrenuta k istoku. Uspe se uza stepenice i izmjeri prag vrata. Širina: jedna trska.
Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
7 A svaka klijet jednu trsku dugačka i jednu trsku široka. Između klijeti: pet lakata. Prag vrata sa strane njihova trijema, iznutra, jedna trska.
Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
8 Izmjeri trijem vrata iznutra: bijaše osam lakata širok,
Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
9 a njegovi polustupovi dva lakta. Trijem vrata bijaše s nutarnje strane.
ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
10 Na svakoj strani istočnih vrata bijahu po tri klijeti. I sve tri bijahu iste mjere. Tako i polustupovi: s obje strane bijahu iste mjere.
Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
11 Zatim izmjeri vrata: bijahu deset lakata široka i trinaest lakata visoka.
Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
12 Pred klijetima bijaše s jedne i s druge strane ograda od jednog lakta. Svaka klijet: šest lakata s jedne i šest lakata s druge strane.
Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
13 A zatim izmjeri vrata od stražnje strane jedne klijeti do stražnje strane nasuprotne klijeti, u širinu: bijaše dvadeset i pet lakata; otvor pred otvorom.
Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
14 Izmjeri i trijem: dvadeset lakata. Predvorje bijaše sve uokolo trijema vrata.
Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
15 Od ulaznog pročelja vrata do nasuprotne strane njihova trijema bijaše pedeset lakata.
Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
16 Na klijetima i njihovim dovracima, s unutrašnje strane sve uokolo, a tako i u trijemu, bijahu prozori s rešetkama. Takvi su prozori bili iznutra, sve naokolo, a na polustupovima palme.
Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
17 Zatim me povede u vanjsko predvorje Doma. I gle, sve oko predvorja prostorije i pločnik. Trideset prostorija na pločniku.
Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
18 Pločnik bijaše sa svake strane vrata i odgovaraše razini vrata. To je donji pločnik.
Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
19 On izmjeri širinu predvorja od donjih vrata do unutrašnjega predvorja, s vanjske strane: sto lakata na istok i na sjever.
Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
20 Sjevernim vratima vanjskoga predvorja izmjeri širinu i dužinu.
Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
21 I ta su imala po tri klijeti sa svake strane, a stupovi im i trijemovi istih mjera kao u prvih vrata: pedeset lakata u dužinu i dvadeset i pet lakata u širinu.
Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
22 Prozori im, trijemovi i palme bijahu iste mjere kao na istočnim vratima, a na prilazu im sedam stepenica; trijem im bijaše s unutrašnje strane.
Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
23 Unutrašnje predvorje imaše vrata što bijahu nasuprot sjevernim vratima; kao i istočna. On izmjeri: između jednih i drugih vrata bijaše sto lakata.
Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
24 Zatim me povede na jug, i gle: i ondje vrata. Izmjeri ondje klijeti, polustupove i trijemove: bijahu iste mjere.
Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
25 Ona, kao i njihovi trijemovi, imahu sve uokolo prozore što bijahu kao i oni prvi. Dužina je i tu iznosila pedeset lakata, a širina dvadeset i pet.
Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
26 K vratima je vodilo sedam stuba; trijem im je bio s unutrašnje strane, a na stupovima imahu po jednu palmu sa svake strane.
Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
27 Unutrašnje predvorje imaše jedna vrata i s južne strane. On izmjeri: od tih vrata do južnih vrata - sto lakata.
Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
28 Zatim me na južna vrata uvede u unutrašnje predvorje. I izmjeri južna vrata: bijahu istih mjera.
Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
29 Klijeti, stupovi i trijemovi bijahu istih mjera. Vrata i njihov trijem imahu svud unaokolo prozore. Pedeset lakata bijaše tu u dužinu, dvadeset i pet lakata u širinu.
Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
30 A sve uokolo trijemovi: dvadeset i pet lakata dugi, a pet lakata široki.
(Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
31 Trijemovi su se pružili prema vanjskom predvorju. Na polustupovima njihovim palme, a stubište im je imalo osam stuba.
Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
32 Zatim me povede k istočnim vratima unutrašnjega predvorja. I izmjeri vrata: bijahu istih mjera.
Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
33 Klijeti im, polustupovi i trijemovi bijahu također istih mjera. Vrata i njihov trijem imahu svud naokolo prozore. U dužinu bješe pedeset lakata, u širinu dvadeset i pet.
Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
34 Trijem im se pružao prema vanjskom predvorju. Na njihovim polustupovima s ove i s one strane bijahu palme. Stubište im imaše osam stuba.
Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
35 Zatim me povede k sjevernim vratima. I izmjeri ih: bijahu istih mjera.
Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
36 Klijeti im, polustupovi i trijemovi bijahu također istih mjera. Vrata i njihov trijem imahu svud uokolo prozore. Pedeset je lakata tu bilo u dužinu, a dvadeset i pet u širinu.
kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
37 Trijem je sezao do vanjskoga predvorja. Na polustupovima s ove i one strane bijahu palme. Stubište imaše osam stuba.
Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
38 Uz trijemove vrata bijaše prostor s posebnim ulazom. Ondje su se ispirale žrtve paljenice.
Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
39 U trijemu vrata s jedne i s druge strane bijahu po dva stola za klanje paljenicÄa, okajnicÄa i naknadnicÄa.
Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
40 I s vanjske strane onomu tko ulazi na ulaz sjevernih vrata bijahu dva stola; i s druge strane, prema trijemu vrata, dva stola.
Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
41 Četiri stola, dakle, s jedne, a četiri stola s druge strane vrata: u svemu osam stolova, na kojima se klahu žrtve.
Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
42 Osim toga, četiri stola za paljenice, od klesanoga kamena. Bili su po lakat i pol široki i lakat visoki. Na njima je stajao pribor za klanje žrtava paljenica i klanica.
Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
43 Stolovi bijahu sve uokolo obrubljeni žljebićima od jednoga dlana, zavrnutima unutra. Na stolove se stavljalo žrtveno meso.
Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
44 Zatim me povede u unutrašnje predvorje. U unutrašnjem predvorju bijahu dvije prostorije: jedna bijaše sa strane sjevernih vrata, okrenuta prema jugu, a druga sa strane južnih vrata, okrenuta prema sjeveru.
Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
45 I on mi reče: “Ta prostorija što je okrenuta na jug određena je za svećenike koji obavljaju službu u Domu.
Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
46 A prostorija što je okrenuta na sjever jest za svećenike koji obavljaju službu na žrtveniku. To su sinovi Sadokovi, oni između sinova Levijevih koji smiju prići k Jahvi da mu služe!”
nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
47 On izmjeri predvorje. Dužina: sto lakata, širina: sto lakata; bijaše četverouglasto. Pred Domom stajaše žrtvenik.
Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
48 A zatim me povede k trijemu. Izmjeri polustupove trijema: bijaše pet lakata na jednoj i pet lakata na drugoj strani. Vrata bijahu široka tri lakta s jedne i tri lakta s druge strane.
Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
49 Trijem bijaše dugačak dvadeset lakata, a širok dvanaest lakata. Deset je stepenica vodilo onamo. Na dovratnicima s jedne i s druge strane stajaše po jedan stup.
Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.

< Ezekiel 40 >